< Yohana 16 >
1 “Nimewaambieni hayo kusudi msiiache imani yenu.
我給你們講論了這些事,免得你們的信仰動搖。
2 Watu watawatenga ninyi na masunagogi yao. Tena, wakati unakuja ambapo kila atakayewaua ninyi atadhani anamhudumia Mungu.
人要把你們逐出會堂;並且時候必到,凡殺害你們的,還以為是盡恭敬天主的義務。
3 Watawatendeeni mambo hayo kwa sababu hawamjui Baba, wala hawanijui mimi.
他們這樣做,是因為沒有認識父,父也沒有認識我。
4 Basi, nimewaambieni mambo haya ili saa yake itakapofika mkumbuke kwamba niliwaambieni. “Sikuwaambieni mambo haya tangu mwanzo kwa sababu nilikuwa pamoja nanyi.
我給你們講論了這一切,是為叫你們在這一切發生時,想起我早就告訴了你們這一切。這些事起初我沒有告訴你們,因為我還與你們同在。」
5 Lakini sasa namwendea yule aliyenituma; na hakuna hata mmoja wenu anayeniuliza: Unakwenda wapi?
「現在我就往派遣我者那那裏去,你們中卻沒有人問我: 你往那裏去?
6 Kwa kuwa nimewaambieni mambo hayo mmejaa huzuni mioyoni mwenu.
只因我給你們說了這話,你們就滿心憂悶。
7 Lakini, nawaambieni ukweli: afadhali kwenu mimi niende zangu, maana nisipokwenda Msaidizi hatakuja kwenu. Lakini nikienda, basi, nitamtuma kwenu.
然而,我將真情告訴你們:我去為你們有益,因為我若不去,護慰者便不會到你們這裏來;我若去了,就要派遣他到你們這裏來。
8 Naye atakapokuja atawathibitishia walimwengu kwamba wamekosea kuhusu dhambi, uadilifu na hukumu ya Mungu.
當他來到時,就要指證世界關於罪惡、正義和審判所犯的錯誤:
9 Wamekosea kuhusu dhambi kwa sababu hawaniamini;
關於罪惡,因為他們沒有信從我;
10 kuhusu uadilifu, kwa sababu naenda zangu kwa Baba, nanyi hamtaniona tena;
關於正義,因為我往父那裏去,而你們再見不到我;
11 kuhusu hukumu kwa sababu mkuu wa ulimwengu huu amekwisha hukumiwa.
關於審判,因為這世界的首領已被判斷了。
12 “Ninayo bado mengi ya kuwaambieni, ila kwa sasa hamwezi kuyastahimili.
我本來還有許多事要告訴你們,然而你們現在不能擔負。
13 Lakini atakapokuja huyo Roho wa kweli atawaongoza kwenye ukweli wote; maana hatasema kwa mamlaka yake mwenyewe, bali atawaambieni yote atakayosikia, na atasema mambo yatakayokuwa yanakuja.
當那一位真理之神來時,他要把你們引入一切真理,因為他不憑自己講論,只把他所聽到的講出來,並把未來的事傳告你們。
14 Yeye atanitukuza mimi kwa kuwa atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
他要光榮我,因為他要把由我所領受的,傳告給你們。
15 Vyote alivyo navyo Baba ni vyangu; ndiyo maana nimesema kwamba huyo Roho Mtakatifu atawaambieni yale atakayopata kutoka kwangu.
凡父所有的一切,都是我的;為此我說:他要由我領受而傳告給你們。」
16 “Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona!”
「只有片時,你們就看不見我了;再過片時,你們又要看見我。」
17 Hapo baadhi ya wanafunzi wake wakaulizana, “Ana maana gani anapotwambia: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona? Tena anasema: Kwa kuwa ninakwenda kwa Baba!”
於是他門徒中有幾個彼此說: 「他給我們所說的:『只有片時,你們就看不見我了;再過片時,你們又要看見我。』還有『我往父那裏去』,是什麼意思?」
18 Basi, wakawa wanaulizana, “Ana maana gani anaposema: Bado kitambo kidogo? Hatuelewi anaongelea nini.”
又說: 「他說的『這只有片時』,究竟有什麼意思?我們不明白他講什麼。」
19 Yesu alijua kwamba walitaka kumwuliza, basi akawaambia, “Je, mnaulizana juu ya yale niliyosema: Bado kitambo kidogo nanyi hamtaniona; na baada ya kitambo kidogo tena mtaniona?
耶穌看出他們願意問他,就對他們說: 「你們不是彼此詣問我所說的: 『只有片時,你們就看不見我了;再過片時,你們又要看見我』的話嗎?
20 Nawaambieni kweli, ninyi mtalia na kuomboleza, lakini ulimwengu utafurahi: mtaona huzuni lakini huzuni yenu itageuka kuwa furaha.
我實實在在告訴你們: 你們要痛哭,哀號,世界卻要歡樂;你們將要憂愁,但你們的憂愁卻要變為喜樂。
21 Wakati mama anapojifungua huona huzuni kwa sababu saa ya maumivu imefika; lakini akisha jifungua hayakumbuki tena maumivu hayo kwa sababu ya furaha kwamba mtu amezaliwa duniani.
婦女生產的時候,感到憂苦,因為她的時辰來到了;既生了孩子,因了喜樂再不記憶那苦楚了,因為一個人已生在世上了。
22 Ninyi pia mna huzuni sasa; lakini nitawajieni tena, nanyi mtajaa furaha mioyoni mwenu, na furaha hiyo hakuna mtu atakayeiondoa kwenu.
如今,你們固然感到憂愁,但我們要再見到你們,那時,你們心裏要喜樂,並且你們的喜樂誰也不能從你們奪去。
23 Siku hiyo hamtaniomba chochote. Kweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu, atawapeni.
那一天,你們什麼也不必問我了。我實實在在告訴你們:你們因我的名無論向父求什麼,他必賜給你們。
24 Mpaka sasa hamjaomba chochote kwa jina langu. Ombeni nanyi mtapata ili furaha yenu ikamilike.
直到現在,你們沒有因我的名求什麼;求罷!必會得到,好使你們的喜樂得以圓滿。」
25 “Nimewaambieni mambo hayo kwa mafumbo. Lakini wakati utakuja ambapo sitasema tena nanyi kwa mafumbo, bali nitawaambieni waziwazi juu ya Baba.
「我用比喻對你們講了這一切;但時候來到,我不用比喻對你們說話,而要明明地向你們傳報有關父的一切。
26 Siku hiyo mtaomba kwa jina langu, na siwaambii kwamba nitamwomba Baba kwa niaba yenu;
在那一天,你們要因我的名祈求,我不向你們說: 我要為你們求父,
27 maana yeye mwenyewe anawapenda ninyi, kwa sababu ninyi mmenipenda mimi na mmeamini kwamba nimetoka kwa Mungu.
因為父愛你們,因你們愛了我,且相信我出自天主。
28 Mimi nilitoka kwa Baba, nikaja ulimwenguni; na sasa nauacha ulimwengu na kurudi kwa Baba.”
我出自父,來到了世界上;我又離開世界,往父那裏去。」
29 Basi, wanafunzi wake wakamwambia, “Ahaa! Sasa unasema waziwazi kabisa bila kutumia mafumbo.
他的門徒便說:「看,現在你明明地講論,不用什麼比喻了。
30 Sasa tunajua kwamba wewe unajua kila kitu, na huna haja ya kuulizwa maswali na mtu yeyote; kwa hiyo tunaamini kwamba umetoka kwa Mungu.”
現在,我們曉得你知道一切,不需要有人問你;因此,我們相信你是出自天主。」
31 Yesu akawajibu, “Je, mnaamini sasa?
耶穌回答說: 「現在你們相信嗎?
32 Wakati unakuja, tena umekwisha fika, ambapo ninyi nyote mtatawanyika kila mtu kwake, nami nitaachwa peke yangu. Kumbe, lakini mimi siko peke yangu, maana Baba yu pamoja nami.
看,時辰要來,且己來到,你們要被驅散,各人歸各人的地方去,撇下我獨自一個,其實我不是獨自一個,因為有父與我同在。
33 Nimewaambieni mambo haya ili mpate kuwa na amani katika kuungana nami. Ulimwenguni mtapata masumbuko; lakini jipeni moyo! Mimi nimeushinda ulimwengu!”
我給你們講了這一切,是要你們在我內得到平安。在世界上你們要受苦難;然而你們放心,我已戰勝了世界。」