< Yohana 19 >

1 Basi, Pilato akaamuru Yesu achukuliwe, apigwe viboko.
時,比拉多命人把耶穌帶去鞭打了。
2 Nao askari wakasokota taji ya miiba, wakamtia kichwani, wakamvika na joho la rangi ya zambarau.
然後兵士們用荊棘編了個茨冠,放在他頭上,給他披上一件紫紅袍,
3 Wakawa wanakuja mbele yake na kusema: “Shikamoo, Mfalme wa Wayahudi!” Wakampiga makofi.
來到他跟前說: 「猶太人的君王,萬歲! 」並給他耳光。
4 Pilato akatoka tena nje, akawaambia, “Tazameni, namleta nje kwenu, mpate kujua kwamba mimi sikuona hatia yoyote kwake.”
比拉多又出去到外面,向他們說:「看,我給你們領出他來,為叫你們知道我在他身上查不出什麼罪狀。」
5 Basi, Yesu akatoka nje amevaa taji ya miiba na joho la rangi ya zambarau. Pilato akawaambia, “Tazameni! Mtu mwenyewe ni huyo.”
於是耶穌帶著茨冠,披著紫紅袍出來了;比拉多就對他們說: 「看,這個人! 」
6 Makuhani wakuu na walinzi walipomwona wakapaaza sauti: “Msulubishe! Msulubishe!” Pilato akawaambia, “Mchukueni basi, ninyi wenyewe mkamsulubishe, kwa maana mimi sikuona hatia yoyote kwake.”
司祭長和差役們一看見耶穌,就喊說: 「釘在十字架上!釘他在十字架上! 」比拉多對他們說: 「你們把他帶去,釘在十字架上罷! 我在他身上查不出什麼罪狀。」
7 Wayahudi wakamjibu, “Sisi tunayo Sheria, na kufuatana na Sheria hiyo, ni lazima afe, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu.”
猶太答覆他說: 「我們有法律,按法律他應該死,因為他自充為天主子。」
8 Pilato aliposikia maneno hayo akazidi kuogopa.
比拉多聽了這話,越發害怕,
9 Basi, akaingia tena ndani ya ikulu, akamwuliza Yesu, “Umetoka wapi wewe?” Lakini Yesu hakumjibu neno.
遂又進了總督府,對耶穌說:「你到底是那裏的?」耶穌卻沒有回答他。
10 Hivyo Pilato akamwambia, “Husemi nami? Je, hujui kwamba ninayo mamlaka ya kukufungua na mamlaka ya kukusulubisha?”
於是比拉多對他說: 「你對我也不說話嗎?你不知道我有權柄釋放你,也有權柄釘你在十字架上嗎?」
11 Yesu akamjibu, “Hungekuwa na mamlaka yoyote juu yangu kama hungepewa na Mungu. Kwa sababu hiyo, yule aliyenikabidhi kwako ana dhambi kubwa zaidi.”
耶穌答說: 「若不是由上賜給你,你對我什麼權柄也沒有;為此,把我交付給你的人,負罪更大。」
12 Tangu hapo, Pilato akawa anatafuta njia ya kumwachilia, lakini Wayahudi wakapiga kelele: “Ukimwachilia huyu mtu, wewe si rafiki yake Kaisari; kila mtu anayejifanya kuwa Mfalme humpinga Kaisari!”
從此,比拉多設法要釋放耶穌,猶太人卻喊說: 「你如果釋放這人,你就不是凱撒的朋友,因為凡自充為王的,就是背叛凱撒。」
13 Basi, Pilato aliposikia maneno hayo akamleta Yesu nje, akaketi juu ya kiti cha hukumu, mahali paitwapo: “Sakafu ya Mawe” (kwa Kiebrania, Gabatha).
比拉多耶穌一聽這話,就把耶穌領出來,到了一一個名叫「石鋪地」──希伯來話叫「加巴達」的地方,坐在審判座位上。
14 Ilikuwa yapata saa sita mchana, siku ya maandalio ya Pasaka. Pilato akawaambia Wayahudi, “Tazameni, Mfalme wenu!”
時值逾越節的預備日,約莫第六時辰,比拉多對猶太人說:「看,你們的君王! 」
15 Wao wakapaaza sauti: “Mwondoe! Mwondoe! Msulubishe!” Makuhani wakuu wakajibu, “Sisi hatuna Mfalme isipokuwa Kaisari!”
他們就喊叫說: 「除掉,除掉,釘他在十字架上! 」比拉多對他們說: 「要我把你們的君王在十字架上嗎?」司祭長答說: 「除了凱撒,我們沒有君王。」
16 Basi, hapo Pilato akamtia Yesu mikononi mwao ili asulubiwe. Basi, wakamchukua Yesu.
於是比拉多把耶穌交給他們去釘死。他們就把耶穌帶去了。
17 Naye akatoka akiwa amejichukulia msalaba wake kwenda mahali paitwapo “Fuvu la Kichwa”, (kwa Kiebrania Golgotha).
耶穌自己背著十字架出來,到了一個名叫「髑髏」的地方,希伯來話叫「哥耳哥達」,
18 Hapo ndipo walipomsulubisha, na pamoja naye waliwasulubisha watu wengine wawili; mmoja upande wake wa kulia na mwingine upande wake wa kushoto, naye Yesu katikati.
他們就在那裏把他釘在十字架上,同他一起另有兩個人: 一個在這邊,一個在那邊,耶穌在中間。
19 Pilato aliandika ilani akaiweka juu ya msalaba. Nayo ilikuwa imeandikwa hivi: “Yesu wa Nazareti, Mfalme wa Wayahudi.”
比拉多寫個牌子,放在十字架上端,寫的是:「納匝肋人耶穌,猶太人的君王。」
20 Wayahudi wengi waliisoma ilani hiyo, maana mahali hapo aliposulubiwa Yesu palikuwa karibu na mji. Tena ilani hiyo ilikuwa imeandikwa kwa Kiebrania, Kilatini, na Kigiriki.
這牌子有許多猶太人唸了,因為耶穌被在十字架上的地方離城很近,是用希伯來、羅馬和希臘文寫的。
21 Basi, makuhani wakuu wakamwambia Pilato, “Usiandike: Mfalme wa Wayahudi, ila Yeye alisema, Mimi ni Mfalme wa Wayahudi.”
於是猶太人的司祭長就對比拉多說: 「不要寫猶太人的君王,該寫他自己說: 我是猶太人的君王。」
22 Pilato akajibu, “Niliyoandika, nimeandika!”
比拉多答覆說:「我寫了,就寫了。」
23 Askari walipokwisha msulubisha Yesu, walizichukua nguo zake, wakazigawa mafungu manne, fungu moja kwa kila askari. Walichukua pia na kanzu yake; kanzu hiyo ilikuwa imefumwa kwa kipande kimoja tu, bila mshono.
兵士將耶穌釘在十字架上後,拿了他的衣服,分成四分,每人一分;又拿了長衣,因那長衣是無縫的,由上到下渾然織成,
24 Basi, hao askari wakashauriana: “Tusiipasue, ila tuipigie kura itakuwa ya nani.” Jambo hilo lilifanyika ili yatimie Maandiko Matakatifu yasemayo: “Waligawana mavazi yangu, na nguo yangu wakaipigia kura.” Basi, ndivyo walivyofanya hao askari.
所以他們彼此說: 「不要把它們撕開,我們擲骰,看是誰的。」這就應驗了經上的話『他們瓜分了我的衣服,為我的長衣,他們拈鬮。』士兵果然這樣作了。
25 Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene.
在耶穌的十字架旁,站著他的母親和他母親的姊妹,還有克羅帕的妻子瑪利亞和瑪利亞瑪達肋納。
26 Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: “Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao.”
耶穌看見母親,又看見他所愛的門徒站在旁邊,就對母親說: 「女人,看你的兒子! 」
27 Halafu akamwambia yule mwanafunzi: “Tazama, huyo ndiye mama yako.” Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
然後又對那門徒說: 「看,你的母親! 」就從那時起,那門徒把她接到自己家裏。
28 Yesu alijua kwamba yote yalikuwa yametimia; na, ili Maandiko Matakatifu yapate kutimia, akasema, “Naona kiu.”
此後,耶穌因知道一切事都完成了,為應驗經上的話,遂說: 『我渴。』
29 Hapo palikuwa na bakuli limejaa siki. Basi, wakachovya sifongo katika hiyo siki, wakaitia juu ya ufito wa husopo, wakamwekea mdomoni.
有一個盛滿了醋的器皿放在那裏,有人便將海綿浸滿了醋,綁在長槍上,送到的口邊。
30 Yesu alipokwisha pokea hiyo siki, akasema, “Yametimia!” Kisha akainama kichwa, akatoa roho.
耶穌一嚐了那醋,便說: 「完成了。」就低下頭,交付了靈魂。
31 Ilikuwa Ijumaa, siku ya Maandalio. Kwa hiyo, kusudi miili isikae msalabani siku ya Sabato, maana siku hiyo ya Sabato ilikuwa siku kubwa, Wayahudi walimwomba Pilato miguu ya hao waliosulubiwa ivunjwe na miili yao iondolewe.
猶太人因那日子是預備日,免得安息日內──那安息日原是個大節日──屍首留在十字架上,就來請求比拉多打斷他們的腿,把他們拿去。
32 Basi, askari walikwenda, wakaivunja miguu ya yule mtu wa kwanza na yule wa pili ambao walikuwa wamesulubiwa pamoja na Yesu.
士兵遂前來,把第一個人的,並與耶穌同釘在十字架上的第二個人的腿打斷了。
33 Lakini walipomfikia Yesu waliona kwamba alikwisha kufa, na hivyo hawakumvunja miguu.
可是,及至來到耶穌跟前,看見他已經死了,就沒有打斷他的腿;
34 Lakini askari mmoja alimtoboa ubavuni kwa mkuki, na mara ikatoka damu na maji.
但是,有一個兵士用槍刺透了他的肋旁,立刻流出了血和水。
35 (Naye aliyeona tukio hilo ametoa habari zake ili nanyi mpate kuamini. Na hayo aliyosema ni ukweli, tena yeye anajua kwamba anasema ukweli.)
那看見這事的人就作證,而他的見證是真實的;並且「那位」知道他所說的是真實的,為叫你們也相信。
36 Jambo hilo lilitendwa ili Maandiko Matakatifu yatimie: “Hapana hata mfupa wake mmoja utakaovunjwa.”
這此事發生,正應驗了經上的話說: 『不可將他的骨頭打斷。』
37 Tena Maandiko mengine yanasema: “Watamtazama yule waliyemtoboa.”
經上另有一句說: 『他們要瞻望他們所刺透的。』
38 Baada ya hayo, Yosefu, mwenyeji wa Armathaya, alimwomba Pilato ruhusa ya kuuchukua mwili wa Yesu. (Yosefu alikuwa mfuasi wa Yesu, lakini kwa siri, maana aliwaogopa viongozi wa Wayahudi). Basi, Pilato akamruhusu. Hivyo Yosefu alikwenda, akauondoa mwili wa Yesu.
這些事以後,阿黎瑪特雅人若瑟──他因怕猶太人,暗中作了耶穌的門徒──來求比拉多,為領取耶穌的遺體;比拉多允許了。於是他來把耶穌的遺體領去了。
39 Naye Nikodemo ambaye hapo awali alikuwa amemwendea Yesu usiku, akaja akiwa amechukua mchanganyiko wa manemane na ubani kiasi cha kilo thelathini.
那以前夜間來見耶穌的尼苛德摩也來了,帶著沒藥及沉香調和的香料,約有一百斤。
40 Basi, waliutwaa mwili wa Yesu, wakaufunga sanda pamoja na manukato kufuatana na desturi ya Wayahudi katika kuzika.
他們取下了耶穌的遺體,照猶太人埋葬的習俗,用殮布和香料把他裹好。
41 Mahali hapo aliposulubiwa Yesu palikuwa na bustani, na katika bustani hiyo kulikuwa na kaburi jipya ambalo hakutiwa bado mtu yeyote ndani yake.
在耶穌被在十字架上的地方,有一個園子,那園子裏有一座新墳墓,裏面還沒有安葬過人。
42 Basi, kwa sababu ya shughuli za Wayahudi za maandalio ya Sabato, na kwa vile kaburi hilo lilikuwa karibu, wakamweka Yesu humo.
只因是猶太人的預備日,墳墓又近,就在那裏安葬了耶穌。

< Yohana 19 >