< Yohana 15 >
1 “Mimi ni mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
我是真葡萄樹,我父是園丁。
2 Yeye huliondoa ndani yangu kila tawi lisilozaa matunda, na kila tawi lizaalo hulisafisha lipate kuzaa zaidi.
凡在我身上不結實的枝條,他便剪掉;凡結實的,他就清理,使他結更多的果實;
3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya ule ujumbe niliowaambieni.
你們因我對你們所講的話,已是清潔的了。
4 Kaeni ndani yangu, nami nikae ndani yenu. Tawi haliwezi peke yake kuzaa matunda lisipokaa katika mzabibu hali kadhalika nanyi hamwezi kuzaa matunda msipokaa ndani yangu.
你們住在我內,我也住在你們內。正如枝條若不留在葡萄樹上,憑自己不能結實;你們若不住在我內,也一無所能。
5 “Mimi ni mzabibu, nanyi ni matawi yake. Akaaye ndani yangu, nami ndani yake, huyo atazaa matunda mengi, maana bila mimi hamwezi kufanya chochote.
我是葡萄樹,你們是枝條;那住在我內,我也住在他內的,他就結許多的果實,因為離了我,你們什麼也不能做。
6 Mtu yeyote asipokaa ndani yangu hutupwa nje kama tawi litupwalo nje hata likakauka. Watu huliokota tawi la namna hiyo na kulitupa motoni liungue.
誰若不住在我內,便彷彿枝條,丟在外面而枯乾了,人便把它拾起來,投入火中焚燒。
7 Mkikaa ndani yangu na maneno yangu yakikaa ndani yenu, basi, ombeni chochote mtakacho nanyi mtapewa.
你們如果住在我內,而我的話也存在你們內,如此,你們願意什麼,求罷!必給你們成就。
8 Baba yangu hutukuzwa kama mkizaa matunda mengi na kuwa wanafunzi wangu.
我父受光榮,即在於你們多結果實,如此你們就成為我的門徒。
9 Mimi nimewapenda ninyi kama vile Baba alivyonipenda mimi. Kaeni katika pendo langu.
正如父愛了我,同樣我也愛了你們;你們應存在我的愛內。
10 Mkizishika amri zangu mtakaa katika pendo langu, kama vile nami nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.
如果你們遵守我的命令,便存在我的愛內,如我遵守了我父[命令而存在他的愛內一樣。
11 Nimewaambieni mambo haya ili furaha yangu ikae ndani yenu, na furaha yenu ikamilike.
我對你們講論了這些事,為使我的喜樂存在你們內,使你們的喜樂圓滿無缺。」
12 Hii ndiyo amri yangu: pendaneni; pendaneni kama nilivyowapenda ninyi.
這是我的命令: 你們該彼些相愛,如同我愛了你們一樣。
13 Hakuna upendo mkuu zaidi kuliko upendo wa mtu atoaye uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.
人若為自己的朋友捨掉性命,再沒有比這更大的愛情了。
14 Ninyi ni rafiki zangu mkifanya ninayowaamuru.
你們如果實行我所命令你們的,你們就是我的朋友。
15 Ninyi siwaiti tena watumishi, maana mtumishi hajui anachofanya bwana wake. Lakini mimi nimewaita ninyi rafiki, kwa sababu nimewajulisha yote ambayo nimeyasikia kutoka kwa Baba yangu.
我不再稱你們為僕人,因為僕人不知道他主人所做的事。我稱你們為朋友,因為凡由我父聽來的一切,我都顯示給你們了。
16 Ninyi hamkunichagua mimi; mimi niliwachagueni na kuwatuma mwende mkazae matunda, matunda yadumuyo, naye Baba apate kuwapa ninyi chochote mumwombacho kwa jina langu.
不是你們揀選了我,而是我揀選了你們,並派你們去結果實,去結常存的果實;如此,你們因我的名無論向求什麼,他必賜給你們。
17 Basi, amri yangu kwenu ndiyo hii: pendaneni.
這就是我命令你們的:你們應該此相愛。」
18 “Kama ulimwengu ukiwachukia ninyi, kumbukeni kwamba umenichukia mimi kabla haujawachukia ninyi.
「世界若恨你們,你們該知道,在你們以前,它已恨了我。
19 Kama mngalikuwa watu wa ulimwengu, ulimwengu ungaliwapenda ninyi kama watu wake. Lakini kwa vile ninyi si wa ulimwengu, ila mimi nimewachagueni kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukieni.
若是你們屬於世界,世界必喜愛你們,有如屬於自己的人;但因你們不屬於世界,而是我從世界中揀選了你們,為此,世界才恨你們。
20 Kumbukeni niliyowaambieni: mtumishi si mkuu zaidi kuliko bwana wake. Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa na ninyi pia; kama wameshika neno langu, watalishika na lenu pia.
你們要記得我對你們所說過的話:沒有僕人大過主人的;如果人們迫害了我,也要迫害你們;如果他們遵守了我的話,也要遵守你們的。
21 Lakini hayo yote watawatendeeni ninyi kwa sababu ya jina langu, kwani hawamjui yeye aliyenituma.
但是,他們為了我名字的緣故,要向你們做這一切,因為他們不認識那派遣我來的。
22 Kama nisingalikuja na kusema nao wasingalikuwa na hatia; lakini sasa hawawezi kujitetea kwamba hawana dhambi.
假使我沒有來,沒有教訓他們,他們就沒有罪;但現在他們對自己的罪,是無可推諉。
23 Anayenichukia mimi, anamchukia na Baba yangu pia.
恨我的,也恨我的父。
24 Kama nisingalifanya kwao mambo ambayo hakuna mtu mwingine amekwisha yafanya wasingalikuwa na hatia; lakini sasa wameona niliyoyafanya wakinichukia mimi, wakamchukia na Baba yangu pia.
假使我在他們中沒有做過其他任何人從未做過的事業,他們便沒有罪;然而,現在他們看見了卻仍恨了我和我父。
25 Na hivi ni lazima yatimie yale yaliyoandikwa katika Sheria yao: Wamenichukia bure!
但這是為應驗他們法律上所記載的話: 『他們無故地惱恨了我。』
26 “Atakapokuja huyo Msaidizi nitakayemtuma kwenu kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia mimi.
當護慰者,就是我從父那裏要給你們派遣的,那發於父的真理之神來到時,他必要為我作證;
27 Nanyi pia mtanishuhudia kwa kuwa mmekuwa nami tangu mwanzo.
並且你們也要作證,因為你們從開始就和我在一起。」