< Luka 21 >

1 Yesu alitazama akawaona wanaume matajiri waliokuwa wanaweka zawadi zao kwenye hazina.
And having looked up, he saw the rich casting their gifts into the treasury.
2 Akamuona mjane mmoja masikini akiweka senti zake mbili.
And he also saw a certain poor widow there casting in two mites.
3 Hivyo akasema, “Kweli nawaambieni, huyu Mjane maskini ameweka nyingi kuliko wengine wote.
And he said, Truly I say to you, that this poor widow cast in more than they all.
4 Hawa wote wametoa hizi zawadi kutoka katika vingi walivyonavyo. Lakini huyu mjane, katika umaskini wake, ametoa fedha zote alizokuwa nazo kwa ajili ya kuishi kwake.”
For all these cast into the offerings of God from their abundance, but this woman from her poverty cast in all the living that she had.
5 Wakati wengine walipokuwa wakisema juu ya hekalu, namna lilivyokuwa limepambwa na mawe mazuri na matoleo, alisema,
And as some spoke about the temple, that it was adorned with fine stones and gifts, he said,
6 “Kwa habari ya mambo haya mnayoyaona, siku zitakuja ambazo hakuna jiwe moja ambalo litaachwa juu ya jiwe jingine ambalo halitabomolewa.”
These things that ye see, the days will come during which there will not be left a stone upon a stone that will not be thrown down.
7 Hivyo wakamuuliza, wakasema, “Mwalimu, mambo haya yatatokea lini? Na nini ni itakuwa ishara kwamba haya mambo yako karibu kutokea?”
And they questioned him, saying, Teacher, when therefore will these things be? And what is the sign when these things are going to happen?
8 Yesu akajibu, “Muwe waangalifu kwamba msidanganywe. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema, 'Mimi ndiye, 'na 'Muda umekaribia'. Msiwafuate.
And he said, Watch that ye may not be led astray, for many will come in my name, saying, I am, and, The time has come near. Go ye not therefore after them.
9 Mkisikia vita na vuruguvurugu msiogope, kwa sababu haya mambo lazima yatokee kwanza, lakini mwisho hautatokea upesi.”
And when ye may hear of wars and tumults, do not be alarmed, for these things must first happen, but the end is not straightaway.
10 Kisha akawaambia, “Taifa litainuka kupigana na taifa jingine, na ufalme juu ya ufalme mwingine.
Then he said to them, Nation will rise against nation, and kingdom against kingdom.
11 Kutakuwa na matetemeko makubwa, na njaa na tauni katika maeneo mbalimbali. Kutakuwa na matukio ya kutisha na ishara za kutisha kutoka mbinguni.
And great earthquakes will be in various places, and famines and plagues. And there will be fearful sights and great signs from the sky.
12 Lakini kabla ya mambo haya yote, wataweka mikono yao juu yenu na kuwatesa, kuwapeleka kwenye masinagogi na magereza, kuwaleta mbele za wafalme na wenye mamlaka kwa sababu ya jina langu.
But before all these things, they will throw their hands on you, and will persecute you, delivering you up to the synagogues and prisons, being brought before kings and rulers for my name's sake.
13 Hii itawafungulia fursa kwa ushuhuda wenu.
But it will go out from you for testimony.
14 Kwahiyo amueni mioyoni mwenu kutoandaa utetezi wenu mapema,
Settle therefore in your hearts not to premeditate to make defense.
15 kwa sababu nitawapa maneno na hekima, ambayo adui zenu wote hawataweza kuipinga au kuikana.
For I will give you a mouth and wisdom that all those who oppose you will not be able to contradict or to resist.
16 Lakini mtakataliwa pia na wazazi wenu, ndugu zenu, jamaa zenu na rafiki zenu, na watawaua baadhi yenu.
And ye will be betrayed even by parents, and kinsmen, and friends, and brothers. And some of you they will condemn to death.
17 Mtachukiwa na kila mmoja kwa sababu ya jina langu.
And ye will be hated by all men because of my name.
18 Lakini hakuna hata unywele mmoja wa vichwa vyenu utakaopotea.
And, no, not a hair of your head will perish.
19 Katika kuvumilia mtaziponya nafsi zenu.
In your perseverance ye gain your souls.
20 Mtakapoona Yerusalemu imezungukwa na majeshi, basi jueni kwamba uharibifu wake umekaribia.
But when ye see Jerusalem surrounded by armies, then know that the desolation of it has come near.
21 Hapo wale walioko Yudea wakimbilie milimani, na wale walioko katikati ya jiji waondoke, na msiwaache walioko vijijini kuingia.
Then let those in Judea flee to the mountains, and let those in the midst of it depart out, and let not those in the rural areas enter into it.
22 Maana hizi ni siku za kisasi, ili kwamba mambo yote yaliyoandikwa yapate kutimilika.
Because these are days of vengeance to fulfill all things that are written.
23 Ole ni kwa wale walio na mimba na kwa wale wanyonyeshao katika siku hizo! Kwa maana kutakuwa na adha kuu juu ya nchi, na ghadhabu kwa watu hawa.
But woe to those who have in the womb, and to those who suckle in those days. For there will be great distress upon the land, and wrath to this people.
24 Na wataanguka kwa ncha ya upanga na watachukuliwa mateka kwa mataifa yote, na Yerusalem itakanyagwa na watu wa mataifa, mpaka wakati wa watu wa mataifa utakapotimilika.
And they will fall by the jaw of the sword, and will be led away captive into all the nations. And Jerusalem will be trampled down by the Gentiles until the times of the Gentiles are fulfilled.
25 Kutakuwa na ishara katika jua, mwezi na nyota. Na katika nchi kutakuwa na dhiki ya mataifa, katika kukata tamaa kutokana na mlio wa bahari na mawimbi.
And there will be signs in sun and moon and stars, and upon the earth distress of nations, with perplexity, roaring of sea and of tossing,
26 Kutakuwa na watu wakizimia kwa hofu na katika kutarajia mambo yatakoyo tokea juu ya dunia. Kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
fainting of men from fear, and of anticipation of the things coming upon the world, for the powers of the heavens will be shaken.
27 Kisha watamwona Mwana wa Adamu akija mawinguni katika nguvu na utukufu mkuu.
And then they will see the Son of man coming in a cloud with power and much glory.
28 Lakini mambo haya yatakapoanza kutokea, simameni, inueni vichwa vyenu, kwa sababu ukombozi wenu umesogea karibu.”
And when these things begin to happen, stand upright, and lift up your heads, because your redemption approaches.
29 Yesu akawaambia kwa mfano, “Uangalieni mtini, na miti yote.
And he spoke a parable to them. Behold the fig tree, and all the trees.
30 Inapotoa machipukizi, mnajionea wenyewe na kutambua kwamba kiangazi tayari kiko karibu.
When they are now sprouting, ye know seeing for yourselves that summer is now near.
31 Vivyo hivyo, mnapoona mambo haya yanatokea, ninyi tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu umekaribia.
Even so ye, when ye see these things happening, know ye that the kingdom of God is near.
32 Kweli, nawaambieni, kizazi hiki hakitapita, mpaka mambo haya yote yatakapotokea.
Truly I say to you, that this generation will, no, not pass away until all things happen.
33 Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
The sky and the earth will pass away, but my words may, no, not pass away.
34 Lakini jiangalieni wenyewe, ili kwamba mioyo yenu isije ikalemewa na ufisadi, ulevi, na mahangaiko ya maisha haya. Kwa sababu ile siku itawajia ghafla
But take heed to yourselves, lest your hearts be weighed down in debauchery and drunkenness and mundane cares, and that day come upon you sudden.
35 kama mtego. Kwasababu itakuwa juu ya kila mmoja aishiye katika uso wa dunia nzima.
For it will come like a trap upon all those who sit upon the face of all the earth.
36 Lakini mwe tayari wakati wote, mwombe kwamba mtakuwa imara vya kutosha kuyaepuka haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele za Mwana wa Adamu.”
Watch ye therefore, making supplication at all times, so that ye may be considered worthy to escape all these things going to happen, and to stand before the Son of man.
37 Hivyo wakati wa mchana alikuwa akifundisha hekaluni na usiku alitoka nje, na kwenda kukesha katika mlima unaoitwa wa Mzeituni.
And during the days he was teaching in the temple, and going forth the nights, he lodged on the mount that is called Olives.
38 Watu wote walimjia asubuhi na mapemaili kumsikiliza ndani ya hekalu.
And all the people rose early in the morning to him in the temple to hear him.

< Luka 21 >