< Matendo 13 >
1 Sasa katika kanisa la Antiokia, palikuwa na baadhi ya manabii na walimu. Walikua Barnaba, Simeoni (aliyeitwa Nigeri). Lukio wa Kirene, Manaeni( ndugu asiye wa damu wa Herode kiongozi wa mkoa), na Sauli.
Now there were some men from the congregation that was in Antioch, prophets and teachers, including Barnabas, and Simeon called Niger, and Lucius the Cyrenian, and Manaen reared with Herod the tetrarch, and Saul.
2 Walipokuwa wakimwabudu Bwana na kufunga, Roho Mtakatifu alisema, “Niteengeeni pembeni Barnaba na Sauli, waifanye kazi niliyo waitia.”
And while they were serving the Lord, and fasting, the Holy Spirit said, Separate to me now Barnabas and Saul for the work that I have called them.
3 Baada ya Kanisa kufunga, kuomba, na kuweka mikono yao juu ya watu hawa, wakawaacha waende.
Then, having fasted and prayed and laid hands on them, they sent them away.
4 Kwa hiyo Barnabas na Sauli walimtii Roho Mtakatifu na walitelemka kuelekea Seleukia; Kutoka huko walisafiri baharini kuelekea kisiwa cha Kipro.
Indeed therefore these men, having been sent forth by the Holy Spirit, went down to Seleucia, and from there they sailed for Cyprus.
5 Walipokuwa katika mji wa Salami, walilitangaza neno la Mungu katika Masinagogi ya Wayahudi. Pia walikuwa pamoja na Yohana Marko kama msaidizi wao.
And after becoming in Salamis, they proclaimed the word of God in the synagogues of the Jews, and they also had John for a helper.
6 Walipokwenda katika kisiwa chote mpaka Pafo, walikuta mtu fulani mchawi, Myahudi nabii wa uongo, ambaye jina lake lilikuwa Bar Yesu.
And after going through the island as far as Paphos, they found a certain sorcerer, a Jewish false prophet, whose name was Bar-jesus,
7 Mchawi huyu alishirikiana na Liwali Sergio Paulus, aliyekuwa mtu mwenye akili. Mtu huyu aliwaalika Barnaba na Sauli, kwa sababu alihitaji kusikia neno la Mungu.
who was with the proconsul, Sergius Paulus, an intelligent man. This man, having summoned Barnabas and Saul, sought to hear the word of God.
8 Lakini Elima “yule mchawi” (hivyo ndivyo jina lake lilivyo tafsiriwa) aliwapinga; alijaribu kumgeuza yule liwali atoke kwenye imani.
But Elymas the sorcerer (for so his name is translated) opposed them, seeking to deviate the proconsul from the faith.
9 Lakini Sauli aliyeitwa Paulo, alikuwa amejazwa na Roho Mtakatikfu, akamkazia macho
But Saul (the man is also Paul) having been filled with the Holy Spirit, and having gazed on him,
10 na akasema “Ewe mwana wa Ibilisi, umejazwa na aina zote za udanganyifu na udhaifu. Wewe ni adui wa kila aina ya haki. Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?
said, O man full of all deceit and all recklessness, thou son of the devil, thou enemy of all righteousness, will thou not cease distorting the straight ways of the Lord?
11 Sasa tazama, mkono wa Bwana upo juu yako, na utakuwa kipofu. Hautaliona Jua kwa muda” mara moja ukungu na giza vilianguka juu ya Elimas; alianza kuzunguka pale akiomba watu wamwongoze kwa kumshika mkono.
And now, behold, a hand of the Lord is upon thee, and thou will be blind, not seeing the sun until a time. And immediately there fell on him gloom and darkness, and going around he sought hand-guides.
12 Baada ya liwali kuona kilichotokea, aliamini, kwa sababu alishangazwa kwa mafundisho kuhusu Bwana.
Then the proconsul, who saw that which happened, believed, being astonished at the doctrine of the Lord.
13 Sasa Paulo na rafiki zake walisafiri majini kutoka Pafo na wakafika Perge katika Pamfilia. Lakini Yohana aliwaacha na kurudi Yerusalemu.
Now those around Paul, having launched from Paphos, they came to Perga in Pamphylia. But John, having departed from them, returned to Jerusalem.
14 Paulo na rafiki yake walisafiri kutoka Perge na wakafika Antiokia ya Pisidia. Huko walikwenda katika sinagogi siku ya Sabato na kukaa chini.
And they, having passed through from Perga, arrived at Antioch of Pisidia, and after entering into the synagogue on the sabbath day, they sat down.
15 Baada ya kusoma sheria na manabii, viongozi wa sinagogi aliwatumia ujumbe wakisema, “Ndugu, kama mnao ujumbe wa kutia moyo watu hapa, semeni”
And after the reading of the law and the prophets the synagogue rulers sent to them, saying, Men, brothers, if there is among you a word of exhortation for the people, speak.
16 Kwa hiyo Paulo alisimama na kuwapungia mkono; alisema, “Wanaume wa Israeli na enyi mnao mtii Mungu, sikilizeni.
And Paul having stood up, and having motioned with the hand, he said, Men! Israelites and those who fear God, listen.
17 Mungu wa hawa watu wa Israeli aliwachagua baba zetu na kuwafanya watu wengi walipokaa katika nchi Misri, na kwa mkono wake kuinuliwa aliwaongoza nje yake.
The God of this people Israel chose our fathers, and raised up the people during the sojourn in the land of Egypt. And with a lofty arm he brought them out of it.
18 Kwa miaka arobaini aliwavumilia katika jangwa.
And for about a forty-year time he was patient with them in the wilderness.
19 Baada ya kuyaharibu mataifa saba katika nchi ya Kaanani, aliwapa watu wetu nchi yao kwa urithi.
And having destroyed seven nations in the land of Canaan, he allotted their land to them.
20 Matukio haya yote yalitokea zaidi ya miaka mia nne na hamsini. Baada ya vitu hivi vyote, Mungu aliwapa waamuzi mpaka Samweli Nabii.
And after these things he gave them judges about four hundred and fifty years until Samuel the prophet.
21 Baada ya haya, watu waliomba mfalme, hivyo Mungu aliwapa Sauli mwana wa Kishi, mtu wa kabila la Benjamini, kuwa mfalme kwa miaka arobaini.
And afterward they asked for a king, and God gave them Saul the son of Kish, a man of the tribe of Benjamin, for forty years.
22 Kisha baada ya Mungu kumuondoa katika ufalme, alimwinua Daudi kuwa mfalme wao. Ilikuwa ni kuhusu Daudi kwamba Mungu alisema, 'Nimempata Daudi mwana wa Yese kuwa mtu apendezwaye na moyo wangu; ambaye atafanya kila kitu nipendacho.'
And having removed him, he raised up David for a king to them, also about whom he said, when he testified, I have found David the son of Jesse, a man according to my heart, who will do all my purposes.
23 Kutoka kwenye ukoo wa mtu huyu Mungu ameiletea Israeli mkombozi, Yesu, kama alivyoahidi kufanya.
From this man's seed according to promise, God brought salvation to Israel,
24 Hili lilianza kutokea, kabla ya Yesu kuja, Yohana kwanza alitangaza ubatizo wa toba kwa watu wote wa Israeli.
John having earlier proclaimed, before his coming presence, the immersion of repentance to Israel.
25 Naye Yohana alipokuwa akimalizia kazi yake, alisema, 'Mwanifikiri mimi ni nani? mimi si yule. Lakini sikilizeni, ajaye nyuma yangu, sisitahili kulegeza viatu vya miguu yake.'
And as John was fulfilling his course, he said, Whom do ye suppose me to be? I am not, but behold, he comes after me of whom I am not worthy to loose the shoes of his feet.
26 Ndugu, watoto wa ukoo wa Abrahamu, na wale ambao kati yenu mnamwabudu Mungu, ni kwa ajili yetu kwamba ujumbe huu wa ukombozi umetumwa.
Men, brothers, sons of the race of Abraham, and those among you who fear God, to you the word of this salvation was sent.
27 Kwa wale waishio Yerusalemu, na watawala wao, hawakumtambua kwa uhalisia, na wala hawakuutambua ujumbe wa manabii ambao husomwa kila Sabato; kwa hiyo walitimiliza ujumbe wa manabii kwa kumhukumu kifo Yesu.
For those who dwell in Jerusalem, and their rulers, not having known this and the voices of the prophets being read at every sabbath, they fulfilled, having condemned him.
28 Japokuwa hawakupata sababu nzuri kwa kifo ndani yake, walimwomba Pilato amuue.
And not having found one cause of death in him, they asked for Pilate to kill him.
29 Walipomaliza mambo yote yaliyoandikwa kuhusu yeye, walimshusha kutoka mtini na kumlaza kaburini.
And when they completed all the things written about him, having taken him down from the tree, they laid him in a tomb.
30 Lakini Mungu alimfufua kutoka wafu.
But God raised him from the dead,
31 Alionekana kwa siku nyingi kwa wale waliokwenda pamoja naye kutoka Galilaya kuelekea Yerusalemu. Watu hawa sasa ni mashahidi wa watu.
who was seen for more days by those who came up with him from Galilee to Jerusalem, who are witnesses of him to the people.
32 Hivyo tunawaletea habari njema kuhusu ahadi walizopewa mababu zetu.
And we proclaim good news to you: the promise to the fathers, which happened because God has fulfilled this to us their children, having raised up Jesus,
33 Mungu aliweka ahadi hizi kwetu, watoto wao, katika hilo alimfufua Yesu na kumrudisha tena katika uhai. Hili pia liliandikwa katika Zaburi ya pili: 'Wewe ni Mwanangu, leo nimekuwa Baba yako'
as also it is written in the second psalm, Thou are my Son, today I have begotten thee.
34 Pia kuhusu ukweli ni kwamba alimfufua kutoka wafu ili kwamba mwili wake usiharibike, ameongea hivi: 'Nitakupatia utakatifu na baraka halisi za Daudi'
And because he raised him from the dead, no longer going to return to decay, he has spoken this way: I will give to you the faithful holy things of David.
35 Hii ndiyo sababu kasema pia katika zaburi nyingine, 'Hautaruhusu mtakatifu wako kuuona uozo.'
Therefore also he says in another, Thou will not give thy Holy Man to see decay.
36 Kwa kuwa baada ya Daudi kutumikia mapenzi ya Mungu katika kizazi chake, alilala, alilazwa pamoja na baba zake, na aliuona uaharibifu,
For indeed David, who served his own generation in the plan of God, became asleep, and was added near his fathers, and saw decay.
37 Lakini aliyefufuliwa na Mungu hakuuona uharibifu.
But he whom God raised up saw no decay.
38 Hivyo na ifahamike kwenu, ndugu, kupitia mtu huyu, msamaha wa dhambi umehubiriwa.
Be it known to you therefore, men, brothers, that through this man remission of sins is proclaimed to you.
39 Kwa yeye kila aaminiye anahesabiwa haki na mambo yote ambayo sheria ya Musa isingewapatia haki.
And from all things of which ye could not be make righteous by the law of Moses, in this man every man who believes is made righteous.
40 Hivyo basi kuweni waangalifu kwamba kitu walichokiongelea manabii kisitokee kwenu:
Watch therefore, lest that which is spoken in the prophets should come upon you:
41 'Tazama, enyi mnaodharau, na mkashangae na mkaangamie; kwa vile nafanya kazi katika siku zenu, Kazi ambayo hamwezi kuiamini, hata kama mtu atawaeleza.”
Behold, ye scoffers, and wonder, and perish, because I work a work in your days, which ye would, no, not believe, if some man should fully narrate it to you.
42 Wakati Paulo na Barnaba walipoondoka, watu wakawaomba waongee maneno haya siku ya Sabato ijayo.
And as they went out from the synagogue of the Jews, the Gentiles urged that these sayings be spoken to them the next sabbath.
43 Wakati mkutano wa sinagogi ulipokwisha, Wayahudi wengi na waongofu thabiti waliwafuata Paulo na Barnaba, ambao waliongea nao na waliwahimiza waendelee katika neema ya Mungu.
Now after the synagogue was dismissed, many of the Jews and of the devout proselytes followed Paul and Barnabas, who, while conversing, persuaded them to continue in the grace of God.
44 Sabato iliyofuata, karibu mji mzima ulikusanyika kusikia neno la Mungu.
And on the coming sabbath almost all the city was assembled to hear the word of God.
45 Wayahudi walipoona makutano, walijawa na wivu na kuongea maneno yaliyopinga vitu vilivyosemwa na Paulo na walimtukana.
But when the Jews saw the multitudes, they were filled of envy, and contradicted the things spoken by Paul, contradicting and slandering.
46 Lakini Paulo na Barnaba waliongea kwa ujasiri na kusema, “Ilikuwa ni muhimu kwamba neno la Mungu liongelewe kwanza kwenu. Kwa kuwa mnalisukumia mbali kutoka kwenu nakujiona kuwa hamkusitahili uzima wa milele, angalieni tutawageukia Mataifa. (aiōnios )
But having spoken boldly, Paul and Barnabas said, It was necessary for the word of God to be spoken first to you, but since ye thrust it away, and judge yourselves unworthy of eternal life, lo, we turn to the Gentiles. (aiōnios )
47 Kama ambavyo Bwana ametuamuru, akisema, 'Nimewaweka ninyi kama nuru kwa watu wa mataifa, kwamba mlete wokovu kwa pande zote za dunia.”
For so the Lord has commanded us: I have placed thee for a light of Gentiles, for thee to be for salvation as far as the extremity of the earth.
48 Mataifa waliposikia hili, walifurahi na kulisifu neno la Bwana. Wengi waliochaguliwa kwa uzima wa milele waliamini. (aiōnios )
And hearing this, the Gentiles were glad and glorified the word of the Lord. And as many as were appointed for eternal life believed. (aiōnios )
49 Neno la Bwana lilienea nchi yote.
And the word of the Lord was spread abroad through the whole region.
50 Lakini wayahudi waliwasihi waliojitoa na wanawake muhimu, pia na viongozi wa mji. Haya yalichochea mateso dhidi ya Paulo na Barnaba na waliwatupa nje ya mipaka ya mji.
But the Jews incited the religious women, and the prominent women, and the principle men of the city, and raised up a persecution against Paul and Barnabas. And they threw them out of their boundaries.
51 Lakini Paulo na Barnaba walikung'uta vumbi ya miguu yao. Kisha walienda kwenye mji wa Ikonia.
But after shaking off the dust of their feet against them, they came to Iconium.
52 Na wanafunzi walijawa na furaha pamoja na Roho mtakatifu.
And the disciples were filled with joy and the Holy Spirit.