< Amosi 9 >

1 Nilimwona Bwana akiwa amesimama kando ya madhabahu, naye akasema: “Piga vichwa vya nguzo ili vizingiti vitikisike. Viangushe juu ya vichwa vya watu wote; na wale watakaosalia nitawaua kwa upanga. Hakuna awaye yote atakayekimbia, hakuna atakayetoroka.
I sawe the Lord standing vpon the altar, and he sayde, Smite the lintel of the doore, that the postes may shake: and cut them in pieces, euen the heads of them all, and I will slay the last of them with the sword: he that fleeth of them, shall not flee away: and he that escapeth of them, shall not be deliuered.
2 Wajapojichimbia chini mpaka kwenye vina vya kuzimu, kutoka huko mkono wangu utawatoa. Wajapopanda juu hadi kwenye mbingu, kutoka huko nitawashusha. (Sheol h7585)
Though they digge into the hell, thence shall mine hande take them: though they clime vp to heauen, thence will I bring them downe. (Sheol h7585)
3 Wajapojificha juu ya kilele cha Karmeli, huko nitawawinda na kuwakamata. Wajapojificha kutoka kwenye uso wangu katika vilindi vya bahari, huko nako nitaamuru joka kuwauma.
And though they hide them selues in the toppe of Carmel, I will search and take them out thence: and though they be hid from my sight in the bottome of the sea, thence will I commande the serpent, and he shall bite them.
4 Wajapopelekwa uhamishoni na adui zao, huko nako nitaamuru upanga uwaue. Nitawakazia macho yangu kwa mabaya wala si kwa mazuri.”
And though they goe into captiuitie before their enemies, thence wil I commande the sword, and it shall slay them: and I will set mine eyes vpon them for euill, and not for good.
5 Bwana, Bwana Mwenye Nguvu Zote, yeye agusaye dunia nayo ikayeyuka, na wote wakaao ndani mwake wakaomboleza: nayo nchi yote huinuka kama Naili, kisha hushuka kama mto wa Misri;
And the Lord God of hosts shall touch the land, and it shall melt away, and al that dwel therein shall mourne, and it shall rise vp wholy like a flood, and shall bee drowned as by the flood of Egypt.
6 yeye ambaye hujenga jumba lake la kifalme katika mbingu na kuisimika misingi yake juu ya dunia, yeye aitaye maji ya bahari na kuyamwaga juu ya uso wa nchi: Bwana ndilo jina lake.
He buildeth his spheres in the heauen, and hath laide the foundation of his globe of elements in the earth: hee calleth the waters of the sea, and powreth them out vpon the open earth: the Lord is his Name.
7 “Je, Waisraeli, ninyi si sawa kwangu kama Wakushi?” asema Bwana. “Je, sikuleta Israeli kutoka Misri, Wafilisti kutoka Kaftori, na Washamu kutoka Kiri?
Are ye not as the Ethiopians vnto mee, O children of Israel, sayeth the Lord? haue not I brought vp Israel out of the land of Egypt? and the Philistims from Caphtor, and Aram from Kir?
8 “Hakika macho ya Bwana Mwenyezi yako juu ya ufalme wenye dhambi. Nami nitauangamiza kutoka kwenye uso wa dunia: hata hivyo sitaiangamiza kabisa nyumba ya Yakobo,” asema Bwana.
Beholde, the eyes of the Lord God are vpon the sinfull kingdome, and I will destroy it cleane out of the earth. Neuerthelesse I will not vtterly destroy the house of Iaakob, saith the Lord.
9 “Kwa kuwa nitatoa amri, na nitaipepeta nyumba ya Israeli miongoni mwa mataifa yote, kama vile nafaka ipepetwavyo katika ungo, na hakuna hata punje moja itakayoanguka chini.
For loe, I will command and I will sift the house of Israel among all nations, like as corne is sifted in a sieue: yet shall not the least stone fall vpon the earth.
10 Watenda dhambi wote miongoni mwa watu wangu watauawa kwa upanga, wale wote wasemao, ‘Maafa hayatatupata wala kutukuta.’
But all the sinners of my people shall dye by the sword, which say, The euill shall not come, nor hasten for vs.
11 “Katika siku ile nitaisimamisha hema ya Daudi iliyoanguka. Nitakarabati mahali palipobomoka na kujenga upya magofu yake, na kuijenga kama ilivyokuwa awali,
In that day will I raise vp the tabernacle of Dauid, that is fallen downe, and close vp the breaches therof, and I will rayse vp his ruines, and I will builde it, as in the dayes of olde,
12 ili wapate kuyamiliki mabaki ya Edomu, na mataifa yote yale yanayobeba Jina langu,” asema Bwana ambaye atafanya mambo haya.
That they may possesse the remnant of Edom, and of all the heathen, because my Name is called vpon them, sayeth the Lord, that doeth this.
13 “Siku zinakuja,” asema Bwana, “wakati mvunaji atatanguliwa na mkulima, naye mpanzi atatanguliwa na yeye akamuaye zabibu. Divai mpya itadondoka kutoka milimani, na kutiririka kutoka vilima vyote.
Behold, the dayes come, saith the Lord, that the plowman shall touche the mower, and the treader of grapes him that soweth seede: and the mountaines shall drop sweete wine, and all the hilles shall melt.
14 Nitawarejesha tena watu wangu Israeli waliohamishwa; wataijenga tena miji iliyoachwa magofu, nao wataishi ndani mwake. Watapanda mizabibu na kunywa divai yake; watalima bustani na kula matunda yake.
And I will bring againe the captiuitie of my people of Israel: and they shall build the waste cities, and inhabite the, and they shall plant vineyardes, and drinke the wine thereof: they shall also make gardens, and eate the fruites of them.
15 Nitaipanda Israeli katika nchi yao wenyewe, hawatangʼolewa tena kutoka nchi ambayo nimewapa,” asema Bwana Mungu wenu.
And I wil plant them vpon their land, and they shall no more bee pulled vp againe out of their lande, which I haue giuen them, sayeth the Lord thy God.

< Amosi 9 >