< Amosi 3 >

1 Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
Heare this worde that the Lord pronounceth against you, O children of Israel, euen against the whole familie which I brought vp from the land of Egypt, saying,
2 “Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
You onely haue I knowen of all the families of the earth: therefore I will visite you for all your iniquities.
3 Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
Can two walke together except they bee agreed?
4 Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
Will a lion roare in ye forest, when he hath no pray? or wil a lions whelpe cry out of his den, if he haue taken nothing?
5 Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
Can a birde fall in a snare vpon the earth, where no fouler is? or will he take vp the snare from the earth, and haue taken nothing at all?
6 Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
Or shall a trumpet be blowen in the citie, and the people be not afraide? or shall there be euil in a citie, and the Lord hath not done it?
7 Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
Surely the Lord God will doe nothing, but he reueileth his secrete vnto his seruantes the Prophets.
8 Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
The lyon hath roared: who will not bee afraide? the Lord God hath spoken: who can but prophecie?
9 Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
Proclayme in the palaces at Ashdod, and in the palaces in the lande of Egypt, and saye, Assemble your selues vpon the mountaines of Samaria: so beholde the great tumultes in the middes thereof, and the oppressed in the middes thereof.
10 Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
For they knowe not to doe right, sayth the Lord: they store vp violence, and robbery in their palaces.
11 Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
Therefore thus saith the Lord God, An aduersary shall come euen rounde about the countrey, and shall bring downe thy strength from thee, and thy palaces shalbe spoyled.
12 Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
Thus saieth the Lord, As the shephearde taketh out of the mouth of the lyon two legges, or a piece of an eare: so shall the children of Israel be taken out that dwell in Samaria in the corner of a bed, and in Damascus, as in a couche.
13 “Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
Heare, and testifie in the house of Iaakob, saith the Lord God, the God of hostes.
14 “Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
Surely in the day that I shall visit the transgressions of Israel vpon him, I wil also visite the altars of Beth-el, and the hornes of the altar shall be broken off, and fall to the ground.
15 Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.
And I wil smite the winter house with the sommer house, and the houses of yuorie shall perish, and the great houses shalbe consumed, sayth the Lord.

< Amosi 3 >