< Amosi 8 >

1 Hili ndilo alilonionyesha Bwana Mwenyezi katika maono: kikapu cha matunda yaliyoiva.
Thus hath the Lord God shewed vnto me, and behold, a basket of summer fruite.
2 Akaniuliza, “Amosi, unaona nini?” Nikajibu, “Kikapu chenye matunda yaliyoiva.” Ndipo Bwana akaniambia, “Wakati umewadia kwa watu wangu Israeli; sitawahurumia zaidi.”
And he said, Amos, what seest thou? And I sayd, A basket of sommer fruite. Then sayd the Lord vnto me, The ende is come vpon my people of Israel, I wil passe by them no more.
3 Bwana Mwenyezi asema, “Katika siku ile, nyimbo katika Hekalu zitageuka kuwa maombolezo. Miili mingi, mingi sana: itatupwa kila mahali! Kimya!”
And the songs of the Temple shalbe howlings in that day, saith the Lord God: many dead bodies shalbe in euery place: they shall cast them forth with silence.
4 Lisikieni hili, ninyi ambao mnawagandamiza wahitaji, na kuwaonea maskini wa nchi,
Heare this, O yee that swallowe vp the poore, that ye may make the needie of the lande to fayle,
5 mkisema, “Ni lini Mwezi Mwandamo utakapopita ili tupate kuuza nafaka, na Sabato itakwisha lini ili tuweze kuuza ngano?” Mkipunguza vipimo, na kuongeza bei, na kudanganya kwa mizani zisizo sawa,
Saying, When will the newe moneth bee gone, that we may sell corne? and the Sabbath, that we may set forth wheate, and make the Ephah small, and the shekel great, and falsifie the weights by deceit?
6 mkiwanunua maskini kwa fedha, na wahitaji kwa jozi ya viatu, na mkiuza hata takataka za ngano pamoja na ngano.
That we may buy the poore for siluer, and the needie for shooes: yea, and sell the refuse of the wheate.
7 Bwana ameapa kwake mwenyewe, aliye Kiburi cha Yakobo: “Kamwe sitasahau chochote ambacho wamefanya.
The Lord hath sworne by the excellencie of Iaakob, Surely I will neuer forget any of their workes.
8 “Je, nchi haitatetemeka kwa ajili ya hili, nao wote waishio ndani mwake hawataomboleza? Nchi yote itainuka kama Naili; itapanda na kushuka kama mto wa Misri.
Shall not the lande tremble for this, and euery one mourne, that dwelleth therein? and it shall rise vp wholy as a flood, and it shall bee cast out, and drowned as by the flood of Egypt.
9 “Katika siku ile,” asema Bwana Mwenyezi, “Nitalifanya jua litue alasiri na kuifanya dunia iwe giza wakati wa mchana mwangavu.
And in that day, saith the Lord God, I will euen cause the sunne to go downe at noone: and I will darken the earth in the cleare day.
10 Nitageuza sikukuu zenu za kidini kuwa maombolezo, na kuimba kwenu kote kuwe kilio. Nitawafanya ninyi nyote mvae nguo ya gunia na kunyoa nywele zenu. Nitaufanya wakati ule uwe kama wa kuombolezea mwana wa pekee, na mwisho wake kama siku ya uchungu.
And I will turne your feastes into mourning, and all your songs into lamentation: and I will bring sackcloth vpon all loynes, and baldnes vpon euery head: and I will make it as the mourning of an onely sonne, and the ende thereof as a bitter day.
11 “Siku zinakuja,” asema Bwana Mwenyezi, “wakati nitakapotuma njaa katika nchi yote: si njaa ya chakula wala kiu ya maji, lakini njaa ya kusikia maneno ya Bwana.
Beholde, the dayes come, sayeth the Lord God, that I will send a famine in the lande, not a famine of bread, nor a thirst for water, but of hearing the word of the Lord.
12 Wanaume watayumbayumba kutoka bahari hadi bahari na kutangatanga kutoka kaskazini mpaka mashariki, wakitafuta neno la Bwana, lakini hawatalipata.
And they shall wander from sea to sea, and from the North euen vnto the East shall they run to and from to seeke the worde of the Lord, and shall not finde it.
13 “Katika siku ile “wasichana wazuri na vijana wanaume wenye nguvu watazimia kwa sababu ya kiu.
In that day shall the faire virgines and the yong men perish for thirst.
14 Wale waapao kwa aibu ya Samaria, au kusema, ‘Hakika kama miungu yenu iishivyo, ee Dani,’ au ‘Hakika kama mungu wa Beer-Sheba aishivyo’: wataanguka, wala hawatasimama tena.”
They that sweare by the sinne of Samaria, and that say, Thy God, O Dan, liueth, and the maner of Beer-sheba liueth, euen they shall fall, and neuer rise vp againe.

< Amosi 8 >