< 2 Samweli 22 >

1 Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
David adressa à Yahvé les paroles de ce cantique, le jour où Yahvé le délivra de la main de tous ses ennemis et de la main de Saül,
2 Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
et il dit: « Yahvé est mon rocher, ma forteresse, et mon libérateur, même le mien;
3 Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
Dieu est mon rocher, en qui je trouve refuge; mon bouclier, et la corne de mon salut, ma haute tour et mon refuge. Mon sauveur, tu me sauves de la violence.
4 Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
J'invoque Yahvé, qui est digne d'être loué; Ainsi je serai sauvé de mes ennemis.
5 “Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
Car les vagues de la mort m'ont entouré. Les flots de l'impiété m'ont fait peur.
6 Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
Les cordes du séjour des morts m'entouraient. Les pièges de la mort m'ont attrapé. (Sheol h7585)
7 Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
Dans ma détresse, j'ai invoqué Yahvé. Oui, j'ai appelé mon Dieu. Il a entendu ma voix hors de sa tempe. Mon cri est parvenu à ses oreilles.
8 “Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
Alors la terre trembla et s'ébranla. Les fondations du ciel ont tremblé et ont été ébranlées, parce qu'il était en colère.
9 Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
De la fumée sortait de ses narines. Un feu dévorant est sorti de sa bouche. Des charbons ont été allumés par elle.
10 Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
Il a aussi incliné les cieux, et il est descendu. Une obscurité épaisse était sous ses pieds.
11 Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
Il était monté sur un chérubin, et il volait. Oui, il a été vu sur les ailes du vent.
12 Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
Il a fait des ténèbres un abri autour de lui, le rassemblement des eaux, et les nuages épais des cieux.
13 Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
A la clarté devant lui, des charbons ardents ont été allumés.
14 Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
Yahvé tonna du ciel. Le Très-Haut a fait entendre sa voix.
15 Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
Il envoya des flèches et les dispersa, des éclairs et les a rendus confus.
16 Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
Alors les canaux de la mer apparurent. Les fondations du monde ont été mises à nu par la réprimande de Yahvé, au souffle de ses narines.
17 “Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
Il a envoyé d'en haut et il m'a pris. Il m'a tiré de nombreuses eaux.
18 Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
Il m'a délivré de mon ennemi puissant, de ceux qui me haïssaient, car ils étaient trop puissants pour moi.
19 Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
Ils sont venus sur moi au jour de ma calamité, mais Yahvé était mon soutien.
20 Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
Il m'a aussi fait sortir dans un grand lieu. Il m'a délivré, car il s'est réjoui de moi.
21 “Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
L'Éternel m'a récompensé selon ma justice. Il m'a récompensé selon la propreté de mes mains.
22 Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
Car j'ai gardé les voies de l'Éternel, et je ne me suis pas éloigné de mon Dieu par méchanceté.
23 Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
Car toutes ses ordonnances étaient devant moi. Quant à ses statuts, je ne m'en suis pas écarté.
24 Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
J'étais aussi parfait envers lui. Je me suis gardé de mon iniquité.
25 Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
C'est pourquoi Yahvé m'a récompensé selon ma justice, Selon ma propreté dans sa vue.
26 “Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
Avec les miséricordieux, tu te montreras miséricordieux. Avec l'homme parfait, vous vous montrerez parfaite.
27 kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
Avec les purs, tu te montreras pur. Avec les tordus, vous vous montrerez astucieux.
28 Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
Tu sauveras le peuple affligé, mais tes yeux sont sur les arrogants, pour les faire tomber.
29 Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
Car tu es ma lampe, Yahvé. Yahvé va éclairer mes ténèbres.
30 Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
Car par toi, je cours contre une troupe. Par mon Dieu, je saute par-dessus un mur.
31 “Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
Quant à Dieu, sa voie est parfaite. La parole de Yahvé est mise à l'épreuve. Il est un bouclier pour tous ceux qui se réfugient en lui.
32 Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
Car qui est Dieu, en dehors de Yahvé? Qui est un rocher, à part notre Dieu?
33 Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
Dieu est ma forte forteresse. Il rend mon chemin parfait.
34 Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
Il rend ses pieds semblables à ceux des biches, et me place sur mes hauts lieux.
35 Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
Il apprend à mes mains à combattre, pour que mes bras fassent un arc de bronze.
36 Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
Tu m'as aussi donné le bouclier de ton salut. Votre gentillesse m'a rendu grand.
37 Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
Tu as élargi mes pas sous moi. Mes pieds n'ont pas glissé.
38 “Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
J'ai poursuivi mes ennemis et je les ai détruits. Je ne me suis pas retourné jusqu'à ce qu'ils soient consommés.
39 Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
Je les ai consumés, et les a transpercés, pour qu'ils ne puissent pas surgir. Oui, ils sont tombés sous mes pieds.
40 Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
Car tu m'as armé de force pour le combat. Tu as soumis à moi ceux qui s'élevaient contre moi.
41 Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
Tu as aussi fait en sorte que mes ennemis me tournent le dos, afin d'exterminer ceux qui me haïssent.
42 Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
Ils regardèrent, mais il n'y avait personne à sauver; même à Yahvé, mais il ne leur a pas répondu.
43 Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
Puis je les ai battus comme de la poussière de la terre. Je les ai écrasés comme la boue des rues, et je les ai répandus.
44 “Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
C'est toi aussi qui m'as délivré de l'oppression de mon peuple. Tu m'as gardé pour être le chef des nations. Un peuple que je n'ai pas connu me servira.
45 nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
Les étrangers se soumettront à moi. Dès qu'ils entendront parler de moi, ils m'obéiront.
46 Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
Les étrangers disparaîtront, et sortiront en tremblant de leurs lieux clos.
47 “Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
Yahvé est vivant! Béni soit mon rocher! Exalté soit Dieu, le rocher de mon salut,
48 Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
même le Dieu qui exécute la vengeance pour moi, qui fait tomber les peuples sous mes ordres,
49 aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
qui m'emmène loin de mes ennemis. Oui, tu me soulèves au-dessus de ceux qui s'élèvent contre moi. Tu me délivres de l'homme violent.
50 Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
C'est pourquoi je te louerai, Yahvé, parmi les nations, et chanteront les louanges de ton nom.
51 Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”
Il accorde une grande délivrance à son roi, et fait preuve de bonté envers ses oints, à David et à sa descendance, pour toujours. »

< 2 Samweli 22 >