< 2 Samweli 21 >

1 Wakati wa utawala wa Daudi kulikuwa na njaa kwa miaka mitatu mfululizo, kwa hiyo Daudi akautafuta uso wa Bwana. Bwana akasema, “Ni kwa sababu ya Sauli na nyumba yake iliyotiwa madoa ya damu, kwa sababu aliwaua Wagibeoni.”
Du temps de David, il y eut une famine pendant trois ans, année après année, et David chercha la face de Yahvé. Yahvé dit: « C'est à cause de Saül et de sa maison sanglante, parce qu'il a fait mourir les Gibéonites. »
2 Mfalme akawaita Wagibeoni na kuzumgumza nao. (Wagibeoni hawakuwa wa wana wa Israeli, ila walikuwa mabaki ya Waamori. Waisraeli walikuwa wameapa kuwaacha hai, lakini Sauli katika wivu wake kwa ajili ya Israeli na Yuda, alikuwa amejaribu kuwaangamiza.)
Le roi appela les Gabaonites et leur dit (les Gabaonites n'étaient pas d'entre les enfants d'Israël, mais d'entre les restes des Amoréens; les enfants d'Israël leur avaient fait un serment, et Saül cherchait à les tuer dans son zèle pour les enfants d'Israël et de Juda);
3 Daudi akawauliza Wagibeoni, “Niwatendee nini? Nitawaridhishaje ili mbariki urithi wa Bwana?”
et David dit aux Gabaonites: « Que dois-je faire pour vous? Et avec quoi dois-je faire l'expiation, afin que vous bénissiez l'héritage de Yahvé? ».
4 Wagibeoni wakamjibu, “Hatuna haki ya kudai fedha wala dhahabu kutoka kwa Sauli au jamaa yake, wala hatuna haki ya kumuua mtu yeyote katika Israeli.” Daudi akawauliza, “Mnataka niwafanyie nini?”
Les Gabaonites lui dirent: « Il n'est question ni d'argent ni d'or entre nous et Saül ou sa maison, et il ne nous appartient pas de faire mourir quelqu'un en Israël. » Il a dit: « Je ferai pour toi tout ce que tu dis. »
5 Wakamjibu mfalme, “Kwa habari ya mtu aliyetuangamiza na kufanya hila mbaya dhidi yetu ili kwamba tuangamizwe na tusiwe na yeyote katika Israeli,
Ils dirent au roi: « L'homme qui nous a consumés et qui a comploté contre nous pour que nous soyons détruits et que nous ne puissions rester dans aucune des frontières d'Israël,
6 tupatieni wazao wake saba wa kiume tuwaue hadharani mbele za Bwana huko Gibea ya Sauli, aliyekuwa amechaguliwa na Bwana.” Basi mfalme akasema, “Nitawakabidhi kwenu.”
qu'on nous livre sept hommes de ses fils, et nous les pendrons à Yahvé à Guibea de Saül, l'élu de Yahvé. » Le roi a dit: « Je vais les donner. »
7 Mfalme akamhifadhi Mefiboshethi mwana wa Yonathani, mwana wa Sauli, kwa sababu ya kile kiapo mbele za Bwana kati ya Daudi na Yonathani.
Mais le roi épargna Mephiboscheth, fils de Jonathan, fils de Saül, à cause du serment de l'Éternel qui était entre eux, entre David et Jonathan, fils de Saül.
8 Lakini mfalme akamchukua Armoni na Mefiboshethi, wana wawili wa Rispa binti Aiya, ambao alikuwa amemzalia Sauli, pamoja na wana watano wa Merabu binti Sauli, aliokuwa amemzalia Adrieli mwana wa Barzilai, Mmeholathi.
Mais le roi prit les deux fils de Ritspa, fille d'Aja, qu'elle avait enfantés à Saül, Armoni et Mephibosheth, et les cinq fils de Merab, fille de Saül, qu'elle avait enfantés à Adriel, fils de Barzillai, le Méholathien.
9 Akawakabidhi kwa Wagibeoni, ambao waliwaua na kuwaweka wazi juu ya kilima mbele za Bwana. Wote saba walianguka kwa pamoja; waliuawa katika siku za kwanza za mavuno, mara tu uvunaji wa shayiri ulipokuwa unaanza.
Il les livra entre les mains des Gabaonites, qui les pendirent sur la montagne devant Yahvé, et tous les sept tombèrent ensemble. Ils furent mis à mort les jours de la moisson, les premiers jours, au début de la récolte de l'orge.
10 Rispa binti Aiya akachukua nguo ya gunia, akajitandikia juu ya mwamba. Kuanzia mwanzo wa mavuno mpaka mvua ziliponyesha juu ya miili ya hao waliouawa, Rispa hakuruhusu ndege wa angani kuwagusa wakati wa mchana, wala wanyama wa mwitu wakati wa usiku.
Ritspa, fille d'Aja, prit un sac et s'en étendit sur le rocher, depuis le début de la moisson jusqu'à ce que l'eau tombe du ciel sur eux. Elle ne permit ni aux oiseaux du ciel de s'y reposer le jour, ni aux animaux des champs la nuit.
11 Daudi alipoambiwa kile Rispa binti Aiya, suria wa Sauli, alichokuwa amekifanya,
On raconta à David ce qu'avait fait Ritspa, fille d'Aja, concubine de Saül.
12 alikwenda akachukua mifupa ya Sauli na mwanawe Yonathani kutoka kwa watu wa Yabeshi-Gileadi. (Walikuwa wameichukua kwa siri kutoka uwanja wa watu wote huko Beth-Shani, mahali ambapo Wafilisti walikuwa wamewatundika baada ya kumuua Sauli huko Gilboa.)
David alla prendre les ossements de Saül et les ossements de Jonathan, son fils, chez les hommes de Jabesh Galaad, qui les avaient volés dans la rue de Beth Shan, où les Philistins les avaient pendus le jour où les Philistins tuèrent Saül à Gilboa;
13 Daudi akaileta mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani kutoka huko, pia mifupa ya wale waliokuwa wameuawa na kutupwa ilikusanywa.
et il fit monter de là les ossements de Saül et les ossements de Jonathan, son fils. Ils recueillirent aussi les ossements de ceux qui avaient été pendus.
14 Wakazika mifupa ya Sauli na ya mwanawe Yonathani katika kaburi la Kishi, babaye Sauli, huko Sela katika nchi ya Benyamini, nao wakafanya kila kitu mfalme alichoagiza. Baada ya hayo, Mungu akajibu maombi kwa ajili ya nchi.
On enterra les ossements de Saül et de Jonathan, son fils, dans le pays de Benjamin, à Zéla, dans le tombeau de Kis, son père, et on exécuta tout ce que le roi avait ordonné. Après cela, Dieu a répondu à la prière pour le pays.
15 Kwa mara nyingine tena kulikuwa na vita kati ya Wafilisti na Israeli. Daudi akashuka pamoja na watu wake ili kupigana dhidi ya Wafilisti, naye akawa amechoka sana.
Les Philistins firent de nouveau la guerre à Israël; David descendit, et ses serviteurs avec lui, et combattit les Philistins. David s'affaiblit;
16 Naye Ishbi-Benobu, mmoja wa wazao wa Warefai, ambaye mkuki wake ulikuwa na uzito wa shekeli 300 za shaba, alikuwa amejifunga upanga mpya, naye alisema angemuua Daudi.
et Ishbibenob, qui était d'entre les fils du géant, et dont la lance pesait trois cents sicles d'airain, armé d'une épée neuve, pensait tuer David.
17 Lakini Abishai mwana wa Seruya akaja kumwokoa Daudi; akampiga huyo Mfilisti, akamwangusha chini na kumuua. Ndipo watu wakamwapia Daudi, wakisema, “Kamwe hutakwenda tena nasi vitani, ili kwamba taa ya Israeli isije ikazimwa.”
Mais Abishaï, fils de Tseruja, lui vint en aide, frappa le Philistin et le tua. Les hommes de David lui jurèrent alors: « Ne sors plus avec nous pour combattre, afin que tu n'éteignes pas la lampe d'Israël. »
18 Baada ya muda, kukawa na vita nyingine na Wafilisti, huko Gobu. Wakati huo Sibekai, Mhushathi, akamuua Safu, mmoja wa wazao wa Warefai.
Après cela, il y eut de nouveau une guerre avec les Philistins à Gob. Et Sibbecaï, le Hushathite, tua Saph, qui était d'entre les fils du géant.
19 Katika vita vingine na Wafilisti huko Gobu, Elhanani mwana wa Yaare-Oregimu, Mbethlehemu, alimuua nduguye Goliathi, Mgiti, ambaye mkuki wake ulikuwa na mpini kama mti wa mfumaji.
Il y eut encore une guerre avec les Philistins à Gob, et Elhanan, fils de Jaaré-Oregim, le Bethléhémite, tua le frère de Goliath, le Gittien, dont le bâton de la lance était comme une poutre de tisserand.
20 Katika vita vingine tena, vilivyopiganwa huko Gathi, kulikuwako na mtu mmoja mkubwa mwenye vidole sita katika kila mkono na vidole sita kila mguu, jumla vidole ishirini na vinne. Yeye alikuwa pia mzao wa Mrefai.
Il y eut encore une guerre à Gath, où se trouvait un homme de grande taille, qui avait six doigts à chaque main et six orteils à chaque pied, au nombre de vingt-quatre.
21 Alipowadhihaki Israeli, Yonathani mwana wa Shimea, nduguye Daudi, akamuua.
Lorsqu'il défia Israël, Jonathan, fils de Schimeï, frère de David, le tua.
22 Hawa wanne walikuwa wazao wa Warefai huko Gathi, nao walianguka kwa mikono ya Daudi na watu wake.
Ces quatre-là étaient nés du géant à Gath, et ils tombèrent par la main de David et par la main de ses serviteurs.

< 2 Samweli 21 >