< 2 Samweli 23 >

1 Haya ni maneno ya mwisho ya Daudi: “Neno la Daudi mwana wa Yese, neno la mtu aliyeinuliwa na Aliye Juu Sana, mtu aliyepakwa mafuta na Mungu wa Yakobo, mwimbaji wa nyimbo wa Israeli:
Voici les dernières paroles de David. David, fils de Jessé, dit, l'homme qui a été élevé en haut dit, l'oint du Dieu de Jacob, le doux psalmiste d'Israël:
2 “Roho wa Bwana alinena kupitia kwangu, neno lake lilikuwa ulimini mwangu.
« L'Esprit de Yahvé a parlé par moi. Sa parole était sur ma langue.
3 Mungu wa Israeli alinena, mwamba wa Israeli akaniambia: ‘Mtu anatawala watu kwa haki, wakati anapotawala akiwa na hofu ya Mungu,
Le Dieu d'Israël a dit, le Rocher d'Israël m'a parlé, Celui qui dirige les hommes avec droiture, qui règne dans la crainte de Dieu,
4 yeye ni kama mwanga wa asubuhi jua lichomozapo asubuhi isiyo na mawingu, kama mwanga baada ya mvua uchipuzao majani kutoka ardhini.’
sera comme la lumière du matin quand le soleil se lève, un matin sans nuages, quand l'herbe tendre jaillit de la terre, par une lumière claire après la pluie ».
5 “Je, si hivyo ilivyo nyumba yangu mbele za Mungu? Je, hajafanya Agano la milele nami, lililopangwa na kuimarishwa kila sehemu? Je, hatanifanya niufurahie wokovu wangu na kunijalia matakwa yangu yote?
Ma maison n'est-elle pas ainsi avec Dieu? Mais il a conclu avec moi une alliance éternelle, ordonné en toutes choses, et sûr, car c'est tout mon salut et tout mon désir. Ne va-t-il pas la faire grandir?
6 Lakini watu waovu wote watatupwa kando kama miiba, ambayo haikusanywi kwa mkono.
Mais tous les impies seront comme des épines qu'on arrache, parce qu'ils ne peuvent pas être pris avec la main.
7 Yeyote agusaye miiba hutumia chombo cha chuma au mpini wa mkuki, nayo huchomwa pale ilipo.”
L'homme qui les touche doit être armé de fer et de la hampe d'une lance. Ils seront entièrement brûlés par le feu à leur place. »
8 Haya ndiyo majina ya mashujaa wa Daudi: Yosheb-Bashebethi, Mtahkemoni, alikuwa kiongozi wa wale Watatu; yeye aliinua mkuki wake dhidi ya watu 800, ambao aliwaua katika pambano moja.
Voici les noms des vaillants hommes que David avait: Josheb Basshebeth, de Tahchemon, chef des capitaines; on l'appelait Adino, l'Eznite, qui tua huit cents personnes à la fois.
9 Wa pili wake alikuwa Eleazari mwana wa Dodai, Mwahohi. Akiwa mmojawapo wa wale mashujaa watatu, alikuwa pamoja na Daudi wakati waliwadhihaki Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko Pas-Damimu kwa ajili ya vita. Kisha watu wa Israeli wakarudi nyuma,
Après lui, Éléazar, fils de Dodaï, fils d'un Ahohite, l'un des trois vaillants hommes qui étaient avec David lorsqu'ils défièrent les Philistins qui étaient là rassemblés pour combattre, et que les hommes d'Israël s'étaient retirés.
10 lakini yeye alisimama imara akawaua Wafilisti hadi mkono wake ukachoka na ukagandamana na upanga. Bwana akawapa ushindi mkubwa siku ile. Vikosi vikarudi kwa Eleazari, kuteka tu nyara za waliokufa.
Il se leva et frappa les Philistins jusqu'à ce que sa main se soit fatiguée, et que sa main se soit gelée à l'épée; et Yahvé fit en ce jour une grande victoire; et le peuple ne revint après lui que pour faire du pillage.
11 Aliyefuata alikuwa Shama mwana wa Agee, Mharari. Wafilisti walipokusanyika pamoja mahali palipokuwa shamba lililojaa dengu, vikosi vya Israeli viliwakimbia.
Après lui, Shammah, fils d'Agee, un Hararien. Les Philistins s'étaient rassemblés en troupe là où il y avait un terrain plein de lentilles; et le peuple fuyait devant les Philistins.
12 Lakini Shama akasimama imara katikati ya lile shamba. Akalitetea na kuwaua Wafilisti, naye Bwana akawapa ushindi mkubwa.
Mais lui se plaça au milieu du terrain, le défendit et tua les Philistins; et Yahvé remporta une grande victoire.
13 Wakati wa mavuno, viongozi watatu kati ya viongozi thelathini walishuka, wakamwendea Daudi katika pango la Adulamu, wakati kikundi cha Wafilisti kilikuwa kimepiga kambi katika Bonde la Warefai.
Trois des trente chefs descendirent et vinrent auprès de David, au temps de la moisson, dans la caverne d'Adullam; et la troupe des Philistins campait dans la vallée des Rephaïm.
14 Wakati huo Daudi alikuwa katika ngome, na kambi ya Wafilisti ilikuwa huko Bethlehemu.
David était alors dans la forteresse, et la garnison des Philistins était alors à Bethléhem.
15 Daudi akatamani maji, akasema, “Laiti mtu angenipatia maji ya kunywa kutoka kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu!”
David dit avec nostalgie: « Oh, si quelqu'un me donnait à boire de l'eau du puits de Bethléem, qui est près de la porte! »
16 Basi mashujaa hao watatu wakapenya katikati ya Wafilisti, wakaenda kuchota maji kutoka kwa kisima kilicho karibu na lango la Bethlehemu, wakamletea Daudi. Lakini Daudi akakataa kuyanywa. Badala yake, aliyamimina mbele za Bwana.
Les trois hommes forts percèrent l'armée des Philistins, puis ils puisèrent de l'eau dans le puits de Bethléem qui est près de la porte, ils la prirent et l'apportèrent à David; mais il ne voulut pas en boire, et il la versa à l'Éternel.
17 Akasema, “Iwe mbali nami, Ee Bwana, kufanya kitu hiki. Je, hii si damu ya watu ambao walikwenda kwa kuhatarisha maisha yao?” Naye Daudi hakuyanywa. Haya yalifanywa na hao mashujaa watatu.
Il dit: « Éloigne-toi de moi, Yahvé, pour que je fasse cela! N'est-ce pas le sang des hommes qui ont risqué leur vie pour y aller? ». C'est pourquoi il ne voulut pas le boire. Les trois hommes forts firent ces choses.
18 Abishai ndugu yake Yoabu mwana wa Seruya ndiye alikuwa kiongozi wa hao Watatu. Aliinua mkuki wake dhidi ya watu 300 ambao aliwaua, kwa hiyo naye akawa na sifa kama hao Watatu.
Abischaï, frère de Joab, fils de Tseruja, était le chef des trois. Il leva sa lance contre trois cents personnes et les tua, et il eut un nom parmi les trois.
19 Je, hakupata heshima kubwa zaidi kuliko hao Watatu? Alikuwa jemadari wao, ingawa hakuhesabiwa miongoni mwao.
N'était-il pas le plus honorable des trois? C'est pourquoi il fut fait leur chef. Cependant, il n'était pas inclus parmi les trois.
20 Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa mpiganaji hodari kutoka Kabseeli ambaye alifanya mambo makubwa ya ujasiri. Aliwaua mashujaa wawili waliokuwa hodari kuliko wote wa Moabu. Pia alishuka shimoni kulipokuwa na theluji na kumuua simba.
Benaja, fils de Jehoiada, fils d'un homme vaillant de Kabzeel, qui avait fait des exploits, tua les deux fils d'Ariel de Moab. Il descendit aussi et tua un lion au milieu d'une fosse, au temps de la neige.
21 Pia alimuua Mmisri mrefu mkubwa. Ingawa Mmisri alikuwa na mkuki mkononi mwake, Benaya alimwendea akiwa na rungu. Alipokonya mkuki kutoka mkononi mwa Mmisri na kumuua kwa mkuki wake mwenyewe.
Il tua un Égyptien énorme, et l'Égyptien avait une lance à la main; mais il descendit vers lui avec un bâton, arracha la lance de la main de l'Égyptien, et le tua avec sa propre lance.
22 Haya yalikuwa mambo ya ushujaa ya Benaya mwana wa Yehoyada; naye pia alikuwa maarufu kama wale mashujaa watatu.
Benaja, fils de Jehojada, fit ces choses, et il eut un nom parmi les trois vaillants hommes.
23 Yeye aliheshimiwa zaidi ya wale Thelathini, lakini hakujumuishwa miongoni mwa wale Watatu. Daudi akamweka kuwa kiongozi wa walinzi wake.
Il était plus honorable que les trente, mais il n'atteignit pas les trois. David le plaça à la tête de sa garde.
24 Miongoni mwa wale Thelathini walikuwepo: Asaheli ndugu wa Yoabu; Elhanani mwana wa Dodo kutoka Bethlehemu;
Asaël, frère de Joab, était l'un des trente: Elhanan, fils de Dodo, de Bethléhem,
25 Shama, Mharodi; Elika, Mharodi;
Shammah, le Harodite, Elika, le Harodite,
26 Helesi, Mpalti; Ira mwana wa Ikeshi kutoka Tekoa;
Hélez, le Paltite, Ira, fils d'Ikkesh, le Tekoïte,
27 Abiezeri kutoka Anathothi; Mebunai, Mhushathi;
Abiezer, l'Anathothite, Mebunnai, le Hushathite,
28 Salmoni, Mwahohi; Maharai, Mnetofathi;
Zalmon, l`Achochite, Maharaï, le Netophathien,
29 Heledi mwana wa Baana, Mnetofathi; Itai mwana wa Ribai kutoka Gibea ya Benyamini;
Héleb, fils de Baana, le Netophathien, Ittaï, fils de Ribaï, de Guibea, des fils de Benjamin,
30 Benaya Mpirathoni; Hidai kutoka mabonde ya Gaashi;
Benaja, de Pirathon, Hiddaï, des ruisseaux de Gaasch.
31 Abi-Alboni, Mwaribathi; Azmawethi, Mbarhumi;
Abialbon, l'Arbathite, Azmaveth, le Barhumite,
32 Eliaba, Mshaalboni; wana wa Yasheni; Yonathani
Eliahba, le Shaalbonite, les fils de Jashen, Jonathan,
33 mwana wa Shama, Mharari; Ahiamu mwana wa Sharari, Mharari;
Shammah, le Hararite, Ahiam, fils de Sharar, l'Ararite,
34 Elifeleti mwana wa Ahasbai, Mmaakathi; Eliamu mwana wa Ahithofeli, Mgiloni;
Eliphelet, fils d'Ahasbai, le fils du Maacathite, Eliam, fils d'Ahithophel, le Gilonite,
35 Hezro, Mkarmeli; Paarai, Mwarbi;
Hezro, le Carmélite, Paaraï, l'Arbite,
36 Igali mwana wa Nathani kutoka Soba; Bani, Mgadi;
Igal, fils de Nathan, de Tsoba, Bani, le Gadite,
37 Seleki, Mwamoni; Naharai, Mbeerothi, aliyekuwa mbeba silaha za Yoabu mwana wa Seruya;
Zelek, l'Ammonite, Naharai, le Beérothite, porteurs d'armes de Joab, fils de Tseruja,
38 Ira, Mwithiri; Garebu, Mwithiri;
Ira, l'Ithrite, Gareb, l'Ithrite,
39 na Uria, Mhiti. Jumla yao wote walikuwa watu thelathini na saba.
et Urie, le Hittite: trente-sept en tout.

< 2 Samweli 23 >