< Markus 5 >

1 Nad jõudsid järve teisele kaldale gerasalaste maa-alale.
Wakafika upande wa pili wa ziwa wakaingia katika nchi ya Wagerasi.
2 Kui Jeesus astus paadist välja, tuli surnuaialt temale vastu mees, kellel oli kuri vaim.
Yesu alipotoka kwenye mashua, mara mtu mmoja mwenye pepo mchafu akatoka makaburini akakutana naye.
3 See mees elas haudade vahel ning teda ei olnud enam võimalik kinni siduda, isegi mitte ahelatega.
Mtu huyu aliishi makaburini, wala hakuna aliyeweza kumzuia hata kwa kumfunga minyororo.
4 Teda oli sageli pandud ahelaisse ja raudadesse, kuid ta rebis ahelad lihtsalt katki ning purustas käe- ja jalarauad tükkideks. Kellelgi ei olnud jõudu, et temast jagu saada.
Kwa kuwa mara kwa mara alikuwa amefungwa minyororo mikononi na miguuni, lakini akaikata hiyo minyororo na kuzivunja zile pingu miguuni mwake. Hapakuwa na mtu yeyote aliyekuwa na nguvu za kumzuia.
5 Päeval ja ööl kisendas ta haudade vahel ja lähedal asuvates mägedes ning lõikus ennast teravate kividega.
Usiku na mchana alikuwa makaburini na milimani, akipiga kelele na kujikatakata kwa mawe.
6 Nähes Jeesust kaugelt, jooksis ta vastu ja langes tema ees põlvili.
Alipomwona Yesu kwa mbali, alimkimbilia, akapiga magoti mbele yake.
7 Ta hüüdis valju häälega: „Mis on sul minuga tegemist, Jeesus, kõigevägevama Jumala Poeg? Vannu Jumala nimel, et sa ei piina mind!“
Akapiga kelele kwa nguvu akisema, “Una nini nami, Yesu, Mwana wa Mungu Aliye Juu Sana? Ninakusihi kwa jina la Mungu, usinitese!”
8 Sest Jeesus oli juba käskinud kurjal vaimul mehest lahkuda.
Kwa kuwa Yesu alikuwa amemwambia, “Mtoke mtu huyu, wewe pepo mchafu!”
9 Siis küsis Jeesus temalt: „Mis su nimi on?“„Mu nimi on Leegion, sest meid on palju!“vastas ta.
Yesu akamuuliza, “Jina lako ni nani?” Akamjibu, “Jina langu ni Legioni, kwa kuwa tuko wengi.”
10 Ta anus Jeesust pidevalt, et Jeesus ei saadaks teda kaugele.
Akamsihi Yesu sana asiwapeleke nje ya nchi ile.
11 Läheduses mäenõlval oli söömas suur seakari.
Palikuwa na kundi kubwa la nguruwe lililokuwa likilisha karibu kando ya kilima.
12 Kurjad vaimud palusid Jeesust: „Saada meid sigadesse, et saaksime nende sisse minna.“
Wale pepo wachafu wakamsihi Yesu wakisema, “Tuamuru twende kwenye wale nguruwe. Turuhusu tuwaingie.”
13 Jeesus lubas neil seda teha. Kurjad vaimud lahkusid mehest ja läksid sigade sisse. Kogu kari − umbes kaks tuhat siga − tormas järsust kaljust alla merre ja uppus.
Basi Yesu akawaruhusu, nao wale pepo wachafu wakatoka, wakawaingia hao nguruwe. Lile kundi lilikuwa na nguruwe wapatao 2,000, nao wote wakateremkia gengeni kwa kasi, nao wakatumbukia ziwani na kuzama.
14 Seakarjused jooksid minema ning levitasid seda uudis kõikjal linnas ja maal. Rahvas tuli välja vaatama, et näha, mis oli juhtunud.
Wale watu waliokuwa wakichunga hao nguruwe wakakimbilia mjini na vijijini kueleza yaliyotukia. Watu wakatoka kwenda kuona hayo yaliyokuwa yametukia.
15 Kui nad leidsid Jeesuse, nägid nad meest, kes oli olnud kurjade vaimude võimuses, sealsamas istumas, riietatult ja täie mõistuse juures − sedasama meest, kellel oli olnud leegion kurje vaime −, ja nad kohkusid!
Walipofika kwa Yesu, wakamwona yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu legioni akiwa ameketi hapo, amevaa nguo na mwenye akili timamu. Wakaogopa.
16 Siis need, kes olid näinud, mis juhtus mehega, kes oli olnud kurjade vaimude meelevallas, ja sigadega, jutustasid teistele.
Wale walioyaona mambo hayo wakawaeleza watu wengine yaliyomtokea yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu, na habari za lile kundi la nguruwe pia.
17 Nad hakkasid paluma, et Jeesus nende piirkonnast lahkuks.
Basi watu wakaanza kumwomba Yesu aondoke katika nchi yao.
18 Kui Jeesus astus paati, siis mees, kes oli olnud kurjade vaimude võimuses, anus, et võiks temaga kaasa minna.
Yesu alipokuwa anaingia kwenye mashua, yule mtu aliyekuwa amepagawa na pepo wachafu akamsihi Yesu waende pamoja.
19 Aga Jeesus keeldus ja ütles talle: „Mine koju omade juurde ja räägi neile, kui palju Issand on sinu heaks teinud ja kuidas ta sinu peale halastas.“
Yesu hakumruhusu, bali alimwambia, “Nenda nyumbani kwa jamaa yako ukawaeleze mambo makuu aliyokutendea Bwana, na jinsi alivyokuhurumia.”
20 Nii läks see mees oma teed ja hakkas Kümnelinnamaal kuulutama kõigest, mida Jeesus oli tema heaks teinud, ja kõik olid hämmastuses.
Yule mtu akaenda zake, akaanza kutangaza katika Dekapoli mambo makuu Yesu aliyomtendea. Nao watu wote wakastaajabu.
21 Jeesus läks paadiga jälle tagasi järve teisele kaldale, kus kogunes tema ümber suur rahvahulk.
Yesu alipokwisha kuvuka tena na kufika ngʼambo, umati mkubwa wa watu ukamzunguka yeye akiwa hapo kando ya bahari.
22 Tema juurde tuli sünagoogi ülem − mees nimega Jairus. Kui ta Jeesust nägi, langes ta tema jalge ette maha
Kisha mmoja wa viongozi wa sinagogi aliyeitwa Yairo akafika pale. Naye alipomwona Yesu, akapiga magoti miguuni pake,
23 ja palus, öeldes: „Minu tütreke on suremas. Palun tule ja pane oma käed tema peale, et ta võiks terveks saada ja elada.“
akamsihi akisema, “Binti yangu mdogo ni mgonjwa mahututi. Tafadhali nakusihi, njoo uweke mikono yako juu yake ili apate kupona, naye atakuwa hai.”
24 Niisiis läks Jeesus temaga kaasa. Kogu rahvas järgnes, rüseledes ja tõugeldes.
Hivyo Yesu akaenda pamoja naye. Umati mkubwa wa watu ukamfuata, nao watu wakawa wanamsonga.
25 Seal oli üks naine, kes oli kaksteist aastat veritsustõve all kannatanud.
Hapo palikuwa na mwanamke aliyekuwa amesumbuliwa na tatizo la kutokwa damu kwa miaka kumi na miwili.
26 Ta oli paljude arstide käe läbi märkimisväärselt kannatanud ning kulutanud ära kõik, mis tal oli. Kuid miski ei olnud teda aidanud, õigupoolest oli olukord ainult kehvemaks läinud.
Mwanamke huyu alikuwa ameteseka sana kwa mikono ya matabibu wengi, na kutumia kila kitu alichokuwa nacho. Lakini badala ya kupona, hali yake ilizidi kuwa mbaya.
27 Ta oli kuulnud Jeesusest, seega tuli ta rahvahulgas tema selja taha ja puudutas tema ülekuube.
Alikuwa amesikia habari za Yesu, naye akaja kwa nyuma yake kwenye umati wa watu, akaligusa vazi lake,
28 Ta ütles endale: „Kui ma ainult saan tema kuube puudutada, siis saan ma terveks.“
kwa maana alisema moyoni mwake, “Kama nikiweza kuligusa vazi lake tu, nitaponywa.”
29 Veritsemine lõppes viivitamatult ja ta tundis, et tema keha on haigusest terveks saanud.
Mara kutoka damu kwake kukakoma, naye akajisikia mwilini mwake amepona kabisa.
30 Jeesus, kes tajus kohe, et temast läks vägi välja, pöördus rahvahulgas ümber ja küsis: „Kes puudutas mu kuube?“
Ghafula Yesu akatambua kuwa nguvu zimemtoka. Akaugeukia ule umati wa watu na kuuliza, “Ni nani aliyegusa mavazi yangu?”
31 Jüngrid vastasid: „Vaata, kuidas rahvas sulle peale tungib. Mis mõttes sa küsid: kes mind puudutas?“
Wanafunzi wake wakamjibu, “Unaona jinsi umati wa watu unavyokusonga. Wawezaje kuuliza, ‘Ni nani aliyenigusa?’”
32 Kuid Jeesus vaatas ikkagi ringi, et näha, kes seda tegi.
Lakini Yesu akaangalia pande zote ili aone ni nani aliyemgusa.
33 Naine, kes mõistis, mis temaga oli juhtunud, tuli ja langes tema ette maha ning rääkis talle kogu loo.
Yule mwanamke, akijua kilichomtokea, akaja, akaanguka miguuni pake akitetemeka kwa hofu, akamweleza ukweli wote.
34 „Mu tütar, sinu kindel usk minusse tegi sind terveks. Mine rahus. Sa oled oma haigusest täielikult tervenenud, “ütles Jeesus talle.
Yesu akamwambia, “Binti, imani yako imekuponya. Nenda kwa amani, upone kabisa ugonjwa wako.”
35 Sel ajal kui ta veel rääkis, tulid mõned inimesed sünagoogi ülema kodust. „Su tütar on surnud, “ütlesid nad. „Pole enam vaja Õpetajat tüüdata.“
Alipokuwa bado anaongea, watu wakafika kutoka nyumbani kwa Yairo. Wakamwambia, “Binti yako amekufa. Kwa nini kuendelea kumsumbua Mwalimu?”
36 Aga Jeesus ei pööranud nende sõnadele tähelepanu. Ta ütles sünagoogi ülemale: „Ära karda, usu lihtsalt minusse.“
Aliposikia hayo waliyosema, Yesu akamwambia huyo kiongozi wa sinagogi, “Usiogope. Amini tu.”
37 Ta ei võtnud endaga kaasa kedagi, välja arvatud Peetruse, Jaakobuse ja Jaakobuse venna Johannese.
Hakumruhusu mtu mwingine yeyote amfuate isipokuwa Petro, Yakobo na Yohana, nduguye Yakobo.
38 Kui nad jõudsid sünagoogi ülema maja juurde, nägi Jeesus segadust ja rahutust, inimesed nutsid ja halisesid.
Walipofika nyumbani kwa yule kiongozi wa sinagogi, Yesu akaona ghasia, watu wakilia na kuomboleza kwa sauti kubwa.
39 Ta läks sisse ja küsis neilt: „Miks te nutate ja halisete? Tüdrukuke ei ole surnud, vaid lihtsalt magab.“
Alipokwisha kuingia ndani, akawaambia, “Kwa nini mnafanya ghasia na kulia? Mtoto hajafa, bali amelala tu.”
40 Nad naersid tema üle põlastavalt. Jeesus käskis kõigil lahkuda. Seejärel läks ta koos lapse isa ja ema ning kolme jüngriga tuppa, kus tüdrukuke lamas.
Wale watu wakamcheka kwa dharau. Lakini yeye akawatoa wote nje, akawachukua baba na mama wa yule mtoto, pamoja na wale wanafunzi aliokuwa nao. Wakaingia ndani mpaka pale alipokuwa yule mtoto.
41 Tüdruku kätt võttes ütles ta: „Talita kuum“, mis tähendab: „Tüdruk, tõuse üles!“
Akamshika mtoto mkono, akamwambia, “Talitha koum!” (maana yake ni, “Msichana, nakuambia: amka!”)
42 Tüdruk, kes oli kaheteistkümneaastane, tõusis kohe üles ja hakkas kõndima. Nad olid juhtunust täielikus jahmatuses.
Mara yule msichana akasimama, akaanza kutembea (alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili). Walipoona haya, wakastaajabu sana.
43 Jeesus keelas neid karmilt, et nad ei räägiks sellest kellelegi, ning käskis tüdrukukesele midagi süüa anda.
Yesu akawaagiza kwa ukali wasimweleze mtu yeyote jambo hilo, naye akawaambia wampe yule msichana chakula.

< Markus 5 >