< Luuka 1 >
1 Nagu sa tead, on paljud teised üritanud kirja panna seda, mis on täide läinud ja puudutab ka meid.
Kwa kuwa watu wengi wamekaa ili kuandika habari za mambo yaliyotukia katikati yetu,
2 Nende jutustused põhinesid esimeste pealtnägijate ja Sõna kuulutajate tõenditel
kama vile yalivyokabidhiwa kwetu na wale waliokuwa mashahidi walioyaona na watumishi wa Bwana,
3 ja ka mina otsustasin, et kuna olen kõike seda algusest peale väga hoolikalt jälginud, oleks hea mõte kõigest toimunust kirja panna täpne jutustus.
mimi nami baada ya kuchunguza kila kitu kwa uangalifu kuanzia mwanzo, niliamua kukuandikia habari za mambo hayo, ewe mtukufu Theofilo,
4 Tegin seda, kallis Teofilos, et sa võiksid olla kindel, et see, mida sulle õpetati, on täiesti usaldusväärne.
ili upate kujua ukweli kuhusu yale uliyofundishwa.
5 Sel ajal kui Heroodes oli Juudamaa kuningas, oli üks preester nimega Sakarias, kes oli pärit Abija preesterlikust rühmast. Ta oli abielus Eliisabetiga, kes põlvnes samuti preester Aaronist.
Wakati wa Herode mfalme wa Uyahudi, palikuwa na kuhani mmoja jina lake Zekaria, ambaye alikuwa wa ukoo wa kikuhani wa Abiya. Elizabeti mkewe alikuwa pia mzao wa Aroni.
6 Nad mõlemad tegid, mis oli Jumala ees õige, ning järgisid hoolikalt kõiki Issanda käske ja määrusi.
Zekaria na Elizabeti mkewe wote walikuwa watu wanyofu mbele za Mungu, wakizishika amri zote za Bwana na maagizo yote bila lawama.
7 Neil ei olnud lapsi, sest Eliisabet ei olnud selleks suuteline, ja nad mõlemad olid juba vanad.
Lakini walikuwa hawana watoto, kwa sababu Elizabeti alikuwa tasa; nao wote wawili walikuwa wazee sana.
8 Kui Sakarias teenis preestrina Jumala ees oma preesterlikus rühmas,
Siku moja ilipokuwa zamu ya kikundi cha Zekaria, yeye akifanya kazi ya ukuhani Hekaluni mbele za Mungu,
9 valiti ta vastavalt preestrite tavale liisu heitmisega Issanda templisse sisenema ja suitsutusrohtu põletama.
alichaguliwa kwa kura kwa kufuata desturi za ukuhani, kuingia Hekaluni mwa Bwana ili kufukiza uvumba.
10 Suitsutusohvri toomise ajal palvetas väljas suur hulk rahvast.
Nao wakati wa kufukiza uvumba ulipowadia, wale wote waliokuwa wamekusanyika ili kuabudu walikuwa nje wakiomba.
11 Issanda ingel ilmus Sakariasele ja seisis suitsutusohvrialtari kõrval paremal pool.
Ndipo malaika wa Bwana, akiwa amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia uvumba, akamtokea Zekaria.
12 Kui Sakarias nägi inglit, oli ta rabatud ja hakkas kartma.
Zekaria alipomwona huyo malaika, akafadhaika sana, akajawa na hofu.
13 Aga ingel ütles talle: „Ära karda, Sakarias! Sinu palvet on kuuldud ja su naine Eliisabet sünnitab sulle poja ja sa pead talle nimeks panema Johannes.
Lakini malaika akamwambia, “Usiogope, Zekaria, kwa maana Mungu amesikia maombi yako. Mkeo Elizabeti atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utamwita jina lake Yohana.
14 Ta toob sulle rõõmu ja heameelt ning tema sünd rõõmustab paljusid.
Yeye atakuwa furaha na shangwe kwako, nao watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.
15 Ta saab suureks Issanda silmis. Ta ei joo veini ega muid alkohoolseid jooke. Teda täidab Püha Vaim juba enne sündimist.
Kwa kuwa atakuwa mkuu mbele za Bwana, kamwe hataonja mvinyo wala kinywaji chochote cha kulevya, naye atajazwa Roho Mtakatifu hata kabla ya kuzaliwa kwake.
16 Ta pöörab paljud iisraellased tagasi Issanda, nende Jumala juurde.
Naye atawageuza wengi wa wana wa Israeli warudi kwa Bwana Mungu wao.
17 Ta läheb Issanda eel Eelija vaimus ja väes, et panna isad taas oma laste peale mõtlema, ning tuua need, kes on mässumeelsed, tagasi õige arusaamise juurde, et valmistada rahvas ette Issanda jaoks.“
Naye atatangulia mbele za Bwana katika roho na nguvu ya Eliya, ili kuigeuza mioyo ya baba kuwaelekea watoto wao, na wasiotii warejee katika hekima ya wenye haki, ili kuliweka tayari taifa lililoandaliwa kwa ajili ya Bwana.”
18 „Kuidas ma saan selles kindel olla?“küsis Sakarias inglilt. „Ma olen vana mees ja ka mu naine on eakas.“
Zekaria akamuuliza malaika, “Jambo hilo linawezekanaje? Mimi ni mzee na mke wangu pia ana umri mkubwa.”
19 „Mina olen Gabriel, “vastas ingel. „Ma seisan Jumala juures ning mind saadeti sinuga rääkima ja sulle seda head uudist tooma.
Malaika akamjibu, akamwambia, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele za Mungu, nami nimetumwa kwako ili nikuambie habari hizi njema.
20 Aga kuna sa ei uskunud seda, mida ma sulle rääkisin, jääd sa tummaks ega saa kõneleda kuni määratud hetkeni, mil mu sõnad täide lähevad.“
Basi sasa kwa kuwa hujaamini maneno yangu ambayo yatatimizwa kwa wakati wake, utakuwa bubu hadi siku ile mambo haya yatakapotukia.”
21 Väljas ootas rahvas Sakariast ja imestas, miks tal templis nii kaua aega läheb.
Wakati huo watu walikuwa wanamngojea Zekaria nje huku wakishangaa kukawia kwake mle Hekaluni.
22 Kui ta lõpuks välja tuli, ei saanud ta nendega rääkida. Nad mõistsid, et ta oli templis näinud nägemust, sest kuigi ta suutis teha žeste, ei suutnud ta üldse rääkida.
Alipotoka akawa hawezi kusema nao, wao wakatambua kuwa ameona maono ndani ya Hekalu. Lakini kwa kuwa alikuwa bubu, akawa anawaashiria kwa mikono.
23 Pärast seda, kui ta oma teenistusaja oli lõpetanud, läks ta koju tagasi.
Muda wake wa kuhudumu Hekaluni ulipomalizika, akarudi nyumbani kwake.
24 Mõne aja pärast jäi tema naine Eliisabet lapseootele. Ta jäi koju viieks kuuks.
Baada ya muda usio mrefu, Elizabeti mkewe akapata mimba, naye akajitenga kwa miezi mitano.
25 „Issand on seda mulle teinud, “ütles ta. „Nüüd on ta võtnud ära mu häbi teiste silmis.“
Akasema, “Hili ndilo Bwana alilonitendea aliponiangalia kwa upendeleo na kuniondolea aibu yangu mbele ya watu.”
26 Eliisabeti lapseootuse kuuendal kuul saatis Jumal ingel Gabrieli noore neiu juurde, kelle nimi oli Maarja ja kes elas Galileas Naatsareti linnas.
Mwezi wa sita baada ya Elizabeti kupata mimba, Mungu alimtuma malaika Gabrieli aende Galilaya katika mji wa Nazareti,
27 Ta oli kihlatud Joosepi-nimelise mehega.
kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu mmoja jina lake Yosefu wa nyumba ya Daudi. Jina la huyu mwanamwali bikira ni Maria.
28 Ingel tervitas teda. „Sul on eriline eesõigus, “ütles ta neiule. „Issand on sinuga.“
Naye malaika akaja kwake akamwambia: “Salamu, wewe uliyebarikiwa, Bwana yu pamoja nawe!”
29 Maarja oli neist sõnadest hämmelduses ja juurdles, mida selline tervitus tähendab.
Maria akafadhaishwa sana na maneno haya, akajiuliza moyoni, “Salamu hii ni ya namna gani?”
30 „Ära karda, Maarja, “jätkas ingel, „sest Jumal on osutanud sinu suhtes armulikkust.
Ndipo malaika akamwambia, “Usiogope, Maria, umepata kibali kwa Mungu.
31 Sa jääd lapseootele ja tood ilmale poja. Sa pead talle nimeks panema Jeesus.
Tazama, utachukua mimba, nawe utamzaa mtoto mwanaume na utamwita jina lake Yesu.
32 Ta saab väga tähtsaks ja teda nimetatakse Kõigekõrgema Pojaks. Issand Jumal annab talle tema isa Taaveti trooni
Yeye atakuwa mkuu, naye ataitwa Mwana wa Aliye Juu Sana. Bwana Mungu atampa kiti cha enzi cha Daudi baba yake.
33 ja ta valitseb igavesti Jaakobi järeltulijate üle. Tema kuningriik ei lõpe iial.“ (aiōn )
Ataimiliki nyumba ya Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” (aiōn )
34 „Kuidas see võimalik on?“küsis Maarja. „Ma olen alles neitsi.“
Maria akamuuliza huyo malaika, “Maadamu mimi ni bikira, jambo hili litawezekanaje?”
35 Ingel vastas: „Püha Vaim tuleb sinu peale ja Kõigekõrgema vägi varjab sind. Laps, kes sünnib, on püha, ja teda hüütakse Jumala pojaks.
Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, nazo nguvu zake Yeye Aliye Juu Sana zitakufunika kama kivuli. Kwa hiyo mtoto atakayezaliwa atakuwa mtakatifu, naye ataitwa Mwana wa Mungu.
36 Ja su sugulane Eliisabet on oma vanas eas samuti lapseootel. Naine, kelle kohta öeldi, et ta ei ole võimeline lapsi saama, on kuuendat kuud lapseootel.
Tazama, jamaa yako Elizabeti amechukua mimba katika uzee wake, na huu ni mwezi wake wa sita, yeye aliyeitwa tasa.
37 Jumala jaoks ei ole miski võimatu.“
Kwa maana kwa Mungu hakuna lisilowezekana.”
38 „Siin ma olen, valmis olema Issanda teenija, “ütles Maarja. „Sündigu minuga just nii, nagu sa ütlesid.“Seejärel ingel lahkus tema juurest.
Maria akasema, “Tazama, mimi ni mtumishi wa Bwana. Na iwe kwangu kama ulivyosema.” Kisha malaika akaondoka, akamwacha.
39 Veidi aja pärast pani Maarja end valmis ja kiirustas Juudamaa mägedesse, linna, kus oli
Wakati huo Maria akajiandaa, akaharakisha kwenda katika mji mmoja kwenye vilima vya Uyahudi.
40 Sakariase maja. Sisse astudes hõikas ta Eliisabetti.
Akaingia nyumbani kwa Zekaria na kumsalimu Elizabeti.
41 Kohe kui Eliisabet kuulis Maarja häält, hüppas laps tema ihus rõõmu pärast. Püha Vaim täitis Eliisabeti
Naye Elizabeti aliposikia salamu ya Maria, mtoto aliyekuwa tumboni mwake akaruka. Elizabeti akajazwa na Roho Mtakatifu,
42 ja ta hüüdis valju häälega: „Kui õnnistatud oled sina naiste hulgas ja kui õnnistatud on laps, kes sinust sünnib!
akapaza sauti kwa nguvu akasema, “Umebarikiwa wewe miongoni mwa wanawake, naye mtoto utakayemzaa amebarikiwa.
43 Miks mind nõnda austatakse, et mu Issanda ema mind külastab?
Lakini ni kwa nini mimi nimepata upendeleo kiasi hiki, hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?
44 Kui ma kuulsin sind tervitust hüüdmas, hüppas laps mu ihus rõõmu pärast.
Mara tu niliposikia sauti ya salamu yako, mtoto aliyeko tumboni mwangu aliruka kwa furaha.
45 Kui õnnelik sa oled, sest sa oled veendunud, et Issand teeb seda, mida ta sulle tõotas!“
Amebarikiwa yeye aliyeamini kwamba lile Bwana alilomwambia litatimizwa.”
46 Maarja vastas: „Kuidas ma ülistan Issandat!
Naye Maria akasema: “Moyo wangu wamwadhimisha Bwana,
47 Olen väga õnnelik Jumalas, mu Päästjas,
nayo roho yangu inamfurahia Mungu Mwokozi wangu,
48 sest ta otsustas, et mina, tema teenija, olen oma tagasihoidlikust taustast hoolimata tema silmis väärtuslik. Nüüdsest peale ütlevad kõik põlvkonnad, et ma olen õnnistatud.
kwa kuwa ameangalia kwa fadhili unyonge wa mtumishi wake. Hakika tangu sasa vizazi vyote vitaniita aliyebarikiwa,
49 Kõigeväeline Jumal on teinud mulle suuri asju, tema nimi on püha.
kwa maana yeye Mwenye Nguvu amenitendea mambo ya ajabu: jina lake ni takatifu.
50 Tema halastus kestab põlvest põlve nendele, kes teda austavad.
Rehema zake huwaendea wale wamchao, kutoka kizazi hadi kizazi.
51 Oma suure jõuga on ta lõhkunud tükkideks need, kes ülbelt ennast targaks peavad.
Kwa kuwa ametenda mambo ya ajabu kwa mkono wake; amewatawanya wale wenye kiburi ndani ya mioyo yao.
52 Ta kisub mõjukad nende troonidelt maha ja ülendab need, kes on alandlikud.
Amewashusha watawala toka kwenye viti vyao vya enzi, lakini amewainua wanyenyekevu.
53 Ta annab näljastele häid asju süüa ja saadab rikkad tühje käsi minema.
Amewashibisha wenye njaa kwa vitu vizuri, bali matajiri amewafukuza mikono mitupu.
54 Ta on aidanud oma sulast Iisraeli ja pidanud teda halastuses meeles,
Amemsaidia mtumishi wake Israeli, kwa kukumbuka ahadi yake ya kumrehemu
55 just nagu ta meie isadele, Aabrahamile ja tema järeltulijatele, igaveseks ajaks tõotas.“ (aiōn )
Abrahamu na uzao wake milele, kama alivyowaahidi baba zetu.” (aiōn )
56 Maarja jäi Eliisabeti juurde kolmeks kuus ja naasis siis koju.
Maria akakaa na Elizabeti karibu miezi mitatu, kisha akarudi nyumbani kwake.
57 Eliisabetil jõudis sünnitamise aeg kätte ja ta tõi ilmale poja.
Ulipowadia wakati wa Elizabeti kujifungua, alizaa mtoto mwanaume.
58 Naabrid ja sugulased kuulsid, kuidas Issand oli talle oma suurt headust osutanud, ning nad tähistasid seda koos temaga.
Majirani zake na jamii zake wakasikia jinsi Bwana alivyomfanyia rehema kuu, nao wakafurahi pamoja naye.
59 Kaheksa päeva pärast tulid nad poissi ümber lõikama. Nad kavatsesid talle isa järgi nimeks panna Sakarias.
Siku ya nane wakaja kumtahiri mtoto, wakataka yule mtoto aitwe Zekaria, ambalo ndilo jina la baba yake.
60 „Ei, “ütles Eliisabet. „Tema nimeks peab saama Johannes.“
Lakini mama yake akakataa na kusema, “Hapana! Jina lake ataitwa Yohana.”
61 „Aga teie sugulaste hulgas pole kedagi, kellel see nimi oleks, “ütlesid nad talle.
Wakamwambia, “Hakuna mtu yeyote katika jamaa yako mwenye jina kama hilo.”
62 Žestide abil küsisid nad Sakariaselt, poisi isalt, mis nime tahaks ta oma pojale panna.
Basi wakamfanyia Zekaria baba yake ishara ili kujua kwamba yeye angependa kumpa mtoto jina gani.
63 Sakarias andis märku, et talle antaks midagi, mille peale kirjutada. Kõigi üllatuseks kirjutas ta: „Tema nimi on Johannes.“
Akaomba wampe kibao cha kuandikia na kwa mshangao wa kila mtu akaandika: “Jina lake ni Yohana.”
64 Kohe suutis ta jälle rääkida ja hakkas Jumalat ülistama.
Papo hapo kinywa chake kikafunguliwa na ulimi wake ukaachiwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.
65 Kõiki läheduses elavaid inimesi täitis juhtunu tõttu aukartus ning kuuldus sellest levis kogu Juuda mägismaal.
Majirani wote wakajawa na hofu ya Mungu, na katika nchi yote ya vilima vya Uyahudi watu walikuwa wakinena juu ya mambo haya yote.
66 Igaüks, kes seda kuulis, mõtles, mida see peaks tähendama. „Kes sellest poisist saab?“küsisid nad, sest oli selge, et ta oli Jumala jaoks väga eriline.
Kila aliyesikia habari hizi alishangaa akauliza, “Je, mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana mkono wa Bwana ulikuwa pamoja naye.
67 Tema isa Sakarias täitus Püha Vaimuga ja kuulutas prohvetlikult:
Zekaria, baba yake, akajazwa na Roho Mtakatifu, naye akatoa unabii, akisema:
68 „Issand, Iisraeli Jumal, on imeline, sest ta on tulnud oma rahva juurde ja nad vabastanud.
“Ahimidiwe Bwana, Mungu wa Israeli, kwa kuwa amewajilia watu wake na kuwakomboa.
69 Ta on andnud meile suure Päästja oma sulase Taaveti järglaste hulgast,
Naye ametusimamishia pembe ya wokovu katika nyumba ya Daudi mtumishi wake,
70 nagu ta tõotas ammu aega tagasi oma pühade prohvetite kaudu. (aiōn )
kama alivyonena kwa vinywa vya manabii wake watakatifu tangu zamani, (aiōn )
71 Ta tõotas päästa meid meie vaenlaste käest, nende käest, kes meid vihkavad.
kwamba atatuokoa kutoka kwa adui zetu, na kutoka mikononi mwao wote watuchukiao:
72 Ta halastas meie isade peale ja pidas meeles oma püha lepingut −
ili kuonyesha rehema kwa baba zetu na kukumbuka Agano lake takatifu,
73 tõotust, mille ta oli andnud meie isale Aabrahamile.
kiapo alichomwapia baba yetu Abrahamu:
74 Ta vabastab meid hirmust ja päästab meid meie vaenlaste käest,
kutuokoa kutoka mikononi mwa adui zetu, tupate kumtumikia yeye pasipo hofu
75 et saaksime teda teenida ning teha kogu oma elu seda, mis on hea ja õige.
katika utakatifu na haki mbele zake, siku zetu zote.
76 Kuigi sa oled alles väike laps, hüütakse sind Kõigekõrgema prohvetiks, sest sa lähed Issanda eel valmistama talle teed ja
“Nawe mtoto wangu, utaitwa nabii wa Aliye Juu Sana; kwa kuwa utamtangulia Bwana na kuandaa njia kwa ajili yake,
77 kuulutama tema rahvale teadmisi päästest pattude andestuse kaudu.
kuwajulisha watu wake juu ya wokovu utakaopatikana kwa kusamehewa dhambi zao,
78 Tänu Jumala hoolitsevale headusele laseb taevas meile koiduvalgust paista,
kwa ajili ya wingi wa rehema za Mungu wetu, nuru itokayo juu itatuzukia
79 et see säraks neile, kes elavad pimeduses ja surma varjus, ning juhiks meid rahu teel.“
ili kuwaangazia wale waishio gizani na katika uvuli wa mauti, kuiongoza miguu yetu katika njia ya amani.”
80 Poiss Johannes kasvas ja sai vaimulikult tugevaks. Ta elas kõrbes, kuni jõudis kätte aeg avalikult Iisraeli teenida.
Yule mtoto akakua na kuongezeka nguvu katika roho; akaishi nyikani hadi siku ile alipojionyesha hadharani kwa Waisraeli.