< Markus 4 >

1 Jeesus hakkas taas mere ääres õpetama. Teda tuli kuulama nii palju rahvast, et ta astus paati ja istus vee peal paadis, sel ajal kui rahvas kuulas teda kaldal.
Yesu akaanza kufundisha tena kando ya bahari. Umati wa watu uliokuwa umekusanyika kumzunguka ulikuwa mkubwa, kiasi kwamba ilimbidi Yesu aingie kwenye mashua iliyokuwa baharini na kuketi humo, nao watu wote walikuwa ufuoni mwa bahari.
2 Ta näitlikustas oma õpetusi paljude lugudega.
Akawafundisha mambo mengi kwa mifano, naye katika mafundisho yake akasema:
3 „Kuulake, “ütles ta. „Üks külvaja läks välja külvama.
“Sikilizeni! Mpanzi alitoka kwenda kupanda mbegu zake.
4 Kui ta külvates seemneid laiali puistas, kukkus osa teerajale, linnud tulid ja sõid seemned sealt ära.
Alipokuwa akitawanya mbegu, nyingine zilianguka kando ya njia, nao ndege wakaja na kuzila.
5 Osa seemneid pudenes kivisele pinnale, kus ei olnud eriti mulda. Madalas mullakihis hakkasid taimed kiiresti kasvama, aga kuna mullakiht ei olnud sügav,
Nyingine zilianguka kwenye ardhi yenye mwamba isiyo na udongo wa kutosha. Zikaota haraka, kwa kuwa udongo ulikuwa haba.
6 kõrvetas päike taimi. Kuna neil ei olnud päris juuri, närbusid taimed peagi.
Lakini jua lilipozidi, mimea ikanyauka na kukauka kwa kuwa mizizi yake haikuwa na kina.
7 Osa seemneid pudenes ohakate sekka. Ohakad kasvasid suureks ja lämmatasid tärkava orase, nii et sellest ei tulnud midagi.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye miiba, nayo miiba hiyo ikakua, ikaisonga hiyo mimea, hivyo haikutoa mazao.
8 Osa seemneid langes heale pinnasele, kus nad idanesid ja kasvasid ning andsid saagiks mõni kolmkümmend, mõni kuuskümmend ja mõni sada korda külvatust rohkem.
Mbegu nyingine zilianguka kwenye udongo mzuri, zikaota vizuri na kukua, zikatoa mazao, moja mara thelathini, nyingine mara sitini, na nyingine mara mia moja.”
9 Kui teil on kuulmiseks kõrvad, siis kuulake, mida ma teile räägin.“
Kisha Yesu akasema, “Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
10 Kui Jeesus oli omapead, küsisid kaksteist jüngrit ja teised, kes olid koos temaga, mida need võrdlused tähendasid.
Alipokuwa peke yake, watu waliokuwepo naye pamoja na wanafunzi wake kumi na wawili wakamuuliza kuhusu mifano yake.
11 Ta ütles neile: „Teie saate Jumala riigi mõistatusest aru. Kuid kõrvalseisjatel on ainult lood,
Naye akawaambia, “Ninyi mmepewa kujua siri ya Ufalme wa Mungu. Lakini kwa wale walioko nje, kila kitu husemwa kwao kwa mifano,
12 nii et kuigi nad näevad, nad tegelikult ei „näe“, ja kuigi nad kuulevad, nad ei mõista, muidu pöörduksid nad minu poole ja saaksid andeks.“
ili, “‘daima waone lakini wasitambue, daima wasikie lakini wasielewe; wasije wakageuka, wakatubu na kusamehewa!’”
13 „Kas te ei saa sellest loost aru?“küsis Jeesus neilt. „Kui ei saa, kuidas te siis kõigist ülejäänud lugudest aru saate?
Kisha Yesu akawauliza, “Hamwelewi maana ya mfano huu? Basi mtaelewaje mifano mingine?
14 Külvaja külvab sõna.
Yule mpanzi hupanda neno.
15 Seemned rajal, kuhu sõna külvati, kujutavad neid, kes kuulevad sõnumit, kuid siis tuleb kohe Saatan ja võtab ära sõna, mis neisse on külvatud.
Hawa ndio wale walio kando ya njia ambako neno lilipandwa. Walisikiapo neno, Shetani huja mara na kulinyakua lile neno lililopandwa ndani yao.
16 Samal kombel kujutab kivine pind, kuhu seemned langesid, neid, kes kuulevad sõna ja võtavad selle kohe rõõmuga vastu.
Nazo zile mbegu zilizoanguka kwenye udongo wenye miamba, ni wale wanaolisikia neno, na mara hulipokea kwa furaha.
17 Aga kuna neil ei ole päris juuri, jäävad nad püsima ainult veidikeseks ajaks, kuni tulevad probleemid või tagakiusamine, ja siis langevad nad kiiresti.
Lakini kwa kuwa hawana mizizi, wao hudumu kwa muda mfupi tu. Kisha dhiki au mateso yanapoinuka kwa ajili ya lile neno, mara wao huiacha imani.
18 Ohakate sekka külvatu kujutab neid, kes kuulevad sõna,
Lakini wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye miiba, hulisikia lile neno;
19 kuid selle maailma mured, rikkuse ahvatlus ja muud segavad asjaolud lämmatavad sõna kasvu ja see ei kanna vilja. (aiōn g165)
lakini masumbufu ya maisha haya, na udanganyifu wa mali na tamaa ya mambo mengine huja na kulisonga lile neno na kulifanya lisizae. (aiōn g165)
20 Ent heale pinnasele külvatud seemned kujutavad neid, kes kuulevad sõna, võtavad selle vastu ja kannavad vilja, andes kolmkümmend, kuuskümmend ja sada korda rohkem kui külvati.
Wengine, kama mbegu iliyopandwa kwenye udongo mzuri, hulisikia lile neno, wakalipokea na kuzaa mazao. Wao huzaa mara thelathini, au mara sitini, au mara mia ya mbegu iliyopandwa.”
21 Kes paneb lambi ämbri või voodi alla?“küsis Jeesus neilt. „Ei, lamp pannakse üles lambijalale.
Akawaambia, “Je, taa huwashwa na kufunikwa chini ya kikapu au mvunguni mwa kitanda? Je, haiwashwi na kuwekwa juu ya kinara chake?
22 Kõik, mis on varjatud, tuleb ilmsiks ja kõik, mis on salajas, saab avalikuks.
Kwa kuwa hakuna kilichofichika ambacho hakitafunuliwa, wala hakuna jambo lolote la siri ambalo halitaletwa nuruni.
23 Kui teil on kõrvad kuulmiseks, siis kuulake, mida ma räägin!
Mwenye masikio ya kusikia, na asikie.”
24 Pange tähele seda, mida te kuulete, “ütles ta neile, „sest teile antakse vastavalt sellele, kui palju tahate vastu võtta, mõõt mõõdu eest.
Naye akawaambia, “Kuweni waangalifu na yale mnayosikia. Kipimo kile mpimacho, ndicho mtakachopimiwa ninyi, hata na zaidi.
25 Neile, kel juba on arusaamine, antakse rohkem, kuid neilt, kes ei taha teada, võetakse ära seegi vähene arusaamine, mis neil on.
Kwa maana kila mtu aliye na kitu atapewa zaidi, naye atakuwa navyo tele. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho atanyangʼanywa.”
26 Jumala riik on nagu mees, kes külvab põllule seemet, “ütles Jeesus.
Pia akawaambia, “Ufalme wa Mungu unafanana na mtu apandaye mbegu shambani.
27 „Ta läheb magama ja tõuseb varakult üles ja nii iga päev, kuid ta ei tea, kuidas seeme idaneb ja tärkab.
Akiisha kuzipanda, usiku na mchana, akiwa amelala au ameamka, mbegu huota na kukua pasipo yeye kujua ikuavyo.
28 Maa annab saaki iseenesest. Kõigepealt tuleb välja oras, seejärel viljapea ja siis küpse viljaga pea.
Udongo huifanya iote kuwa mche, halafu suke, kisha nafaka kamili kwenye suke.
29 Kui vili on küps, koristab põllumees selle sirbiga, sest saak on valmis.
Lakini nafaka inapokuwa imekomaa, mara mkulima huingia shambani na mundu wa kuvunia, maana mavuno yamekuwa tayari.”
30 Millega võrrelda Jumala riiki? Missugust näidet kasutada?“küsis ta.
Akawaambia tena, “Tuufananishe Ufalme wa Mungu na nini? Au tutumie mfano gani ili kuueleza?
31 „See on nagu sinepiseeme − kõige pisem seeme.
Ni kama punje ya haradali, ambayo ni mbegu ndogo sana kuliko mbegu zote zinazopandwa ardhini.
32 Aga kui see maha külvata, siis kasvab sellest taim, mis on suurem kui teised taimed. Selle oksad on piisavalt suured, nii et linnud saavad seal varjus olla.“
Lakini ikishaota, hukua ikawa mmea mkubwa kuliko yote ya bustanini, ikawa na matawi makubwa hata ndege wa angani wanaweza kujenga viota kwenye matawi yake.”
33 Jeesus kasutas rahvale kõneledes palju selliseid näitlikke lugusid, et nad mõistaksid võimalikult hästi.
Kwa mifano mingine mingi kama hii Yesu alinena nao neno lake, kwa kadiri walivyoweza kulielewa.
34 Õigupoolest kasutas ta avalikult rääkides üksnes jutustusi, kuid omaette olles selgitas ta oma jüngritele kõike.
Hakusema nao neno lolote pasipo mfano. Lakini alipokuwa na wanafunzi wake, aliwafafanulia kila kitu.
35 Samal päeval hiljem − õhtul − ütles ta oma jüngritele: „Lähme üle mere teisele poole.“
Siku hiyo ilipokaribia jioni, aliwaambia wanafunzi wake, “Tuvukeni twende mpaka ngʼambo.”
36 Jätnud rahvahulga maha, läksid jüngrid koos Jeesusega paati. Nende juures oli veel teisigi paate.
Wakauacha ule umati wa watu, na wakamchukua vile alivyokuwa kwenye mashua. Palikuwa pia na mashua nyingine nyingi pamoja naye.
37 Peagi hakkas möllama kohutav torm, lained paiskusid vastu paati ja lõid vett sisse.
Kukawa na dhoruba kali, nayo mawimbi yakaipiga ile mashua hata ikawa karibu kujaa maji.
38 Jeesus magas ahtris, pea padjale toetatud. Jüngrid äratasid ta kisendades: „Õpetaja, kas sa ei hooli sellest, et me oleme uppumas?“
Yesu alikuwa katika shetri, akiwa analala juu ya mto. Wanafunzi wake wakamwamsha, wakamwambia, “Mwalimu, hujali kama tunazama?”
39 Jeesus ärkas. Ta käskis tuulel vaibuda ja ütles lainetele: „Rahunege! Ärge möllake!“Tuul vaibus ja vesi jäi täiesti tüüneks.
Akaamka, akaukemea ule upepo, akayaambia yale mawimbi, “Uwe kimya! Tulia!” Ule upepo ukatulia, kukawa shwari kabisa.
40 „Miks te nii väga kohkusite? Kas te ei ole õppinud mind usaldama?“küsis ta neilt.
Yesu akawaambia wanafunzi wake, “Kwa nini mnaogopa hivyo? Je, bado hamna imani?”
41 Nad olid jahmunud ja ehmunud. Nad küsisid üksteiselt: „Kes ta ometi on? Isegi tuul ja lained kuuletuvad talle!“
Nao wakawa wameogopa sana, wakaulizana, “Ni nani huyu ambaye hata upepo na mawimbi vinamtii?”

< Markus 4 >