< Job 41 >

1 Kan du draga Leviathan med en krok, och fatta hans tungo med ett snöre?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 Kan du sätta honom en ring i näsona, och borra honom hans kindben igenom med en syl?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 Menar du, att han skall mycket bedjas före, eller smeka dig?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 Menar du, att du kan göra ett förbund med honom, att du må hafva honom till en träl evinnerliga?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 Kan du spela med honom såsom med en fogel; eller binda honom dinom pigom?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 Menar du, att sällskapet skola skära honom sönder, att han blifver utdelad ibland köpmännerna?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 Kan du fylla ena not med hans hud, och någon fiskaryssjo med hans hufvud?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 När du kommer dina hand vid honom, så kom ihåg, att det en strid är, den du icke uthålla kan.
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 Si, hans hopp skall fela honom, och han skall uppenbarligen fördrifven varda.
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 Ingen är så dristig, att han honom uppväcka tör. Ho är då den, som för mig bestå kan?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 Ho hafver något gifvit mig tillförene, att jag må honom det vedergälla? Mitt är allt det under hela himmelen är.
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 Jag vill icke förtiga hans kraft; ej heller hans magt, eller huru välskapad han är.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 Ho kan upptäcka honom hans kläde? Eller ho tör vågat, att fatta honom i tänderna?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 Ho kan öppna hans anletes kindben? Förskräckeliga stå hans tänder allt omkring.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 Hans fjäll äro lika som sköldar, sammanfäste hvar i annan.
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 Det ena hänger in i det andra, så att vädret icke går deremellan;
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 Det hänger hvar i annan, och hålla sig tillsammans, så att de icke kunna skiljas åt.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 Hans njusande är såsom ett glimmande ljus; hans ögon äro såsom morgonrodnans ögnahvarf.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 Utaf hans mun fara bloss och eldbrandar.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 Utaf hans näso går rök, såsom utaf heta grytor och kettlar.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 Hans ande är glödande kol, och utu hans mun går låge.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 Han hafver en starkan hals, och det är honom lust, då han något förderfvar.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 Hans kötts ledamot hänga vid hvartannat; de äro faste i honom, att han icke rörd varder.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 Hans hjerta är hårdt såsom sten, och så fast som ett stycke af understenen i qvarnene.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 När han reser sig, förfära sig de starke; och när han får dem fatt, är der ingen nåde.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 Om man vill till honom med svärd, så rörer han sig intet; eller med spets, skott och harnesk.
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 Han aktar jern såsom strå, och koppar såsom ruttet trä.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 Ingen skytte förjagar honom; slungostenar äro honom såsom agnar.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Hammaren aktar han såsom strå; han bespottar de bäfvande spetsar.
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 Han kan ligga på skarpt grus; han lägger sig uppå det skarpt är, såsom på dyngo.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 Han gör, att djupa hafvet sjuder såsom en gryta, och rörer det ihop, såsom man blandar ena salvo.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 Efter honom är vägen ljus; djupet aktar han såsom en gamlan gråhårotan.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 På jordene kan ingen liknas honom; han är gjord till att vara utan fruktan.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 Han föraktar allt det högt är; han är Konung öfver alla högmodiga.
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”

< Job 41 >