< Tito 3 >

1 Wakumbushe watu kuwastahi watawala na wenye mamlaka, kuwatii na kuwa tayari kwa kila namna kutenda mambo yote mema.
Remind them to be in subjection to rulers and to authorities, to be obedient, to be ready for every good work,
2 Waambie wasimtukane mtu yeyote; bali waishi kwa amani na masikizano, wawe daima wapole kwa kila mtu.
to speak evil of no one, not to be contentious, to be gentle, showing courtesy to all people.
3 Maana, wakati mmoja sisi tulikuwa wapumbavu, wakaidi na wapotovu. Tulikuwa watumwa wa tamaa na anasa za kila aina. Tuliishi maisha ya uovu na wivu; watu walituchukia nasi tukawachukia.
For we were also once foolish, disobedient, deceived, serving various lusts and pleasures, living in malice and envy, hateful, and hating one another.
4 Lakini wakati wema na upendo wa Mungu, Mwokozi wetu, ulipofunuliwa,
But when the kindness of God our Savior and his love toward humankind appeared,
5 alituokoa. alituokoa si kwa sababu ya jambo lolote jema tulilotenda sisi, bali alituokoa kwa sababu ya huruma yake, kwa njia ya Roho Mtakatifu anayetujalia tuzaliwe upya na kuwa na maisha mapya kwa kutuosha kwa maji.
not by works of righteousness, which we did ourselves, but according to his mercy, he saved us, through the washing of rebirth and renewing by the Holy Spirit,
6 Mungu alitumiminia Roho Mtakatifu bila kipimo kwa njia ya Yesu Kristo, Mwokozi wetu,
whom he poured out on us richly, through Jesus Christ our Savior;
7 ili kwa neema yake tupate kukubaliwa kuwa waadilifu na kuupokea uzima wa milele tunaoutumainia. (aiōnios g166)
that, being justified by his grace, we might be made heirs according to the hope of everlasting life. (aiōnios g166)
8 Jambo hili ni kweli. Ninakutaka uyatilie mkazo mambo haya, ili wale wanaomwamini Mungu, wawe na hamu ya kuutumia wakati wao katika kutenda mema, ambayo ni mambo mazuri na ya manufaa kwa watu.
This saying is faithful, and concerning these things I desire that you affirm confidently, so that those who have believed God may be careful to maintain good works. These things are good and profitable for people;
9 Lakini jiepushe na ubishi wa kipumbavu, ugomvi na mabishano juu ya Sheria. Mambo hayo hayana faida yoyote na ni ya bure tu.
but shun foolish questionings, genealogies, strife, and disputes about the law; for they are unprofitable and vain.
10 Mtu anayesababisha mafarakano mpe onyo la kwanza na la pili, kisha achana naye.
Reject a divisive person after a first and second warning;
11 Wajua kwamba mtu wa namna hiyo amepotoka kabisa, na dhambi zake zathibitisha kwamba amekosea.
knowing that such a one is perverted, and sins, being self-condemned.
12 Baada ya kumtuma kwako Artema au Tukiko, fanya bidii kuja Nikopoli unione, maana nimeamua kukaa huko wakati wa majira ya baridi.
When I send Artemas to you, or Tychicus, be diligent to come to me to Nicopolis, for I have determined to winter there.
13 Jitahidi kumsaidia mwana sheria Zena na Apolo ili waweze kuanza ziara zao na uhakikishe kwamba wana kila kitu wanachohitaji.
Send Zenas, the Law scholar, and Apollos on their journey speedily, that nothing may be lacking for them.
14 Ni lazima watu wetu wajifunze kuutumia wakati wao katika kutenda mema ili wasaidie katika mahitaji ya kweli, na maisha yao yawe ya kufaa.
Let our people also learn to maintain good works for necessary uses, that they may not be unfruitful.
15 Watu wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu rafiki zetu katika imani. Nawatakieni nyote neema ya Mungu.
All who are with me greet you. Greet those who love us in faith. Grace be with you all.

< Tito 3 >