< Tito 2 >
1 Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho safi.
But say the things which fit sound doctrine,
2 Waambie wazee kwamba wanapaswa kuwa na kiasi, wawe na busara na wataratibu; wanapaswa kuwa timamu katika imani yao, upendo na uvumilivu.
that older men should be sober-minded, worthy of respect, self-controlled, sound in faith, in love, and in patience:
3 Hali kadhalika waambie wanawake wazee wawe na mwenendo wa uchaji wa Mungu; wasiwe wachongezi, au watumwa wa pombe. Wanapaswa kufundisha mambo mema,
and that older women likewise be reverent in behavior, not slanderers nor enslaved to much wine, teachers of that which is good;
4 ili wawazoeze kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto,
that they may train the young women to love their husbands, to love their children,
5 wawe na kiasi na safi, waangalie vizuri mambo ya nyumbani, na wawatii waume zao, ili ujumbe wa Mungu usije ukadharauliwa.
to be self-controlled, pure, working at home, kind, and being subject to their own husbands, so that God's word may not be discredited.
6 Kadhalika, wahimize vijana wawe na kiasi.
Likewise, exhort the younger men to be self-controlled;
7 Katika mambo yote wewe mwenyewe unapaswa kuwa mfano wa matendo mema. Uwe mnyofu na uwe na uzito katika mafundisho yako.
in all things showing yourself an example of good works. In your teaching show integrity, seriousness,
8 Maneno yako yasiwe na hitilafu yoyote ili adui zako waaibike wasipopata chochote kibaya cha kusema juu yetu.
and a sound message that cannot be condemned; that he who opposes you may be ashamed, having no evil thing to say about us.
9 Watumwa wanapaswa kuwatii wakuu wao na kuwapendeza katika mambo yote. Wasibishane nao,
Exhort servants to be in subjection to their own masters, and to be well-pleasing in all things; not contradicting;
10 au kuiba vitu vyao. Badala yake wanapaswa kuonyesha kwamba wao ni wema na waaminifu daima, ili, kwa matendo yao yote, wayapatie sifa njema mafundisho juu ya Mungu, Mwokozi wetu.
not stealing, but showing all good fidelity; that they may adorn the doctrine of God, our Savior, in all things.
11 Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.
For the grace of God has appeared, bringing salvation to all people,
12 Neema hiyo yatufunza kuachana na uovu wote na tamaa za kidunia; tuwe na kiasi, tuishi maisha adili na ya kumcha Mungu katika ulimwengu huu wa sasa, (aiōn )
instructing us to say "No" to ungodliness and worldly desires, and to live soberly, righteously, and godly in this present age; (aiōn )
13 tukiwa tunangojea siku ile ya heri tunayoitumainia, wakati utakapotokea utukufu wa Mungu Mkuu na Mwokozi wetu Yesu Kristo.
looking for the blessed hope and appearing of the glory of our great God and Savior, Jesus Christ;
14 Yeye alijitoa mwenyewe kwa ajili yetu ili atukomboe kutoka katika uovu wote na kutufanya watu safi walio wake yeye mwenyewe, watu walio na hamu ya kutenda mema.
who gave himself for us, that he might redeem us from all iniquity, and purify for himself a people for his own possession, zealous for good works.
15 Basi, fundisha mambo hayo na tumia mamlaka yako yote ukiwahimiza na kuwaonya wasikilizaji wako. Mtu yeyote na asikudharau.
Say these things and exhort and reprove with all authority. Let no one despise you.