< Mathayo 2 >
1 Yesu alizaliwa mjini Bethlehemu, mkoani Yudea, wakati Herode alipokuwa mfalme. Punde tu baada ya kuzaliwa kwake, wataalamu wa nyota kutoka mashariki walifika Yerusalemu,
當黑落德為王時,耶穌誕生在猶大的白冷;看,有賢士從東方來到耶路撒冷,說:
2 wakauliza, “Yuko wapi mtoto, Mfalme wa Wayahudi, aliyezaliwa? Tumeiona nyota yake ilipotokea mashariki, tukaja kumwabudu.”
「才誕生的猶太人君王在哪裏﹖我們在東方見了衪的星,特來朝拜衪。」
3 Mfalme Herode aliposikia hayo, alifadhaika, yeye pamoja na wakazi wote wa Yerusalemu.
黑落德王一聽說,就驚慌起來,全耶路撒冷也同他一起驚慌。
4 Basi akawaita pamoja makuhani wakuu wote na walimu wa Sheria, akawauliza, “Kristo atazaliwa wapi?”
他便召集了眾司祭和民間的經師,仔細考問他們:默西亞應當生在哪裏。
5 Nao wakamjibu, “Mjini Bethlehemu, mkoani Yudea. Ndivyo nabii alivyoandika:
他們對他說:「在猶太的白冷,因為先知曾這樣記載:
6 Ewe Bethlehemu katika nchi ya Yuda, kwa vyovyote wewe si mdogo kabisa kati ya viongozi wa Yuda; maana kwako atatokea kiongozi atakayewaongoza watu wangu, Israeli.”
『你猶大的白冷啊!你在猶大的群邑中,決不是最小的,因為將由你出來一位領袖,衪將牧養我的百姓以色列。』
7 Hapo, Herode aliwaita faraghani hao wataalamu wa nyota, akawauliza wakati hasa ile nyota ilipowatokea.
於是黑落德暗暗把賢士叫來,你細詢問他們那星出現的時間;
8 Kisha akawatuma Bethlehemu akisema, “Nendeni mkachunguze kwa makini habari za mtoto huyo. Mkisha mpata nileteeni habari ili nami niende nikamwabudu.”
然後打發他們往白冷去,說:你們去仔細尋訪嬰孩,幾時找到了給我報信,好讓我也去朝拜衪。」
9 Baada ya kumsikiliza mfalme, hao wataalamu wa nyota wakaenda. Kumbe ile nyota waliyokuwa wameiona upande wa mashariki iliwatangulia hata ikaenda kusimama juu ya mahali pale alipokuwa mtoto.
他們聽了王的話,就走了。看,他們在東方所見的那星,走在他們前面,直至來到嬰所在的地方,就停在面。
10 Walipoiona hiyo nyota, walifurahi mno.
他們一見到那星,極其高興喜歡。
11 Basi, wakaingia nyumbani, wakamwona yule mtoto pamoja na Maria mama yake; wakapiga magoti, wakamsujudia. Kisha wakafungua hazina zao, wakampa zawadi: dhahabu, ubani na manemane.
他們走進屋內,看見嬰兒和他的母親瑪利亞,遂俯伏朝拜了衪,打開自己的寶匣,給衪奉獻了禮物,即黃金、乳香和歿藥。
12 Mungu aliwaonya katika ndoto wasimrudie Herode; hivyo wakarudi makwao kwa njia nyingine.
他們在夢中得到啟示,不要回到黑落德那裏,就由另一條路返回自己的地方去了。
13 Baada ya wale wageni kuondoka, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto, akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, mkimbilie Misri. Kaeni huko mpaka nitakapokwambia, maana Herode anakusudia kumwua huyu mtoto.”
他們離去後,看,上主的天使顯於若瑟說:「起來,帶著嬰孩和衪的母親,逃往埃及去,住在那裏,直到我再通知你,因為黑落德即將尋找這嬰孩,要把衪殺掉。」
14 Hivyo, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akaondoka usiku, akaenda Misri.
若瑟便起來,星夜帶口嬰孩姓衪的母親,退避到屐及去口
15 Akakaa huko mpaka Herode alipokufa. Jambo hilo lilifanyika ili neno alilosema Bwana kwa njia ya nabii litimie: “Nilimwita Mwanangu kutoka Misri.”
留在那裏,直到黑落德死去。這就應驗了上主藉先知所說的話:「我從埃及召回了我失兒子。」
16 Herode alipogundua kwamba wale wataalamu wa nyota walikuwa wamemhadaa, alikasirika sana. Akaamuru watoto wote wa kiume mjini Bethlehemu na kandokando yake wenye umri wa miaka miwili na chini yake wauawe. Alifanya hivyo kufuatana na muda aliopata kujua kutoka kwa wale wataalamu wa nyota.
那時,黑落德見了自己受了士們的愚弄,就大發忿怒,依照他由賢士們所探得的時期,差人將白冷及其周圍境內所有兩歲及兩歲以下的嬰兒殺死,
17 Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyosemwa kwa njia ya nabii Yeremia:
於是應驗了耶肋米亞先知所說的話:
18 “Sauti imesikika mjini Rama, kilio na maombolezo mengi. Raheli anawalilia watoto wake, wala hataki kutulizwa, maana wote wamefariki.”
「在辣瑪聽到了聲音,痛哭哀號不止;辣黑爾痛哭她的子女,不願受人安慰,因為他們不在了。」
19 Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri,
黑落德死後,看,上主的天使在埃及托夢顯於若瑟說:
20 akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa.”
「起來,帶著孩子和衪的母親,往以色列地去,因為那些謀殺孩子性命的人死了。」
21 Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli.
他便起來,帶著孩子和衪的母親,進了以色列地域;
22 Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya,
但是一聽說阿爾赫勞繼他父親黑落德作了猶太王,就害怕到那裏去;夢人得到了啟示後,便退避到加里肋亞境內,
23 akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa Mnazare.”
去住在一座名叫納匝肋的城中,如此應驗了先知所說的話:「衪將稱為納匝肋人。」