+ Mathayo 1 >
1 Yesu Kristo alikuwa mzawa wa Daudi, mzawa wa Abrahamu. Hii ndiyo orodha ya ukoo wake:
亞巴郎之子,達味之子耶穌基督的祖譜:
2 Abrahamu alimzaa Isaka, Isaka alimzaa Yakobo, Yakobo alimzaa Yuda na ndugu zake,
亞巴郎生依撒各,依撒各生雅各伯,雅各伯生猶大和他的兄弟們;
3 Yuda alimzaa Faresi na Zera (mama yao alikuwa Tamari), Faresi alimzaa Hesroni, Hesroni alimzaa Rami,
猶由塔瑪爾生培勒茲和則辣黑,培勒茲生赫茲龍,赫茲龍生阿蘭,
4 Rami alimzaa Aminadabu, Aminadabu alimzaa Nashoni, Nashoni alimzaa Salmoni,
阿蘭生阿米納達布,阿米納達布生納赫雄,納赫雄生撒爾孟,
5 Salmoni alimzaa Boazi (mama yake Boazi alikuwa Rahabu). Boazi na Ruthi walikuwa wazazi wa Obedi, Obedi alimzaa Yese,
撒爾孟由辣哈布生波阿次,波阿次由盧德生敖貝得,敖貝得生葉瑟,
6 naye Yese alimzaa Mfalme Daudi. Daudi alimzaa Solomoni (mama yake Solomoni alikuwa mke wa Uria).
葉瑟生達味王。達味由烏黎雅的妻子生撒羅滿,
7 Solomoni alimzaa Rehoboamu, Rehoboamu alimzaa Abiya, Abiya alimzaa Asa,
撒羅滿生勒哈貝罕,勒哈貝罕生阿彼雅,阿彼雅生阿撒,
8 Asa alimzaa Yehoshafati, Yehoshafati alimzaa Yoramu, Yoramu alimzaa Uzia,
阿撒生約沙法特,約沙法特生約蘭,約蘭生烏齊雅,
9 Uzia alimzaa Yothamu, Yothamu alimzaa Ahazi, Ahazi alimzaa Hezekia,
烏齊雅生約當,約當生阿哈次,阿哈次生希則克雅,
10 Hezekia alimzaa Manase, Manase alimzaa Amoni, Amoni alimzaa Yosia,
希則克雅生默納舍,默納舍生阿孟,阿孟生約史雅,
11 Yosia alimzaa Yekonia na ndugu zake. Huo ulikuwa wakati Wayahudi walipopelekwa uhamishoni Babuloni.
約史雅在巴比倫流徙期間生耶苛尼雅和他的兄弟們,
12 Baada ya Wayahudi kupelekwa uhamishomi Babuloni: Yekonia alimzaa Shealtieli, Shealtieli alimzaa Zerobabeli,
流徙巴比倫以後,耶苛尼雅生沙耳提耳,沙耳提耳生則魯巴比耳,
13 Zerobabeli alimzaa Abiudi, Abiudi alimzaa Eliakimu, Eliakimu alimzaa Azori,
則魯巴比耳生阿彼鳥得,阿彼鳥得生厄里雅金,厄里雅金生阿左耳。
14 Azori alimzaa Zadoki, Zadoki alimzaa Akimu, Akimu alimzaa Eliudi,
阿左耳生匝多克,匝多克生阿歆,阿歆生厄里烏得,
15 Eliudi alimzaa Eleazeri, Eleazeri alimzaa Mathani, Mathani alimzaa Yakobo,
厄里烏得生厄肋阿匝爾,厄肋阿匝爾生瑪堂,瑪堂生雅各伯,
16 Yakobo alimzaa Yosefu, aliyekuwa mume wake Maria, mama yake Yesu, aitwaye Kristo.
雅各伯生若瑟、瑪利亞的丈夫,瑪利亞生耶穌,衪稱為基督。
17 Basi, kulikuwa na vizazi kumi na vinne tangu Abrahamu mpaka Daudi, vizazi kumi na vinne tangu Daudi mpaka Wayahudi walipochukuliwa mateka Babuloni, na vizazi kumi na vinne tangu kuchukuliwa mateka mpaka wakati wa Kristo.
所以從亞巴郎到達味共十四代,從達味到流徙巴比倫共十四代,從流徙巴比倫到基督共十四代。
18 Basi, hivi ndivyo Yesu Kristo alivyozaliwa: Maria, mama yake, alikuwa ameposwa na Yosefu. Lakini kabla hawajakaa pamoja kama mume na mke, alionekana kuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
耶穌基督的誕生是這樣的:衪的母親許配於若瑟後,在同居前,她因聖神有孕的事已顯示出來。
19 Yosefu, mumewe, kwa vile alikuwa mwadilifu, hakutaka kumwaibisha hadharani; hivyo alikusudia kumwacha kwa siri.
她的丈夫若瑟,因是義人,不願公開羞她,有意暗暗地休退她。
20 Alipokuwa bado anawaza jambo hilo, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akamwambia, “Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumchukua Maria awe mke wako, maana amekuwa mja mzito kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
當他在思慮這事時,看,在夢人上主的天使顯現給他說:「達味之子若瑟,不要怕娶你的妻子瑪利亞,因為那在她內受生的,是出於聖神。
21 Atajifungua mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yesu, kwa kuwa yeye atawaokoa watu wake kutoka katika dhambi zao.”
她要生一個兒子,妳要給衪起名叫耶穌,因為衪要把自己的民族,由他們的罪惡中拯救出來。」
22 Basi, haya yote yalitukia ili litimie lile neno Bwana alilosema kwa njia ya nabii:
這一切事的發生,是為應驗上主藉先知所說的話:
23 “Bikira atachukua mimba, atamzaa mtoto wa kiume, naye ataitwa Emanueli” (maana yake, “Mungu yu pamoja nasi”).
「看,一位貞女,將懷孕生子,人將稱衪的名字為厄瑪奴耳,意思是:天主與我們同在。
24 Hivyo, Yosefu alipoamka usingizini alifanya kama malaika huyo alivyomwambia, akamchukua mke wake nyumbani.
若瑟從睡夢中醒來,就照上主的天使所囑咐的辦了,娶了他的妻子;
25 Lakini hakumjua kamwe kimwili hata Maria alipojifungua mtoto wa kiume. Naye Yosefu akampa jina Yesu.
若瑟雖然沒認識她,她就生了一個兒子,給衪起名叫耶穌。