< Luka 3 >

1 Mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Kaisari Tiberio, Pontio Pilato alikuwa anatawala mkoa wa Yudea. Herode alikuwa mkuu wa mkoa wa Galilaya, na Filipo, ndugu yake, alikuwa mkuu wa mikoa ya Iturea na Trakoniti. Lusania alikuwa mkuu wa mkoa wa Abilene,
And in the fifteenth year of the government of Tiberius Caesar—Pontius Pilate being governor of Judea, and Herod tetrarch of Galilee, and his brother Philip, tetrarch of Ituraea and of the region of Trachonitis, and Lysanias tetrarch of Abilene,
2 na Anasi na Kayafa walikuwa makuhani wakuu mjini Yerusalem. Wakati huo ndipo neno la Mungu lilipomjia Yohane, mwana wa Zakariya, kule jangwani.
[and] Annas and Caiaphas being chief priests—there came a word of God to John the son of Zacharias, in the wilderness,
3 Basi, Yohane akaenda katika sehemu zote zilizopakana na mto Yordani, akihubiri watu watubu na kubatizwa ili Mungu awaondolee dhambi.
and he came to all the region around the Jordan, proclaiming an immersion of conversion for forgiveness of sins,
4 Ndivyo ilivyoandikwa katika kitabu cha nabii Isaya: “Sauti ya mtu imesikika jangwani: Mtayarishieni Bwana njia yake; nyosheni mapito yake.
as it has been written in the scroll of the words of Isaiah the prophet: “A voice of one crying in the wilderness: Prepare the way of the LORD, Make His paths straight;
5 Kila bonde litafukiwa, kila mlima na kilima vitasawazishwa; palipopindika patanyooshwa, njia mbaya zitatengenezwa.
Every valley will be filled, And every mountain and hill will be made low, And the crooked will become straightness, And the rough become smooth ways;
6 Na, watu wote watauona wokovu utokao kwa Mungu.”
And all flesh will see the salvation of God.”
7 Basi, Yohane akawa anawaambia watu wengi waliofika ili awabatize: “Enyi kizazi cha nyoka! Ni nani aliyewadokezea kwamba mngeweza kuiepuka ghadhabu inayokuja?
Then he said to the multitudes coming forth to be immersed by him, “Brood of vipers! Who prompted you to flee from the coming wrath?
8 Basi, onyesheni kwa matendo kwamba mmetubu. Msianze sasa kusema: Sisi ni watoto wa Abrahamu. Nawaambieni hakika, Mungu anaweza kuyageuza mawe haya yawe watoto wa Abrahamu!
Make, therefore, fruits worthy of conversion, and do not begin to say within yourselves, We have a father—Abraham; for I say to you that God is able to raise children to Abraham out of these stones;
9 Lakini, sasa hivi shoka limewekwa tayari kukata mizizi ya miti. Kila mti usiozaa matunda mazuri utakatwa na kutupwa motoni.”
and also the axe is already laid to the root of the trees, every tree, therefore, not making good fruit is cut down, and it is cast into fire.”
10 Umati wa watu ukamwuliza, “Tufanye nini basi?”
And the multitudes were questioning him, saying, “What, then, will we do?”
11 Akawajibu, “Aliye na nguo mbili amgawie yule asiye na nguo; aliye na chakula afanye vivyo hivyo.”
And he answering says to them, “He having two coats, let him impart to him having none; and he having food, let him do in like manner.”
12 Nao watoza ushuru wakaja pia ili wabatizwe, wakamwuliza, “Mwalimu, tufanye nini?”
And there also came tax collectors to be immersed, and they said to him, “Teacher, what will we do?”
13 Naye akawaambia, “Msitoze ushuru zaidi ya kima kilichowekwa.”
And he said to them, “Exact no more than that directed you.”
14 Nao askari wakamwuliza, “Na sisi tufanye nini?” Naye akawajibu, “Msichukue vitu vya mtu yeyote kwa nguvu wala kumshtaki yeyote kwa uongo. Toshekeni na mishahara yenu.”
And also questioning him were those warring, saying, “And we, what will we do?” And he said to them, “Do violence to no one, nor accuse falsely, and be content with your wages.”
15 Wote walikuwa wanatazamia kitu fulani; basi, wakaanza kujiuliza mioyoni mwao kuhusu Yohane: kuwa labda yeye ndiye Kristo.
And the people are looking forward, and all are reasoning in their hearts concerning John, whether or not he may be the Christ;
16 Hapo Yohane akawaambia wote, “Mimi ninawabatiza kwa maji, lakini anakuja mwenye uwezo zaidi kuliko mimi ambaye sistahili hata kumfungulia kamba za viatu vyake. Yeye atawabatizeni kwa Roho Mtakatifu na kwa moto.
John answered, saying to all, “I indeed immerse you in water, but He comes who is mightier than I, of whom I am not worthy to loose the strap of His sandals—He will immerse you in the Holy Spirit and fire;
17 Yeye ni kama mtu anayeshika mikononi mwake chombo cha kupuria nafaka, aipure nafaka yake, akusanye ngano ghalani mwake, na makapi ayachome kwa moto usiozimika.”
whose winnowing shovel [is] in His hand, and He will thoroughly cleanse His floor, and will gather the wheat into His storehouse, and He will burn the chaff with unquenchable fire.”
18 Hivyo, pamoja na mawaidha mengine mengi, Yohane aliwahimiza watu akiwahubiria Habari Njema.
And therefore, indeed, with many other things, exhorting, he was proclaiming good news to the people,
19 Lakini Yohane alimgombeza Herode, mkuu wa mkoa, kwa sababu alikuwa amemchukua Herodia, mke wa ndugu yake, na kumfanya mke wake; na pia kwa ajili ya mabaya yote aliyokuwa amefanya.
and Herod the tetrarch, being reproved by him concerning Herodias, the wife of his brother Philip, and concerning all the evils that Herod did,
20 Kisha Herode akazidisha ubaya wake kwa kumtia Yohane gerezani.
added also this to all, that he shut up John in the prison.
21 Watu wote walipokuwa wamekwisha batizwa, Yesu naye alibatizwa. Na alipokuwa akisali, mbingu zilifunguka,
And it came to pass, in all the people being immersed, Jesus also being immersed, and praying, Heaven was opened,
22 na Roho Mtakatifu akamshukia akiwa na umbo kama la njiwa. Sauti ikasikika kutoka mbinguni: “Wewe ndiwe Mwanangu mpendwa, nimependezwa nawe.”
and the Holy Spirit came down in a bodily appearance, as if a dove, on Him, and a voice came out of Heaven, saying, “You are My Son, the Beloved, in You I delighted.”
23 Yesu alipoanza kazi yake hadharani, alikuwa na umri upatao miaka thelathini, na watu walidhani yeye ni mwana wa Yosefu, mwana wa Heli.
And Jesus Himself was beginning to be about thirty years of age, being, as was supposed, Son of Joseph,
24 Heli alikuwa mwana wa Mathati, mwana wa Lawi, mwana wa Melki, mwana wa Yanai, mwana wa Yosefu,
the [son] of Eli, the [son] of Matthat, the [son] of Levi, the [son] of Melchi, the [son] of Janna, the [son] of Joseph,
25 mwana wa Matathia, mwana wa Amosi, mwana wa Nahumu, mwana wa Hesli, mwana wa Nagai,
the [son] of Mattathias, the [son] of Amos, the [son] of Nahum, the [son] of Esli,
26 mwana wa Maathi, mwana wa Matathia, mwana wa Shemeni, mwana wa Yoseki, mwana wa Yuda,
the [son] of Naggai, the [son] of Maath, the [son] of Mattathias, the [son] of Semei, the [son] of Joseph, the [son] of Judah,
27 mwana wa Yohanani, mwana wa Resa, mwana wa Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, mwana wa Neri,
the [son] of Joanna, the [son] of Rhesa, the [son] of Zerubbabel, the [son] of Shealtiel,
28 mwana wa Melki, mwana wa Adi, mwana wa Kosamu, mwana wa Elmadamu, mwana wa Eri,
the [son] of Neri, the [son] of Melchi, the [son] of Addi, the [son] of Cosam, the [son] of Elmodam, the [son] of Er,
29 mwana wa Yoshua, mwana wa Eliezeri, mwana wa Yorimu, mwana wa Mathati, mwana wa Lawi,
the [son] of Jose, the [son] of Eliezer, the [son] of Jorim, the [son] of Matthat,
30 mwana wa Simeoni, mwana wa Yuda, mwana wa Yosefu, mwana wa Yonamu, mwana wa Eliakimu,
the [son] of Levi, the [son] of Simeon, the [son] of Judah, the [son] of Joseph, the [son] of Jonan, the [son] of Eliakim,
31 mwana wa Melea, mwana wa Mena, mwana wa Matatha, mwana wa Nathani, mwana wa Daudi,
the [son] of Melea, the [son] of Mainan, the [son] of Mattatha, the [son] of Nathan,
32 mwana wa Yese, mwana wa Obedi, mwana wa Boazi, mwana wa Salmoni, mwana wa Nashoni,
the [son] of David, the [son] of Jesse, the [son] of Obed, the [son] of Boaz, the [son] of Salmon, the [son] of Nahshon,
33 mwana wa Aminadabu, mwana wa Admini, mwana wa Arni, mwana wa Hesroni, mwana wa Feresi, mwana wa Yuda,
the [son] of Amminadab, the [son] of Aram, the [son] of Esrom, the [son] of Perez,
34 mwana wa Yakobo, mwana wa Isaka, mwana wa Abrahamu, mwana wa Tera, mwana wa Nahori,
the [son] of Judah, the [son] of Jacob, the [son] of Isaac, the [son] of Abraham, the [son] of Terah, the [son] of Nahor,
35 mwana wa Serugi, mwana wa Reu, mwana wa Pelegi, mwana wa Eberi, mwana wa Sala,
the [son] of Serug, the [son] of Reu, the [son] of Peleg, the [son] of Eber,
36 mwana wa Kainani, mwana wa Arfaksadi, mwana wa Shemu, mwana wa Noa, mwana wa Lameki,
the [son] of Salah, the [son] of Cainan, the [son] of Arphaxad, the [son] of Shem, the [son] of Noah, the [son] of Lamech,
37 mwana wa Mathusala, mwana wa Henoki, mwana wa Yaredi, mwana wa Mahalaleli, mwana wa Kenani,
the [son] of Methuselah, the [son] of Enoch, the [son] of Jared, the [son] of Mahalaleel,
38 mwana wa Enosi, mwana wa Sethi, mwana wa Adamu, aliyekuwa wa Mungu.
the [son] of Cainan, the [son] of Enos, the [son] of Seth, the [son] of Adam, the [son] of God.

< Luka 3 >