< Luka 2 >
1 Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote chini ya utawala wake wajiandikishe.
And it came to pass in those days, there went forth a decree from Caesar Augustus that all the world be registered—
2 Kuandikishwa huku kulikuwa mara ya kwanza, wakati Kirenio alipokuwa mkuu wa mkoa wa Siria.
this census first came to pass when Quirinius was governor of Syria—
3 Basi, wote waliohusika walikwenda kujiandikisha, kila mtu katika mji wake.
and all were going to be registered, each to his proper city,
4 Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya. Kwa kuwa alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yuda alikozaliwa Mfalme Daudi.
and Joseph also went up from Galilee, out of the city of Nazareth, to Judea, to the city of David, that is called Beth-Lehem, because of his being of the house and family of David,
5 Alikwenda kujiandikisha pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mja mzito.
to register himself with Mary his betrothed wife, being with Child.
6 Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia,
And it came to pass, in their being there, the days were fulfilled for her bringing forth,
7 akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni.
and she brought forth her Son—the firstborn, and wrapped Him up, and laid Him down in the manger, because there was not a place for them in the guest-chamber.
8 Katika sehemu hizo, walikuwako wachungaji wakikesha usiku mbugani kulinda mifugo yao.
And there were shepherds in the same region, lodging in the field and keeping the night-watches over their flock,
9 Malaika wa Bwana akawatokea ghafla, na utukufu wa Bwana ukawaangazia pande zote. Wakaogopa sana.
and behold, a messenger of the LORD stood over them, and the glory of the LORD shone around them, and they feared [with] a great fear.
10 Malaika akawaambia, “Msiogope! Nimewaleteeni habari njema ya furaha kuu kwa watu wote.
And the messenger said to them, “Do not fear, for behold, I bring you good news of great joy that will be to all the people,
11 Kwa maana, leo hii katika mji wa Daudi, amezaliwa Mwokozi kwa ajili yenu, ndiye Kristo Bwana.
because today in the city of David a Savior was born to you, who is Christ the LORD!
12 Na hiki kitakuwa kitambulisho kwenu: mtamkuta mtoto mchanga amevikwa nguo za kitoto, amelazwa horini.”
And this [is] the sign to you: you will find a Baby wrapped up, lying in the manger.”
13 Mara kundi kubwa la jeshi la mbinguni likajiunga na huyo malaika, wakamsifu Mungu wakisema:
And suddenly there came with the messenger a multitude of the heavenly host, praising God, and saying,
14 “Utukufu kwa Mungu juu mbinguni, na amani duniani kwa watu aliopendezwa nao!”
“Glory in the highest to God, and on earth peace, among men—good will!”
15 Baada ya hao malaika kuondoka na kurudi mbinguni, wachungaji wakaambiana: “Twendeni moja kwa moja mpaka Bethlehemu tukalione tukio hili Bwana alilotujulisha.”
And it came to pass, when the messengers were gone away from them to the heavens, that the men, the shepherds, said to one another, “We may indeed go over to Beth-Lehem and see this thing that has come to pass, that the LORD made known to us!”
16 Basi, wakaenda mbio, wakamkuta Maria na Yosefu na yule mtoto mchanga amelazwa horini.
And they came, having hurried, and found both Mary, and Joseph, and the Baby lying in the manger,
17 Hao wachungaji walipomwona mtoto huyo wakawajulisha wote habari waliyokuwa wamesikia juu yake.
and having seen, they made known abroad concerning the saying spoken to them concerning the Child.
18 Wote waliosikia hayo walishangaa juu ya habari walizoambiwa na wachungaji.
And all who heard [it] wondered concerning the things spoken to them by the shepherds;
19 Lakini Maria aliyaweka na kuyatafakari mambo hayo yote moyoni mwake.
and Mary was preserving all these things, pondering [them] in her heart;
20 Wale wachungaji walirudi makwao huku wakimtukuza na kumsifu Mungu kwa yote waliyokuwa wamesikia na kuona; yote yalikuwa kama walivyokuwa wameambiwa.
and the shepherds turned back, glorifying and praising God for all those things they heard and saw, as it was spoken to them.
21 Siku nane baadaye, wakati wa kumtahiri mtoto ulipofika, walimpa jina Yesu, jina ambalo alikuwa amepewa na malaika kabla hajachukuliwa mimba.
And when eight days were fulfilled to circumcise the Child, then was His Name called Jesus, having been so called by the messenger before His being conceived in the womb.
22 Siku zilipotimia za Yosefu na Maria kutakaswa kama walivyotakiwa na Sheria ya Mose, wazazi hao walimchukua mtoto, wakaenda naye Yerusalemu ili wamweke mbele ya Bwana.
And when the days of their purification were fulfilled, according to the Law of Moses, they brought Him up to Jerusalem, to present to the LORD,
23 Katika Sheria ya Bwana imeandikwa: “Kila mzaliwa wa kwanza wa kiume atawekwa wakfu kwa Bwana.”
as it has been written in the Law of the LORD: “Every male opening a womb will be called holy to the LORD,”
24 Pia walikwenda ili watoe sadaka: hua wawili au makinda wawili ya njiwa, kama ilivyotakiwa katika Sheria ya Bwana.
and to give a sacrifice, according to that said in the Law of the LORD: “A pair of turtle-doves, or two young pigeons.”
25 Wakati huo huko Yerusalemu kulikuwa na mtu mmoja, mwema na mcha Mungu, jina lake Simeoni. Yeye alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa Israeli. Roho Mtakatifu alikuwa pamoja naye.
And behold, there was a man in Jerusalem whose name [is] Simeon, and this man is righteous and devout, looking for the comforting of Israel, and the Holy Spirit was on him,
26 Roho Mtakatifu alikuwa amemhakikishia kwamba hatakufa kabla ya kumwona Masiha wa Bwana.
and it has been divinely told him by the Holy Spirit—not to see death before he may see the Christ of the LORD.
27 Basi, akiongozwa na Roho Mtakatifu, Simeoni aliingia Hekaluni; na wazazi wa Yesu walipomleta Hekaluni mtoto wao ili wamfanyie kama ilivyotakiwa na Sheria,
And he came in the Spirit into the temple, and in the parents bringing in the child Jesus, for their doing according to the custom of the Law regarding Him,
28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu na kusema:
then he took Him in his arms, and blessed God, and he said,
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako, waweza kumruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
“Now You send Your servant away, O LORD, according to Your word, in peace,
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu utokao kwako,
because my eyes saw Your salvation,
31 ambao umeutayarisha mbele ya watu wote:
which You prepared before the face of all the peoples,
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa, na utukufu kwa watu wako Israeli.”
a light to the uncovering of nations, and the glory of Your people Israel.”
33 Baba na mama yake Yesu walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
And Joseph and His mother were wondering at the things spoken concerning Him,
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;
and Simeon blessed them and said to His mother Mary, “Behold, this [One] is set for the falling and rising again of many in Israel, and for a sign spoken against—
35 na hivyo mawazo ya watu wengi yataonekana wazi. Nawe mwenyewe, uchungu ulio kama upanga mkali utauchoma moyo wako.”
(and also a sword will pass through your own soul)—that the reasonings of many hearts may be revealed.”
36 Palikuwa na nabii mmoja mwanamke, mzee sana, jina lake Ana, binti Fanueli, wa kabila la Asheri. Alikuwa ameishi na mumewe kwa miaka saba tangu alipoolewa.
And there was Anna, a prophetess, daughter of Phanuel, of the tribe of Asher, she was much advanced in days, having lived with a husband seven years from her virginity,
37 Halafu alibaki mjane hadi wakati huo akiwa mzee wa miaka themanini na minne. Wakati huo wote alikaa Hekaluni akifunga na kusali usiku na mchana.
and she [is] a widow of about eighty-four years, who did not depart from the temple, serving with fasts and supplications, night and day,
38 Saa hiyohiyo alijitokeza mbele, akamshukuru Mungu, na akaeleza habari za huyo mtoto kwa watu wote waliokuwa wanatazamia ukombozi wa Yerusalemu.
and she, at that hour, having come in, was confessing, likewise, to the LORD, and was speaking concerning Him to all those looking for redemption in Jerusalem.
39 Hao wazazi walipokwisha fanya yote yaliyoamriwa na Sheria ya Bwana, walirudi makwao Nazareti, mkoani Galilaya.
And when they completed all things according to the Law of the LORD, they turned back to Galilee, to their city of Nazareth;
40 Mtoto akakua, akazidi kupata nguvu, akajaa hekima, na neema ya Mungu ilikuwa pamoja naye.
and the Child grew and was strengthened in spirit, being filled with wisdom, and the grace of God was on Him.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka.
And His parents were going yearly to Jerusalem, at the Celebration of the Passover,
42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi.
and when He became twelve years old, they having gone up to Jerusalem according to the custom of the celebration,
43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari.
and having finished the days, in their returning the child Jesus remained behind in Jerusalem, and Joseph and His mother did not know,
44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki.
and having supposed Him to be in the company, they went a day’s journey, and were seeking Him among the relatives and among the acquaintances,
45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta.
and having not found Him, they turned back to Jerusalem seeking Him.
46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali.
And it came to pass, after three days they found Him in the temple, sitting in the midst of the teachers, both hearing them and questioning them,
47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima.
and all those hearing Him were astonished at His understanding and answers.
48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.”
And having seen Him, they were amazed, and His mother said to Him, “Child, why did You do this to us? Behold, Your father and I, sorrowing, were seeking You.”
49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”
And He said to them, “Why [is it] that you were seeking Me? Did you not know that it is necessary for Me to be in the things of My Father?”
50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia.
And they did not understand the saying that He spoke to them,
51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake.
and He went down with them, and came to Nazareth, and He was subject to them, and His mother was keeping all these sayings in her heart,
52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu.
and Jesus was advancing in wisdom, and in stature, and in favor with God and men.