< Luka 21 >

1 Yesu alitazama kwa makini, akawaona matajiri walivyokuwa wanatia sadaka zao katika hazina ya Hekalu,
uYesu akalila akavagha avakinhaata vamofu valyale vivika amatekelo ghave muvutile
2 akamwona pia mama mmoja mjane akitumbukiza humo sarafu mbili ndogo.
akamwagha unfwile jumonga nkotofu ivika isenti sake ivili. pe
3 Basi, akasema, “Nawaambieni kweli, mama huyu mjane ametia zaidi katika hazina kuliko wote.
akati,”kyang'haani nikuvavula unfwile uju unkotofu ivikile indalama nyinga kukila avange voooni.
4 Kwa maana, wengine wote wametoa sadaka zao kutokana na ziada ya mali zao, lakini huyu mama, ingawa ni maskini, ametoa kila kitu alichohitaji kwa kuishi.”
ava vooni vahumisie ilitekelo ili kuhuma mufinga fino valinafyo. neke unfwile uju mu vukotofu vwake ahumisie indalamasooni sino avele naso vwimila uvwumi vwake”
5 Baadhi ya wanafunzi walikuwa wanazungumza juu ya Hekalu, jinsi lilivyopambwa kwa mawe ya thamani, pamoja na sadaka zilizotolewa kwa Mungu. Yesu akasema,
ye avange valyale vijova isa nyumba inyimike ja kufunyila, ndavule jilyavikilue na mavue amanono na matekelo, akati,
6 “Haya yote mnayoyaona—zitakuja siku ambapo hakuna hata jiwe moja litakalosalia juu ya lingine; kila kitu kitaharibiwa.”
mu mhola isa mbombo sino mukusagha, ifighono fikwisa fino nakwekuliva nilivue limo lino lililekua nkyanya ja livue ilinge lino nalilighua.
7 Basi, wakamwuliza, “Mwalimu, mambo hayo yatatokea lini? Na ni ishara gani zitakazoonyesha kwamba karibu mambo hayo yatokee?”
pe vakamposia vakati, Mbulanisi isi sooni silihumila lighi? kwe kiliku kino kiliva kye kivalilo kuuti agha ghalipipi kuhumila?
8 Yesu akawajibu, “Jihadharini, msije mkadanganyika. Maana wengi watatokea na kulitumia jina langu wakisema: Mimi ndiye, na, Wakati ule umekaribia. Lakini ninyi msiwafuate!
uYesu akamwamula, “muvisaghe maaso kuuti namungasyanguaghe. ulwakuva vingi vikwisa ku litavua lyango viti,”une nene, nu nsiki ghulipipi. namungavavingililaghe.
9 Basi, mtakaposikia habari za vita na misukosuko, msitishike; maana ni lazima hayo yatokee kwanza, lakini mwisho wa yote, bado.”
mungapulike ivuluguvulugu namungoghwopaghe, ulwakuva isi sooni sinoghile sihumile taasi. neke uvusililo navulihimila ng'hani ng'hani”
10 Halafu akaendelea kusema: “Taifa moja litapigana na taifa lingine, na ufalme mmoja utapigana na ufalme mwingine.
pe pano akavavula,” iisi jilikwima na kutovana ni jinge, uvutwa ku vutwa uvunge.
11 Kila mahali kutakuwa na mitetemeko mikubwa ya ardhi, kutakuwa na njaa na tauni. Kutakuwa na vituko vya kutisha na ishara kubwa angani.
kuliva ni finsenyena ifikome, injala ni nhamu isa kwambukila siliva papinga. kwe kuliva ni finu fya kwoghofia ni fivalilo fya kwoghofia kuhuma kukyanya.
12 Lakini kabla ya kutokea hayo yote, watawatieni nguvuni, watawatesa na kuwapelekeni katika masunagogi na kuwatia gerezani; mtapelekwa mbele ya wafalme na watawala kwa ajili ya jina langu.
neke isio sooni ye sikyale kuhumila, tiko avaanhu vilikuvakoola umue na kukuvapumusia. vilikuvawala kukuahigha mu nyumba isa kufunyila, na kukuvadindila mu ndinde. kange mulitwalua ku vatwa na ku vanya vutavulilua kuuti muhighue ulwakuva umue muli vavvulanisivua vango.
13 Hii itawapeni fursa ya kushuhudia Habari Njema.
neke kulyumue aghuo ghuva ghwe nsiki ghwa kwoleka ulwitiko lwinu.
14 Muwe na msimamo huu mioyoni mwenu: hakuna kufikiria kabla ya wakati juu ya jinsi mtakavyojitetea,
pe lino mwamulaghe mu moojo ghinu ku ling'ania avimilisi viinu ye lukyale.
15 kwa sababu mimi mwenyewe nitawapeni ufasaha wa maneno na hekima, hivyo kwamba zenu hawataweza kustahimili wala kupinga.
ulwakuva nikuvapela amasio agha vukoola vuno avalugu viinu voni vikunuagha kusigha na kukujikana.
16 Wazazi wenu, ndugu, jamaa na rafiki zenu watawasaliti ninyi; na baadhi yenu mtauawa.
neke mulikanwa na vapafi vinu, avanyalukolo vinu, avapipi vinu na vamanyani vinu, kange vilikuvabuda vamonga mu lyumue,
17 Watu wote watawachukieni kwa sababu ya jina langu.
vilikunkalalila umuunu ghweni ku litavua lyango.
18 Lakini, hata unywele mmoja wa vichwa vyenu hautapotea.
neke nakwelule nambe ulunyele lumo lwa matu ghinu luno lulisova.
19 Kwa uvumilivu wenu, mtayaokoa maisha yenu.
ku lugudo mukusisosia inumbula sinu.
20 “Mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, ndipo mtambue ya kwamba wakati umefika ambapo mji huo utaharibiwa.
kyale muvoona ilikaaja lya Yelusalemu lisyungutilue navalua lilugu pe mukagulaghe kuuti unsiki ughwa kutipulua ghuli pipi.
21 Hapo walioko Yudea wakimbilie milimani; wale walio mjini watoke; na wale walio mashambani wasirudi mjini.
apuo vano vali ku Yudea vakimbililaghe ku fidunda, na vala vano vali pakate pa mpulo vavukaghe, kange namungavalekaghe vano vali kufikaaja kukwingila.
22 Kwa maana siku hizo ni siku za adhabu, ili yote yaliyoandikwa yatimie.
ulwakuva ifi fye fighono fya kuhombekesia, neke kuuti ghooni ghano ghalembilue ghiise kuvombeka.
23 Ole wao waja wazito na wanyonyeshao siku hizo! Kwa maana kutakuwa na dhiki kubwa katika nchi, na hasira ya Mungu itawajia watu hawa.
iga ku vala vano vali nuvukunue na vala vano vikwong'esia ku fighono ifio! ulwakuva kuliiva nulupumuko lukome mu iisi, ni ng'halasi ku vaaanhu ava.
24 Wengine watauawa kwa upanga, wengine watachukuliwa mateka katika nchi zote; na mji wa Yerusalemu utakanyagwa na watu wa mataifa mengine, hadi nyakati zao zitakapotimia.
avaanhu avange vilibudua ni bambaavange vilitwalua ku vukamiku iisi isinge, ni Yelusalemu jilikanyua na vaanhu va iisi kuhanga unsiki ghwa vaanhu va iisi pano ghuuva ghufikile.
25 “Kutakuwa na ishara katika jua na mwezi na nyota. Mataifa duniani yatakuwa na dhiki kwa sababu ya wasiwasi kutokana na mshindo wa mawimbi ya bahari.
fili vineka ifivalilo ku lijuva, umwesi ni nhondue, neke pa iisi apa inyanja siliva na mavingo amavaha amanya mughindi, uluo lulipelela avaanhu ava fisina fyonikuuva nulupumuko nu ludwesi.
26 Watu watazirai kwa sababu ya uoga, wakitazamia mambo yatakayoupata ulimwengu; kwa maana nguvu za mbingu zitatikiswa.
isi sooni siliva sikwisa mu iisi, avaanhu ghulifua umwoojovwimila kukwoghopa kyongo. vilisaghagha kuuti lukwisa ulutalamu ulukome, ulwakuva ifinu ifya kukyanya filisukanisivua,
27 Halafu, watamwona Mwana wa Mtu akija katika wingu, mwenye nguvu na utukufu mwingi.
pepano vilikumwagha umwana ghwa muunhu ikwisa kuhuma mumafunde ku ngufu nu vwimike uvuvaha.
28 Wakati mambo hayo yatakapoanza kutukia, simameni na kuinua vichwa vyenu juu, kwa maana ukombozi wenu umekaribia.”
neke isio sooni silava sitengula kuhumila, mwimaghe, inulagha amatu ghinu, ulwakuva uvupoki vwinu vuvelelile pavupipi.
29 Kisha akawaambia mfano: “Angalieni mtini na miti mingine yote.
uYesu akavavula ku kihwanikisio akati, lolagha umpiki ghwa tini na mapiki ghoni.
30 Mnapoona kwamba imeanza kuchipua majani, mwatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
pano muvona amapiki ghatengwile kulemba, mukujilolela jumue na kukagula kuuti amasiki gha lufuke ghalipipi.
31 Vivyo hivyo, mtakapoona mambo hayo yanatendeka, mtatambua kwamba Ufalme wa Mungu umekaribia.
vule vule pano muvona agha ghihumila umue kagulagha kuuti, uvutwa vwa Nguluve vulipipi.
32 Nawaambieni hakika, kizazi hiki cha sasa hakitapita kabla ya hayo yote kutendeka.
kyang'haani nikuvavula, ikisina iki nakilikila, kuhanga isi sooni sihumile.
33 Mbingu na dunia vitapita, lakini maneno yangu hayatapita.
uvulanga ni iisi silikila, neke amasio ghango looli naghilikila.
34 “Muwe macho, mioyo yenu isije ikalemewa na anasa, ulevi na shughuli za maisha haya. La sivyo, Siku ile itawajieni ghafla.
neke mujilolelelaghe jumue, neke kuuti, amoojo ghinu naghangalemuaghe nu vuhojofu, uvughasi, nuvukaming'anilua vwa iisi iji. ulwakuva ikighono ikio kilavisila mu lwa ng'enyemukila hwene lutegho.
35 Kwa maana itawajia kama mtego, wote wanaoishi duniani pote.
ulwakuva jiiva kwa muunhu ghweni juno ikukala pa maaso gha iisi jooni.
36 Muwe waangalifu basi, na salini daima ili muweze kupata nguvu ya kupita salama katika mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Mtu.”
lino muvisaghe maaso unsiki ghwoni, mun'sumaghe uNguluve kuuti muva lukangafu lwa kukwilana kukughaseghuka agha ghoni ghano kyale ghihumila, na kukwima pavulongolo pa mwana ghwa Muunhu”.
37 Wakati wa mchana, siku hizo, Yesu alikuwa akifundisha watu Hekaluni; lakini usiku alikuwa akienda katika mlima wa Mizeituni na kukaa huko.
mu fighono ifio pamwisi, uYesu alyale ivulanisia avaanhu mu luviika ulwa nyumba inyimike ja kufunyila. pakilo akalutagha kughona ku kidunda ikya Miseituni.
38 Watu wote walikuwa wanakwenda Hekaluni asubuhi na mapema, wapate kumsikiliza.
neke jaatu avaanhu voni vakasisimukagha lulwakilo na kuluta mu nyumba inyimike ja kufunyila kuuti vampulikisie.

< Luka 21 >