< Luka 20 >
1 Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
And it came to pass, on one of those days, as He is teaching the people in the temple, and proclaiming good news, the chief priests and the scribes, with the elders, came on [Him],
2 wakasema, “Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?”
and spoke to Him, saying, “Tell us by what authority You do these things? Or who is he that gave to You this authority?”
3 Yesu akawaambia, “Na mimi nitawaulizeni swali:
And He answering said to them, “I will question you—I also—one thing, and tell Me:
4 mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?”
the immersion of John, was it from Heaven, or from men?”
5 Lakini wao wakajadiliana hivi: “Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: Mbona hamkumsadiki?
And they reasoned with themselves, saying, “If we may say, From Heaven, He will say, Why, then, did you not believe him?
6 Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii.”
And if we may say, From men, all the people will stone us, for they are having been persuaded John to be a prophet.”
7 Basi, wakamwambia, “Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi.”
And they answered that they did not know from where [it was],
8 Yesu akawaambia, “Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani.”
and Jesus said to them, “Neither do I say to you by what authority I do these things.”
9 Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: “Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
And He began to speak to the people this allegory: “A certain man planted a vineyard, and gave it out to farmers, and went abroad for a long time,
10 Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
and at the season he sent a servant to the farmers, that they may give to him from the fruit of the vineyard, but the farmers having beat him, sent [him] away empty.
11 Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
And he added to send another servant, and they also having beaten and dishonored that one, sent [him] away empty;
12 Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
and he added to send a third, and this one also, having wounded, they cast out.
13 Yule mwenye shamba akafikiri: Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.
And the owner of the vineyard said, What will I do? I will send my son, the beloved, perhaps having seen this one, they will respect [him];
14 Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.
and having seen him, the farmers reasoned among themselves, saying, This is the heir; come, we may kill him, that the inheritance may become ours;
15 Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua.” Yesu akauliza, “Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
and having cast him outside of the vineyard, they killed [him]; what, then, will the owner of the vineyard do to them?
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu.” Watu waliposikia maneno hayo, walisema: “Hasha! Yasitukie hata kidogo!”
He will come, and destroy these farmers, and will give the vineyard to others.” And having heard, they said, “Let it not be!”
17 Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, “Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!
And He, having looked on them, said, “What, then, is this that has been written: A stone that the builders rejected—this became head of a corner?
18 Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa.”
Everyone who has fallen on that stone will be broken, and on whom it may fall, it will crush him to pieces.”
19 Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
And the chief priests and the scribes sought to lay hands on Him in that hour, and they feared the people, for they knew that He spoke this allegory against them.
20 Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
And having watched [Him], they sent forth ones lying in wait, feigning themselves to be righteous, that they might take hold of His word, to deliver Him up to the rule and to the authority of the governor,
21 Hao wapelelezi wakamwambia, “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
and they questioned Him, saying, “Teacher, we have known that You say and teach correctly, and do not receive a person, but in truth teach the way of God.
22 Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!”
Is it lawful to us to give tribute to Caesar or not?”
23 Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
And He, having perceived their craftiness, said to them, “Why do you tempt Me?
24 “Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?”
Show Me a denarius; of whom does it have an image and inscription?” And they answering said, “Of Caesar”:
25 Nao wakamjibu, “Ni vya Kaisari.” Yesu akawaambia, “Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu.”
and He said to them, “Give back, therefore, the things of Caesar to Caesar, and the things of God to God”;
26 Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
and they were not able to take hold on His saying before the people, and having wondered at His answer, they were silent.
27 Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
And certain of the Sadducees, who are denying that there is a resurrection, having come near, questioned Him,
28 “Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
saying, “Teacher, Moses wrote to us if anyone’s brother may die, having a wife, and he may die childless—that his brother may take the wife, and may raise up seed to his brother.
29 Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
There were, then, seven brothers, and the first having taken a wife, died childless,
30 Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
and the second took the wife, and he died childless,
31 na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba—wote walikufa bila kuacha watoto.
and the third took her, and in like manner also the seven—they left no children, and they died;
32 Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
and last of all the woman also died:
33 Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba.”
in the resurrection, then, of which of them does she become wife? For the seven had her as wife.”
34 Yesu akawaambia, “Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa; (aiōn )
And Jesus answering said to them, “The sons of this age marry and are given in marriage, (aiōn )
35 lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa. (aiōn )
but those accounted worthy to obtain that age, and the resurrection that is out of the dead, neither marry, nor are they given in marriage; (aiōn )
36 Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
for neither are they able to die anymore—for they are like messengers—and they are sons of God, being sons of the resurrection.
37 Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
And that the dead are raised, even Moses showed at the Bush, since he calls the LORD the God of Abraham, and the God of Isaac, and the God of Jacob;
38 Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye.”
and He is not a God of dead men, but of living, for all live to Him.”
39 Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, “Mwalimu, umejibu vema kabisa.”
And certain of the scribes answering said, “Teacher, You said well”;
40 Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
and they no longer dared question Him anything.
41 Yesu akawauliza, “Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
And He said to them, “How do they say the Christ is [the] son of David,
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
and David himself says in [the] Scroll of Psalms, The LORD said to my Lord, Sit on My right hand,
43 mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.
Until I will make Your enemies Your footstool;
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye, Bwana, basi atakuwaje mwanawe?”
David, then, calls Him Lord, and how is He his son?”
45 Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
And all the people hearing, He said to His disciples,
46 “Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
“Take heed of the scribes, who are wishing to walk in long robes, and are cherishing salutations in the markets, and first seats in the synagogues, and first couches at the banquets,
47 Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!”
who devour the houses of the widows, and make long prayers for a pretense, these will receive more abundant judgment.”