< Luka 19 >
1 Yesu aliingia mjini Yeriko, akawa anapita katika njia za mji huo.
And having entered, He was passing through Jericho,
2 Kulikuwa na mtu mmoja mjini, jina lake Zakayo ambaye alikuwa mkuu wa watoza ushuru tena mtu tajiri.
and behold, a man, by name called Zaccheus, and he was a chief tax collector, and he was rich,
3 Alitaka kuona Yesu alikuwa nani, lakini kwa sababu ya umati wa watu, na kwa vile alikuwa mfupi, hakufaulu.
and he was seeking to see Jesus, who He is, and was not able for the multitude, because he was small in stature,
4 Hivyo, alitangulia mbio, akapanda juu ya mkuyu ili aweze kumwona Yesu, kwa maana alikuwa apitie hapo.
and having run forward before, he went up on a sycamore, that he may see Him, because through that [way] He was about to pass by.
5 Basi, Yesu alipofika mahali pale, aliangalia juu akamwambia, “Zakayo, shuka upesi, maana leo ni lazima nishinde nyumbani mwako.”
And as Jesus came up to the place, having looked up, He saw him and said to him, “Zaccheus, having hurried, come down, for it is necessary for Me to remain in your house today”;
6 Zakayo akashuka haraka, akamkaribisha kwa furaha.
and he having hurried came down, and received Him rejoicing;
7 Watu wote walipoona hayo, wakaanza kunung'unika wakisema, “Amekwenda kukaa kwa mtu mwenye dhambi.”
and having seen [it], they were all murmuring, saying, “He went in to lodge with a sinful man!”
8 Lakini Zakayo akasimama akamwambia Yesu, “Sikiliza Bwana! Mimi nitawapa maskini nusu ya mali yangu, na kama nimenyang'anya mtu yeyote kitu, nitamrudishia mara nne.”
And Zaccheus having stood, said to the LORD, “Behold, half of my goods, Lord, I give to the poor, and if I took by false accusation anything of anyone, I give back fourfold.”
9 Yesu akamwambia, “Leo wokovu umefika katika nyumba hii, kwa vile huyu pia ni wa ukoo wa Abrahamu.
And Jesus said to him, “Today salvation came to this house, inasmuch as he also is a son of Abraham;
10 Kwa maana Mwana wa Mtu amekuja kutafuta na kuokoa waliopotea.”
for the Son of Man came to seek and to save the lost.”
11 Wakati watu walipokuwa bado wanasikiliza hayo, Yesu akawaambia mfano. (Hapo alikuwa anakaribia Yerusalemu, na watu wale walidhani kwamba muda si muda, Ufalme wa Mungu ungefika.)
And while they are hearing these things, having added He spoke an allegory, because of His being near to Jerusalem, and of their thinking that the Kingdom of God is immediately about to appear.
12 Hivyo akawaambia, “Kulikuwa na mtu mmoja wa ukoo wa kifalme aliyefanya safari kwenda nchi ya mbali ili apokee madaraka ya ufalme, halafu arudi.
He therefore said, “A certain man of birth went on to a far country, to take to himself a kingdom, and to return,
13 Basi, kabla ya kuondoka aliwaita watumishi wake kumi, akawapa kiasi cha fedha kila mmoja na kumwambia: Fanyeni nazo biashara mpaka nitakaporudi.
and having called ten servants of his own, he gave ten minas to them and said to them, Do business—until I come;
14 Lakini wananchi wenzake walimchukia na hivyo wakatuma wajumbe waende wakaseme: Hatumtaki huyu atutawale.
and his citizens were hating him, and sent a delegation after him, saying, We do not wish this one to reign over us.
15 “Huyo mtu mashuhuri alirudi nyumbani baada ya kufanywa mfalme, na mara akaamuru wale watumishi aliowapa zile fedha waitwe ili aweze kujua kila mmoja amepata faida gani.
And it came to pass, on his coming back, having taken the kingdom, that he commanded these servants to be called to him, to whom he gave the money, that he might know what anyone had done in business.
16 Mtumishi wa kwanza akatokea, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara kumi ya zile fedha ulizonipa.
And the first came near, saying, Lord, your mina gained ten minas;
17 Naye akamwambia: Vema; wewe ni mtumishi mwema. Kwa kuwa umekuwa mwaminifu katika jambo dogo, utakuwa na madaraka juu ya miji kumi!
and he said to him, Well done, good servant, because you became faithful in a very little, be having authority over ten cities.
18 Mtumishi wa pili akaja, akasema: Mheshimiwa, faida iliyopatikana ni mara tano ya zile fedha ulizonipa.
And the second came, saying, Lord, your mina made five minas;
19 Naye akamwambia pia: Nawe utakuwa na madaraka juu ya miji mitano.
and he also said to this one, And you, become [ruler] over five cities.
20 “Mtumishi mwingine akaja, akasema: Chukua fedha yako; niliificha salama katika kitambaa,
And another came, saying, Lord, behold, your mina, that I had lying away in a napkin;
21 kwa maana niliogopa kwa sababu wewe ni mtu mkali. Wewe ni mtu ambaye huchukua yasiyo yako, na huchuma ambacho hukupanda.
for I was afraid of you, because you are an austere man; you take up what you did not lay down, and reap what you did not sow.
22 Naye akamwambia: Nakuhukumu kutokana na msemo wako, ewe mtumishi mbaya! Ulijua kwamba mimi ni mtu mkali, ambaye huchukua yasiyo yangu na kuchuma nisichopanda.
And he says to him, Out of your mouth I will judge you, evil servant: you knew that I am an austere man, taking up what I did not lay down, and reaping what I did not sow!
23 Kwa nini basi, hukuiweka fedha yangu benki, nami ningeichukua pamoja na faida baada ya kurudi kwangu?
And why did you not give my money to the bank, and I, having come, might have received it with interest?
24 Hapo akawaambia wale waliokuwa pale: Mnyang'anyeni hizo fedha, mkampe yule aliyepata faida mara kumi.
And to those standing by he said, Take the mina from him, and give to him having the ten minas—
25 Nao wakamwambia: Lakini Mheshimiwa, huyo ana faida ya kiasi hicho mara kumi!
(and they said to him, Lord, he has ten minas)—
26 Naye akawajibu: Kila aliye na kitu atapewa na kuzidishiwa. Lakini yule asiye na kitu, hata kile alicho nacho kitachukuliwa.
for I say to you that to everyone having will be given, and from him not having, also what he has will be taken from him,
27 Na sasa, kuhusu hao maadui wangu ambao hawapendi niwe mfalme wao, waleteni hapa, mkawaue papa hapa mbele yangu.”
but those my enemies, who did not wish me to reign over them, bring here and slay before me.”
28 Yesu alisema hayo, kisha akatangulia mbele yao kuelekea Yerusalemu.
And having said these things, He went on before, going up to Jerusalem.
29 Alipokaribia kufika Bethfage na Bethania, karibu na mlima wa Mizeituni, aliwatuma wanafunzi wake wawili,
And it came to pass, as He came near to Bethphage and Bethany, to that called the Mount of Olives, He sent two of His disciples,
30 akawaambia: “Nendeni katika kijiji kilicho mbele yenu. Mtakapokuwa mnaingia kijijini, mtamkuta mwana punda amefungwa ambaye hajatumiwa na mtu. Mfungeni, mkamlete hapa.
having said, “Go away into the village in front of [you], in which, entering in, you will find a colt bound, on which no one of men ever sat, having loosed it, bring [it];
31 Kama mtu akiwauliza, kwa nini mnamfungua, mwambieni, Bwana ana haja naye.”
and if anyone questions you, Why do you loose [it]? Thus you will say to him: The LORD has need of it.”
32 Basi, wakaenda, wakakuta sawa kama alivyowaambia.
And those sent, having gone away, found according as He said to them,
33 Walipokuwa wanamfungua yule mwana punda, wenyewe wakawauliza, “Kwa nini mnamfungua mwana punda huyu?”
and while they are loosing the colt, its owners said to them, “Why do you loose the colt?”
34 Nao wakawajibu, “Bwana anamhitaji.”
And they said, “The LORD has need of it”;
35 Basi, wakampelekea Yesu yule mwana punda. Kisha wakatandika mavazi yao juu yake wakampandisha Yesu.
and they brought it to Jesus, and having cast their garments on the colt, they sat Jesus on it.
36 Yesu akaendelea na safari, na watu wakatandaza mavazi yao barabarani.
And as He is going, they were spreading their garments in the way,
37 Alipofika karibu na Yerusalemu, katika mteremko wa mlima wa Mizeituni, umati wote na wanafunzi wake, wakaanza kushangilia na kumtukuza Mungu kwa sauti kubwa, kwa sababu ya mambo makuu waliyoyaona;
and as He is coming near now, at the descent of the Mount of Olives, the whole multitude of the disciples began rejoicing to praise God with a great voice for all the mighty works they had seen,
38 wakawa wanasema: “Abarikiwe Mfalme ajaye kwa jina la Bwana. Amani mbinguni, na utukufu juu mbinguni!”
saying, “Blessed [is] the King coming in the Name of the LORD; peace in Heaven, and glory in the highest!”
39 Hapo baadhi ya Mafarisayo waliokuwako katika lile kundi la watu, wakamwambia Yesu, “Mwalimu, wanyamazishe wanafunzi wako!”
And certain of the Pharisees from the multitude said to Him, “Teacher, rebuke Your disciples”;
40 Yesu akawajibu, “Nawaambieni, kama hawa wakinyamaza, hakika hayo mawe yatapaza sauti.”
and He answering said to them, “I say to you that if these will be silent, the stones will cry out!”
41 Alipokaribia zaidi na kuuona ule mji, Yesu aliulilia
And when He came near, having seen the city, He wept over it,
42 akisema: “Laiti ungelijua leo hii yale yaletayo amani! Lakini sasa yamefichika machoni pako.
saying, “If you knew, even you, at least in this your day, the things for your peace; but now they were hid from your eyes.
43 Maana siku zaja ambapo adui zako watakuzungushia maboma, watakuzingira na kukusonga pande zote.
Because days will come on you, and your enemies will cast a rampart around you, and surround you around, and press you on every side,
44 Watakupondaponda wewe pamoja na watoto wako ndani ya kuta zako; hawatakuachia hata jiwe moja juu jingine, kwa sababu hukuutambua wakati Mungu alipokujia kukuokoa.”
and lay you low, and your children within you, and they will not leave in you a stone on a stone, because you did not know the time of your inspection.”
45 Kisha, Yesu aliingia Hekaluni, akaanza kuwafukuzia nje wafanyabiashara
And having entered into the temple, He began to cast forth those selling in it, and those buying,
46 akisema, “Imeandikwa: Nyumba yangu itakuwa nyumba ya sala; lakini ninyi mmeifanya kuwa pango la wanyang'anyi.”
saying to them, “It has been written, My house is a house of prayer—but you made it a den of robbers.”
47 Yesu akawa anafundisha kila siku Hekaluni. Makuhani wakuu, walimu wa Sheria na viongozi wa watu walitaka kumwangamiza,
And He was teaching daily in the temple, but the chief priests and the scribes were seeking to destroy Him—also the chiefs of the people—
48 lakini hawakuwa na la kufanya, maana watu wote walikuwa wakimsikiliza kwa makini kabisa.
and they were not finding what they will do, for all the people were hanging on Him, hearing Him.