< 2 Timotheo 2 >
1 Basi, wewe mwanangu, uwe na nguvu katika neema tunayopata katika kuungana na Kristo Yesu.
Thou therefore, my son, be strong in the grace which is by Jesus the Messiah.
2 Chukua yale mafundisho uliyonisikia nikitangaza mbele ya mashahidi wengi, uyakabidhi kwa watu wanaoaminika, ambao wataweza kuwafundisha wengine pia.
And the things thou hast heard from me by many witnesses, these commit thou to faithful men, who are competent to teach others also.
3 Shiriki katika mateso kama askari mwaminifu wa Kristo yesu.
And endure evils, as a good soldier of Jesus the Messiah.
4 Mwanajeshi vitani hujiepusha na shughuli za maisha ya kawaida ili aweze kumpendeza mkuu wa jeshi.
No man, on becoming a soldier, entangleth himself with the business of the world; that he may please him who enlisted him.
5 Mwanariadha yeyote hawezi kushinda na kupata zawadi ya ushindi kama asipozitii sheria za michezo.
And if one contend in the games, he is not crowned, unless he contendeth according to the rules.
6 Mkulima ambaye amefanya kazi ngumu anastahili kupata sehemu ya kwanza ya mavuno.
The husbandman who laboreth, ought first to feed on his fruits.
7 Fikiria hayo ninayosema, kwani Bwana atakuwezesha uyaelewe yote.
Consider what I say. Our Lord give thee wisdom in all things.
8 Mkumbuke Yesu Kristo aliyefufuliwa kutoka wafu, aliyekuwa wa ukoo wa Daudi, kama isemavyo Habari Njema ninayoihubiri.
Be mindful of Jesus the Messiah, that he arose from the dead; who was of the seed of David, according to my gospel,
9 Kwa sababu ya kuihubiri Habari Njema mimi nateseka na nimefungwa minyororo kama mhalifu. Lakini neno la Mungu haliwezi kufungwa minyororo,
in which I suffer evils unto bonds, as if an evil-doer: but the word of God is not in bonds.
10 na hivyo navumilia kila kitu kwa ajili ya wateule wa Mungu, ili wao pia wapate ukombozi upatikanao kwa njia ya Yesu Kristo, na ambao huleta utukufu wa milele. (aiōnios )
Therefore I endure every thing, for the elect's sake; that they also may obtain life, in Jesus the Messiah, with eternal glory. (aiōnios )
11 Usemi huu ni wa kweli: “Ikiwa tulikufa pamoja naye, tutaishi pia pamoja naye.
Faithful is the saying, For if we shall have died with him, we shall also live with him;
12 Tukiendelea kuvumilia, tutatawala pia pamoja naye. Tukimkana, naye pia atatukana.
and, if we shall have suffered, we shall also reign with him. But if we shall have rejected him, he will reject us.
13 Tukikosa kuwa waaminifu, yeye hubaki mwaminifu daima, maana yeye hawezi kujikana mwenyewe.”
And if we shall have not believed in him, he abideth in his fidelity; for he cannot reject himself.
14 Basi, wakumbushe watu wako mambo haya, na kuwaonya mbele ya Mungu waache ubishi juu ya maneno. Ubishi huo haufai, ila huleta tu uharibifu mkuu kwa wale wanaousikia.
Of these things admonish thou them and charge them, before our Lord, that they dispute not, with unprofitable words, to the subversion of those who hear them.
15 Jitahidi kupata kibali kamili mbele ya Mungu kama mfanyakazi ambaye haoni haya juu ya kazi yake, na ambaye hufundisha sawa ule ujumbe wa kweli.
And study to present thyself before God, perfectly, a laborer who is not ashamed, one who correctly announceth the word of truth.
16 Jiepushe na majadiliano ya kidunia na ya kipumbavu; kwani hayo huzidi kuwatenga watu mbali na Mungu.
Avoid vain discourses, in which there is no profit; for they very much add to the wickedness of those occupied with them.
17 Mafundisho ya aina hiyo ni kama donda linalokula mwili. Miongoni mwa hao waliofundisha hayo ni Humenayo na Fileto.
And their discourse, like an eating cancer, will lay hold upon many. And one of these is Hymeneus, and another Philetus;
18 Hawa wamepotoka kabisa mbali na ukweli, na wanatia imani ya watu wengine katika wasiwasi kwa kusema ati ufufuo wetu umekwisha fanyika.
who have wandered from the truth, while they say, The resurrection of the dead hath passed: and they subvert the faith of some.
19 Lakini msingi thabiti uliowekwa na Mungu uko imara, na juu yake yameandikwa maneno haya: “Bwana anawafahamu wale walio wake,” na “Kila asemaye yeye ni wa Bwana, ni lazima aachane na uovu.”
But the firm foundation of God standeth; and it hath this seal, The Lord knoweth them who are his: and, Let every one who invoketh the name of our Lord, stand aloof from iniquity.
20 Katika nyumba kubwa kuna mabakuli na vyombo vya kila namna: vingine ni vya fedha na dhahabu, vingine vya mbao na udongo, vingine ni vya matumizi ya pekee na vingine kwa ajili ya matumizi ya kawaida.
But in a great house, there are not only vessels of gold or silver, but also of wood and of pottery; and some of them for honor, and some for dishonor.
21 Basi, kama mtu atajitakasa kwa kujitenga mbali na mambo hayo yote maovu, atakuwa chombo cha matumizi ya pekee, kwa sababu amewekwa wakfu, anamfaa Bwana wake na yupo tayari kwa kila kazi njema.
If therefore any one purge himself from these things, he will be a pure vessel for honor, fit for the use of his Lord, and prepared for every good work.
22 Jiepushe na tamaa za ujana, fuata uadilifu, imani, upendo, amani, pamoja na watu wote ambao wanamwomba Bwana kwa moyo safi.
Fly from all the lusts of youth; and follow after righteousness, and faith, and love, and peace, with them that invoke our Lord with a pure heart.
23 Epuka ubishi wa kijinga na kipumbavu; wajua kwamba hayo huleta magomvi.
Avoid those foolish discussions which afford no instruction; for thou knowest, that they generate contests.
24 Mtumishi wa Bwana asigombane. Anapaswa kuwa mpole kwa watu wote, mwalimu mwema na mvumilivu,
And a servant of our Lord ought not to contend, but to be mild towards every one, and instructive, and patient;
25 ambaye ni mpole anapowaonya wapinzani wake, kwani huenda Mungu akawajalia nafasi ya kutubu, wakapata kuujua ukweli.
that with mildness he may enlighten those who dispute against him, if perhaps God may give them repentance, and they may acknowledge the truth,
26 Hapo fahamu zao zitawarudia tena, wakaponyoka katika mtego wa Ibilisi aliyewanasa na kuwafanya wayatii matakwa yake.
and may recollect themselves, and may escape out of the snare of Satan, at whose pleasure they have been held ensnared.