< 1 Timotheo 1 >

1 Mimi Paulo, mtume wa Yesu Kristo kwa amri ya Mungu Mwokozi wetu na Yesu Kristo tumaini letu,
PAUL, a legate of Jesus the Messiah, by the command of God our life-giver, and of the Messiah, Jesus our hope;
2 nakuandikia Timotheo mwanangu halisi katika imani. Nakutakia neema, huruma na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Kristo Yesu Bwana wetu.
to Timothy, my true son in the faith: grace and mercy and peace, from God our Father, and the Messiah, Jesus our Lord.
3 Napenda ukae huko Efeso, kama nilivyokuomba nilipokuwa ninakwenda Makedonia. Wako watu fulani huko wanaofundisha mafundisho ya uongo. Wakomeshe watu hao.
When I was going into Macedonia, I requested thee to remain at Ephesus, and to charge certain persons not to teach different doctrines;
4 Waambie waachane na zile hadithi tupu na orodha ndefu za mababu, ambazo huleta tu ubishi, wala haviwajengi watu katika mpango ujulikanao kwa imani.
and not to throw themselves into fables and stories about genealogies, of which there is no end, which produce contention rather than edification in the faith of God.
5 Shabaha ya amri hii ni kuhimiza mapendo yatokayo katika moyo safi, dhamiri njema, na imani ya kweli.
Now the end of the command is love, which is from a pure heart, and from a good conscience, and from true faith.
6 Watu wengine wamepotoka na kugeukia majadiliano yasiyo na maana.
But from these some have strayed, and have turned aside to vain words;
7 Wanapenda kuwa walimu wa Sheria, lakini hawaelewi maneno yao wenyewe au mambo wanayosisitiza.
because they wished to be teachers of the law, while they understood not what they speak, nor the thing about which they contend.
8 Twajua kwamba Sheria ni njema, kama ikitumiwa ipasavyo.
Now, we know, that the law is a good thing, if a man conduct himself in it, according to the law,
9 Lakini tunapaswa kukumbuka kwamba sheria haziwekwi kwa ajili ya watu wema, bali kwa ajili ya wahalifu na wasiotii, wasiomcha Mungu na wenye dhambi, watu wasio na dini na wa kidunia. Watu wanaowaua baba na mama zao, au wauaji wowote wale;
he knowing that the law was not established for the righteous, but for the evil, and the rebellious, and the ungodly, and the sinful, and the perverse and for the impure, and for smiters of their fathers and smiters of their mothers, and for murderers,
10 sheria imewekwa kwa ajili ya waasherati, wafiraji, wanaowaiba watu, waongo, na wanaoapa uongo au wanaofanya chochote ambacho ni kinyume cha mafundisho ya kweli.
and for whoremongers, and for copulators with males, and for the stealers of free people, and for liars, and for violators of oaths, and for whatever is contrary to sound doctrine,
11 Mafundisho hayo hupatikana katika Habari Njema ambayo mimi nimekabidhiwa niihubiri, Habari Njema ya Mungu mtukufu na mwenye heri.
namely that of the glorious gospel of the blessed God, with which I am intrusted.
12 Namshukuru Bwana wetu Yesu Kristo aliyenipa nguvu kwa ajili ya kazi yangu. Namshukuru kwa kuniona mimi kuwa ni mwaminifu, akaniteua nimtumikie,
And I thank him who strengthened me, even our Lord Jesus the Messiah; who accounted me faithful, and appointed me to his ministry;
13 ingawa pale awali mimi nilimtukana na kumtesa na kumdhulumu. Lakini Mungu alinionea huruma, kwa sababu sikuwa na imani bado, na hivyo sikujua nilichokuwa ninafanya.
me I say, who before was a blasphemer, and a persecutor, and a reviler; but I obtained mercy, because I did it while ignorant and without faith.
14 Lakini Bwana wetu alinijalia neema yake kwa wingi, akanipa imani na upendo katika kuungana na Kristo Yesu.
And in me the grace of our Lord abounded, and faith and love, which is in Jesus the Messiah.
15 Usemi huu ni wa kuaminika, na tena unafaa kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja ulimwenguni kuwaokoa wenye dhambi. Nami ni mkosefu zaidi kuliko hao wote,
Faithful is the declaration, and worthy to be received, that Jesus the Messiah came into the world to give life to sinners, of whom I was the primary.
16 lakini Mungu alinionea huruma, ili Kristo aonyeshe uvumilivu wake wote kwangu mimi, kama mfano kwa wale wote ambao baadaye watamwamini na kupokea uzima wa milele. (aiōnios g166)
But for this cause had he mercy on me, that in me first Jesus the Messiah might display all his long suffering, for an example to them who were to believe on him unto life eternal. (aiōnios g166)
17 Kwake yeye aliye Mfalme wa milele na asiyekufa, yeye aliye Mungu pekee—kwake viwe heshima na utukufu milele na milele! Amina. (aiōn g165)
And to the king eternal, incorruptible, and invisible, the sole God, be honor and glory for ever and ever! Amen. (aiōn g165)
18 Mwanangu Timotheo, nakukabidhi amri hii kufuatana na maneno ya unabii yaliyosemwa zamani juu yako. Yatumie maneno hayo yawe silaha yako katika kupigana vita vizuri,
This injunction I commit to thee, my son Timothy, according to the former predictions concerning thee, that in them thou mightest war this good warfare,
19 na ushike imani yako na dhamiri njema. Watu wengine hawakusikiliza dhamiri zao na hivyo wakaiharibu imani yao.
in faith and a good conscience; for they who have repudiated this, have become destitute of faith;
20 Miongoni mwao ni Humenayo na Aleksanda ambao nimewakabidhi kwa Shetani, ili wafundishwe wasimtukane Mungu.
like Hymeneus and Alexander, whom I have delivered up to Satan, that they may learn not to be blasphemers.

< 1 Timotheo 1 >