< 2 Wathesalonike 1 >

1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba yetu na wa Bwana Yesu Kristo.
Paul and Silvanus and Timothy to the church of the Thessalonians in God our Father, and in the Lord Jesus Christ;
2 Tunawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana Yesu Kristo.
grace be to you and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
3 Ndugu, tunapaswa kushukuru Mungu daima kwa ajili yenu. Inafaa kwetu kufanya hivyo kwani imani yenu inakua sana na kupendana kwenu kunaongezeka sana.
We ought always to give thanks to God on your account, my brethren, as it is fit; because your faith increaseth greatly, and the love of every one of you towards each other aboundeth:
4 Ndio maana sisi tunajivunia ninyi katika makanisa ya Mungu. Tunaona fahari juu ya jinsi mnavyoendelea kuamini na kustahimili katika udhalimu wote na mateso mnayopata.
so that we ourselves boast of you among the churches of God, for your patience and faith under all your persecutions and afflictions which ye endure.
5 Hayo yote yanathibitisha kwamba hukumu ya Mungu ni ya haki, na matokeo yake ninyi mtastahili Utawala wake ambao kwa ajili yake mnateseka.
Which are a demonstration of the just judgement of God, that ye may be counted worthy of the kingdom of God, for which ye also suffer:
6 Mungu atafanya jambo la haki: atawalipa mateso wale wanaowatesa ninyi,
seeing it is a righteous thing with God to render affliction to those that afflict you;
7 na kuwapeni nafuu ninyi mnaoteseka, na sisi pia. Atafanya jambo hilo wakati Bwana atakapotokea kutoka mbinguni pamoja na malaika wake na wakuu
and to you, who are in trouble, rest with us, at the revelation of the Lord Jesus from heaven,
8 na miali ya moto, kuwaadhibu wale wanaomkataa Mungu na wale wasiotii Habari Njema ya Bwana wetu Yesu.
with his mighty angels, in flaming fire, taking vengeance on those who know not God, and who obey not the gospel of our Lord Jesus Christ:
9 Adhabu yao itakuwa kuangamizwa milele na kutengwa mbali na utukufu wake mkuu, (aiōnios g166)
who shall be punished with everlasting destruction, by the presence of the Lord and by his glorious power: (aiōnios g166)
10 wakati atakapokuja Siku ile kupokea utukufu kutoka kwa watu wake na heshima kutoka kwa wote wanaoamini. Ninyi pia mtakuwa miongoni mwao, kwani mmeuamini ule ujumbe tuliowaletea.
in that day, when He shall come to be glorified in his saints, and to be admired in all them that believe; because our testimony among you was believed.
11 Ndiyo maana tunawaombeeni daima. Tunamwomba Mungu wetu awawezeshe muyastahili maisha aliyowaitia myaishi. Tunamwomba, kwa uwezo wake, atimize nia yenu ya kutenda mema na kukamilisha kazi yenu ya imani.
Wherefore we pray always for you, that our God would count you worthy of this calling, and fulfil all the good pleasure of his goodness, and the work of faith with power:
12 Kwa namna hiyo, jina la Bwana wetu Yesu litapata utukufu kutoka kwenu, nanyi mtapata utukufu kutoka kwake kwa neema ya Mungu wetu na ya Bwana Yesu Kristo.
that the name of our Lord Jesus Christ may be glorified in you, and ye in Him, according to the grace of our God, and of the Lord Jesus Christ.

< 2 Wathesalonike 1 >