< 1 Wathesalonike 1 >

1 Mimi Paulo, Silwano na Timotheo tunawaandikia ninyi jumuiya ya kanisa la Thesalonike, ambao ni watu wake Mungu Baba, na wa Bwana Yesu Kristo.
Paul and Silvanus and Timothy to the church of the Thessalonians in God the Father, and in the Lord Jesus Christ. Grace be to you, and peace from God our Father, and from the Lord Jesus Christ.
2 Tunamshukuru Mungu daima kwa ajili yenu ninyi nyote na kuwakumbukeni daima katika sala zetu.
We give thanks to God always for you all, making mention of you in our prayers.
3 Maana, mbele ya Mungu Baba yetu, twakumbuka jinsi mnavyoonyesha imani yenu kwa matendo, jinsi upendo wenu unavyowawezesha kufanya kazi kwa bidii, na jinsi tumaini lenu katika Bwana wetu Yesu Kristo lilivyo thabiti.
Incessantly remembering your work of faith, and labor of love, and patience of hope in our Lord Jesus Christ, before our God and Father:
4 Ndugu, twajua kwamba Mungu anawapenda na kwamba amewateua muwe watu wake,
knowing, beloved brethren, your election by God.
5 maana wakati tulipowahubirieni ile Habari Njema haikuwa kwa maneno tu, bali pia kwa nguvu na kwa Roho Mtakatifu, tukiwa na hakika kwamba ujumbe huo ulikuwa wa kweli. Mnajua jinsi tulivyoishi pamoja nanyi; tuliishi kwa manufaa yenu.
For our gospel came not to you in word only, but also in power, and in the holy Ghost, and in much certainty; as ye know what sort of persons we were among you for your sakes.
6 Ninyi mlifuata mfano wetu, na kumwiga Bwana. Ingawa mliteswa sana, mliupokea ujumbe huo kwa furaha itokayo kwa Roho Mtakatifu.
And ye became imitators of us and of the Lord, having received the word tho' in much affliction, yet with joy of the holy Ghost.
7 Kwa hiyo ninyi mmekuwa mfano mzuri kwa waumini wote wa Makedonia na Akaya.
So that ye became examples to all the believers in Macedonia and Achaia.
8 Maana, kutokana na bidii yenu ujumbe wa Bwana umesikika si tu huko Makedonia na Akaya, bali imani yenu kwa Mungu imeenea popote. Tena hatuhitaji kusema zaidi.
For the word of the Lord sounded forth from you, not only in Macedonia and Achaia; but also in every place your faith towards God is spread abroad, so that we have no need to say any thing of it.
9 Watu hao wanazungumza juu ya ziara yetu kwenu: jinsi mlivyotukaribisha, jinsi mlivyoziacha sanamu mkamgeukia Mungu aliye hai na wa kweli,
For they themselves declare concerning us what kind of entrance we had among you, and how ye turned to God from idols, to serve the living and true God;
10 na sasa mwamngojea Mwanae ashuke kutoka mbinguni, Yesu, ambaye Mungu alimfufua kutoka wafu, na ambaye anatuokoa katika ghadhabu ya Mungu inayokuja.
and to wait for his Son from heaven, whom He raised from the dead, even Jesus who delivereth us from the wrath to come.

< 1 Wathesalonike 1 >