< 2 Petro 1 >

1 Mimi Simoni Petro, mtumishi na mtume wa Yesu Kristo, nawaandikia ninyi ambao, kwa wema wake Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo, mmejaliwa imani ileile ya thamani kuu tuliyojaliwa sisi.
Simon Peter, a servant and an apostle of Jesus Christ, to them that have obtained like precious faith with us, in the righteousness of our God, and of our saviour Jesus Christ:
2 Nawatakieni neema na amani tele katika kumjua Mungu na Yesu Bwana wetu.
grace and peace be multiplied unto you, in the acknowledgement of God, and of Jesus our Lord;
3 Kwa uwezo wake wa kimungu, Mungu ametujalia mambo yote tunayohitaji, ili tuishi maisha ya kumcha Mungu kwa kumjua yeye aliyetuita tuushiriki utukufu na wema wake yeye mwenyewe.
as his divine power hath given us all things that pertain to life and godliness, through the knowledge of Him who hath called us by that glory and virtue,
4 Kwa namna hiyo ametujalia zawadi kuu na za thamani ambazo alituahidia, ili kwa zawadi hizo mpate kuziepa kabisa tamaa mbaya zilizomo duniani, na mpate kuishiriki hali yake ya kimungu.
by which are given unto us exceeding great and precious promises; that by these ye may become partakers of a divine nature, having escaped the corruption that is in the world through lust.
5 Kwa sababu hiyo, fanyeni bidii ya kuongeza fadhila katika imani yenu: ongezeni elimu katika fadhila yenu,
And to this giving all diligence, add to your faith fortitude;
6 kuwa na kiasi katika elimu yenu, uvumilivu katika kuwa na kiasi, uchaji wa Mungu katika uvumilivu wenu,
and to fortitude knowledge; and to knowledge temperance; and to temperance patience; and to patience piety;
7 udugu katika uchaji wenu, na mapendo katika udugu wenu.
and to piety brotherly affection; and to brotherly affection charity.
8 Mkiwa na sifa hizo zote kwa wingi, zitawawezesheni kuwa watendaji na kupata faida katika kumjua Bwana wetu Yesu Kristo.
For if these be in you and abound, they will not suffer you to be idle, nor unfruitful in the knowledge of our Lord Jesus Christ.
9 Lakini mtu asiye na sifa hizo ni kipofu, hawezi kuona na amesahau kwamba alikwisha takaswa dhambi zake za zamani.
But he, that hath not these, is blind, or short-sighted, having forgot his baptismal purification from his former sins.
10 Kwa hiyo basi, ndugu zangu, fanyeni bidii zaidi kuufanya huo wito wenu mlioitiwa na Mungu uwe jambo la kudumu katika maisha yenu; kama mkiishi namna hiyo hamtaanguka kamwe.
Wherefore, my brethren, be the more diligent thus to make your calling and election sure; for if ye do these things ye shall never fall.
11 Kwa namna hiyo mtafaulu kupewa haki kamili ya kuingia katika Utawala wa milele wa Bwana na Mwokozi wetu Yesu Kristo. (aiōnios g166)
For so an entrance shall be administered unto you abundantly into the everlasting kingdom of our Lord and Saviour Jesus Christ. (aiōnios g166)
12 Kwa hiyo nitaendelea kuwakumbusheni daima mambo haya, ingawa mmekwisha yafahamu, na mko imara katika ukweli mlioupokea.
Wherefore I will not neglect to put you always in mind of these things, though ye know them, and are established in the present truth.
13 Nadhani ni jambo jema kwangu, muda wote niishio hapa duniani, kuwapeni moyo na kuwakumbusheni juu ya mambo haya.
And I think it my duty, while I am in this tabernacle, to stir you up by way of remembrance:
14 Najua kwamba karibu nitauweka kando mwili huu wenye kufa, kama Bwana alivyoniambia waziwazi.
knowing that I must soon lay down this my tabernacle, even as our Lord Jesus Christ hath shewed me.
15 Basi, nitajitahidi kuwapatieni njia ya kuyakumbuka mambo haya kila wakati, baada ya kufariki kwangu.
And I will endeavour that after my departure also ye may always be able to call these things to remembrance.
16 Wakati tulipowafundisheni juu ya ukuu wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo, hatukutegemea hadithi tupu zisizo na msingi. Sisi tuliuona utukufu wake kwa macho yetu wenyewe.
For we did not follow artfully devised fables, when we made known unto you the power and coming of our Lord Jesus Christ; but were eye-witnesses of his majesty.
17 Sisi tulikuwapo wakati alipopewa heshima na kutukuzwa na Mungu Baba, wakati sauti ilipomjia kutoka kwake yeye aliye Utukufu Mkuu, ikisema: “Huyu ni Mwanangu mpenzi, nimependezwa naye.”
For He received from God the Father honor and glory when a voice came to Him from the magnificent glory, saying, "This is my beloved Son, in whom I am well pleased."
18 Tena, sisi wenyewe tulisikia sauti hiyo kutoka mbinguni wakati tulipokuwa pamoja naye juu ya ule mlima mtakatifu.
And this voice, from heaven we heard, when we were with Him in the holy mount.
19 Tena, ujumbe wa manabii watuthibitishia jambo hilo; nanyi mwafanya vema kama mkiuzingatia, maana ni kama taa inayoangaza mahali penye giza mpaka Siku ile itakapopambazuka na mwanga wa nyota ya asubuhi utakapong'ara mioyoni mwenu.
We have also the more sure word of the prophets, to which ye do well to attend, as to a lamp shining in a dark place, till the day dawn, and the morning-star rise in your hearts:
20 Zaidi ya hayo, lakini, kumbukeni kwamba hakuna mtu yeyote awezaye kufafanua mwenyewe unabii ulio katika Maandiko Matakatifu.
knowing this first, that no prophecy of scripture is of private interpretation;
21 Maana hakuna ujumbe wa kinabii unaotokana na matakwa ya binadamu, bali watu walinena ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mtakatifu.
for prophecy was not delivered of old at the will of man, but holy men of God spake as they were moved by the holy Spirit.

< 2 Petro 1 >