< 2 Petro 3 >

1 Wapenzi wangu, hii ni barua ya pili ninayowaandikia. Katika barua hizo mbili nimejaribu kufufua fikira safi akilini mwenu kwa kuwakumbusheni mambo haya.
This second epistle, my beloved, I now write unto you; in both which I stir up your sincere mind in remembrance,
2 Napenda mkumbuke maneno yaliyosemwa na manabii watakatifu, na ile amri ya Bwana na Mwokozi mliyopewa na mitume wenu.
that ye may be mindful of the words formerly spoken by the holy prophets, and of the commandment of us the apostles of the Lord and Saviour: knowing this first,
3 Awali ya yote jueni kwamba siku za mwisho watakuja watu ambao mienendo yao inatawaliwa na tamaa zao mbaya. Watawadhihaki ninyi
that there will come in the last days scoffers,
4 na kusema: “Aliahidi kwamba atakuja! Je, sasa yuko wapi? Mambo ni yaleyale tangu babu zetu walipokufa; hali ya vitu ni ileile kama ilivyokuwa mwanzo wa ulimwengu!”
walking after their own lusts, and saying, Where is the declaration of his coming? for except that the fathers are fallen asleep, all things remain as they were from the beginning of the creation.
5 Watu hao, kwa makusudi, husahau kwamba zamani Mungu alinena, nazo mbingu na nchi zikaumbwa. Dunia iliumbwa kutoka katika maji na kwa maji;
For they are willingly ignorant of this, that by the Word of God the heavens were made of old, and the earth too from the water, and subsisting on the water.
6 na kwa maji hayo, yaani yale maji ya gharika kuu, dunia ya wakati ule iliangamizwa.
Whence the old world being drowned in water perished.
7 Lakini mbingu na nchi za sasa zahifadhiwa kwa neno la Mungu kwa ajili ya kuharibiwa kwa moto. Zimewekwa kwa ajili ya Siku ile ambapo watu wasiomcha Mungu watahukumiwa na kuangamizwa.
But the heavens and the earth, that now are, by the same Word are kept in store, reserved unto fire on the day of judgement and destruction of ungodly men.
8 Lakini, wapenzi wangu, msisahau kitu kimoja! Mbele ya Bwana, hakuna tofauti kati ya siku moja na miaka elfu; kwake yote ni mamoja.
But, beloved; be not ignorant of this one thing, that one day is with the Lord as a thousand years, and a thousand years as one day.
9 Bwana hakawii kutimiza yale aliyoahidi kama watu wengine wanavyofikiri kuwa atakawia. Yeye ana saburi kwa ajili yenu, maana hapendi hata mmoja wenu apotee, bali huwavuta wote wapate kutubu.
The Lord is not slow as to his promise (as some count it slowness) but is long-suffering towards us, not willing that any should perish, but that all should come to repentance.
10 Siku ya Bwana itakuja kama mwizi. Siku hiyo, mbingu zitatoweka kwa kishindo kikuu; vitu vyake vya asili vitateketezwa kwa moto, nayo dunia itatoweka pamoja na kila kitu kilichomo ndani yake.
But the day of the Lord will come as a thief in the night, in which the heavens shall pass away with a great noise, and the elements being set on fire shall be dissolved, and the earth and the works therein shall be burnt up.
11 Maadamu kila kitu kitaharibiwa namna hiyo, je, ninyi mnapaswa kuwa watu wa namna gani? Mnapaswa kuishi kitakatifu na kumcha Mungu,
Seeing then that all these things shall be dissolved, what manner of persons ought ye to be in holy conversation and godliness,
12 mkiingojea Siku ile ya Mungu na kuifanya ije upesi—Siku ambayo mbingu zitateketezwa kwa moto na kuharibiwa, na vitu vyake vya asili vitayeyushwa kwa joto.
expecting and hastening on the coming of the day of God, whereby the heavens being set on fire shall be dissolved, and the burning elements shall be melted.
13 Lakini sisi, kufuatana na ahadi yake, twangojea mbingu mpya na dunia mpya ambayo imejaa uadilifu.
But we, according to his promise, look for new heavens and a new earth, in which righteousness dwelleth.
14 Kwa hiyo wapenzi wangu, mkiwa mnangojea Siku ile, fanyeni bidii kuwa safi kabisa bila hatia mbele ya Mungu, na kuwa na amani naye.
Wherefore, beloved, seeing ye expect these things, give diligence to be found of Him in peace, spotless and blameless;
15 Mnapaswa kuuona uvumilivu wa Bwana kuwa ni nafasi anayowapeni mpate kuokolewa, kama Paulo ndugu yetu mpenzi alivyowaandikia akitumia hekima aliyopewa na Mungu.
and account the long-suffering of our Lord salvation, as our beloved brother Paul also, according to the wisdom given to him, hath written unto you;
16 Hayo ndiyo asemayo katika barua zake zote anapozungumzia suala hilo. Yapo mambo kadhaa katika barua zake yaliyo magumu kuyaelewa, mambo ambayo watu wajinga, wasio na msimamo, huyapotosha kama wanavyopotosha sehemu nyingine za Maandiko Matakatifu. Hivyo wanasababisha maangamizi yao wenyewe.
as also in all his epistles, speaking in them of these things: in which are some things hard to be understood, which the illiterate and unstable wrest, as they do also the other scriptures, to their own destruction.
17 Lakini ninyi, wapenzi wangu, mmekwisha jua jambo hili. Basi, muwe na tahadhari msije mkapotoshwa na makosa ya waasi, mkaanguka kutoka katika msimamo wenu imara.
Do ye therefore, beloved, as ye know these things before, take heed least being seduced together with them by the error of the wicked, ye should fall from your own stedfastness.
18 Lakini endeleeni kukua katika neema na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo. Utukufu uwe kwake, sasa na hata milele! Amina. (aiōn g165)
But grow in grace, and in the knowledge of our Lord and Saviour Jesus Christ: to Him be glory both now and for ever. Amen. (aiōn g165)

< 2 Petro 3 >

The World is Destroyed by Water
The World is Destroyed by Water