< 2 Wakorintho 8 >

1 Ndugu, tunapenda kuwapa habari juu ya neema ambazo Mungu ameyajalia makanisa ya Makedonia.
弟兄們! 如今田願意告訴你們:天主在馬其頓所施與的恩惠,
2 Waumini wa huko walijaribiwa sana kwa taabu; lakini furaha yao ilikuwa kubwa hivi hata wakawa wakarimu kupita kiasi, ingawaje walikuwa maskini sana.
就是他們在患難頻繁的試探中所充滿的喜樂,和他們極度的貧困所湧出的豐厚慷慨,。
3 Naweza kushuhudia kwamba walikuwa wakarimu kadiri ya nguvu zao na hata zaidi. Kwa hiari yao wenyewe,
我可以作證:他們是盡了力量,甚至超過了力量,自動的捐輸,
4 walitusihi sana wapewe nafasi ya kushiriki katika huduma hii ya kuwasaidia watu wa Mungu.
再三懇求我們准他們分享供應聖徒的恩惠。
5 Hilo lilikuwa jambo ambalo hatukulitazamia kabisa! Kwanza walijitolea wao wenyewe kwa Bwana, kisha wakajitolea wenyewe kwetu pia, kufuatana na mapenzi ya Mungu.
他們所作的,不但如我們所盻望的,而且按照天主的旨意把自己先奉獻給主也獻給了我們;
6 Kwa sababu hiyo, tulimsihi Tito aliyeianza kazi hiyo awasaidieni pia muitekeleze huduma hii ya upendo miongoni mwenu.
因此我們請求弟鐸,他既然開始了這慈善的事,也在你們中予以完成。
7 Ninyi mna kila kitu: imani, uwezo wa kusema, elimu; bidii yote ya kutenda mema, na upendo wenu kwetu. Hivyo, tunatazamia muwe wakarimu katika huduma hii ya upendo.
就如你們在一切事上,在信德語言、知識和各種熱情上,並在我們所交於你們的愛情上,超群出眾,這樣也要在這慈善事上超群出眾。
8 Siwapi ninyi amri, lakini nataka tu kuonyesha jinsi wengine walivyo na bidii ya kusaidia ili nipate kujua jinsi upendo wenu ulivyo wa kweli.
我說這話並不是出命,而是藉別人的熱情來試探你們愛情的真誠。
9 Maana, ninyi mnajua neema ya Bwana wetu Yesu Kristo: yeye, ingawa alikuwa na kila kitu, alijifanya maskini kwa ajili yenu, ili kutokana na umaskini wake, awatajirishe.
因為你們知道我們的主耶穌基督的恩賜:衪本是富有的,為了你們卻成了貧困的,好使你們因著衪的貧困而成為富有的。
10 Kuhusu jambo hili, basi, nawapeni shauri hili: inafaa kwenu kutekeleza sasa yale mliyoanza mwaka jana. Ninyi mlikuwa wa kwanza kuchukua hatua na kuamua kufanya hivyo.
我在這事上只給你們供獻意見,因為這樣更適合於你們,因為你們從去年不但己開始實行了,而且還是出於自願。
11 Basi, kamilisheni shughuli hiyo; na kama vile mlivyokuwa na hamu kubwa ya kusaidia, basi, fanyeni bidii vivyo hivyo, kadiri ya uwezo wenu, kuikamilisha.
所以如今,請完成你們所實行的事罷! 好使你們怎樣甘心情願,也怎樣照所有的予以完成,
12 Maana ikiwa mtu ana moyo wa kusaidia, Mungu hupokea kila anachoweza kutoa: hadai zaidi.
因為只要有甘心情願在,蒙受悅納是照所有,不是照所無的。
13 Ninyi hampaswi kuongezewa taabu kusudi wengine wapunguziwe mzigo wao; sivyo, ila ni lazima tujali usawa na haki.
這不是說要使別人輕鬆,叫你們為難;而是說要出於均勻:
14 Kila mlicho nacho sasa cha ziada kiwasaidie wale wanaohitaji, ili nao wakati watakapokuwa na ziada, wawasaidie ninyi katika mahitaji yenu, na hivyo kuwe na usawa.
在現今的時候,你們的富裕彌補了他們的缺乏,好使他們的富裕也彌補的你們的缺乏,這樣就有了均勻,
15 Kama Maandiko yasemavyo: “Aliyekusanya kwa wingi hakuwa na ziada, na yule aliyekusanya kidogo hakupungukiwa.”
正如所記載的:『多收的沒有富裕,少收的也沒有不足。』
16 Namshukuru Mungu aliyeweka ndani ya moyo wa Tito hamu hiyo niliyo nayo mimi ya kuwasaidia.
感謝天主,把我對你們所有的同樣慹情賜在弟鐸的心裏,
17 Si tu kwamba alikubali ombi letu, ila pia alikuwa na hamu kubwa ya kusaidia, hata akaamua kwa hiari yake mwenyewe kuja kwenu.
因為他接受了我們的請求,而且因他更為關心,便自動起身往你們那裏去了。
18 Pamoja naye, tunamtuma ndugu mmoja ambaye sifa zake katika kueneza Habari Njema zimeenea katika makanisa yote.
同時我也打發了一位弟兄和他同去,這人在宣講福音上所受讚美傳遍了各教會──
19 Zaidi ya hayo, yeye amechaguliwa na makanisa awe mwenzetu safarini wakati tunapopeleka huduma hii yetu ya upendo, huduma tunayoifanya kwa ajili ya utukufu wa Bwana na uthibitisho wa nia yetu njema.
不但如此,而且各教會也派定他作我們的旅伴,我們經管這事是為主的光榮,並為表現我們的好心──
20 Tunataka kuepa lawama zinazoweza kutokea kuhusu usimamizi wetu juu ya zawadi hii karimu.
我們這樣防範,是為避免有人在我們所經營的這巨款上來毀謗我們,
21 Nia yetu ni kufanya vema, si tu mbele ya Bwana, lakini pia mbele ya watu.
因為我們不但在主面前關心我們的美名,而也在人的面前前。
22 Basi, pamoja na ndugu hao, tumemtuma ndugu yetu mwingine ambaye mara nyingi tumempa majaribio mbalimbali, tukamwona kuwa ni mwenye hamu kubwa ya kusaidia; hata sasa amekuwa na moyo zaidi kwa sababu ana imani sana nanyi.
我們還打發了一位弟兄與他們同去,我們在許多事上,屢次驗過他是熱情的;如今因他對你們大有信心,當然更加熱情了。
23 Tito ni mwenzangu; tunafanya kazi pamoja kwa ajili yenu; lakini kuhusu hawa ndugu zetu wengine, wanaokuja pamoja nao, hao ni wajumbe wa makanisa, na utukufu kwa Kristo.
論到弟鐸,他是我的同伴,為你們也是我的助手;論到我們的那兩位弟兄,他們是教會的使者,是基督的光榮,
24 Basi, waonyesheni uthabiti wa upendo wenu, makanisa yapate kuona kweli kwamba fahari ninayoona juu yenu ni ya halali.
所以你們要在眾教會前,向他們證實你們的愛情,和我們對你們所有的誇耀。

< 2 Wakorintho 8 >