< 1 Wakorintho 1 >

1 Mimi Paulo, niliyeitwa kuwa mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na ndugu Sosthene,
因天主的旨意,蒙召為耶穌基督宗徒的保祿和索斯特及弟兄,
2 tunawaandikia ninyi mlio kanisa la Mungu huko Korintho. Ninyi mmefanywa watakatifu katika kuungana na Kristo Yesu, mkaitwa muwe watu wa Mungu, pamoja na watu wote popote wanaomwomba Bwana wetu Yesu Kristo aliye Bwana wao na wetu pia.
致書給格林多的天主教會,就是給那些在基督耶穌內受祝聖,與一切在各地呼求我們的主,亦即他們和我們的主尸基督之名,一同蒙召為聖的人。
3 Nawatakieni neema na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu na Bwana wetu Yesu Kristo.
願恩寵與平安,由我們的父天主和主耶穌基督賜給你們。
4 Ninamshukuru Mungu wangu daima kwa ajili yenu kwa sababu amewatunukia ninyi neema yake kwa njia ya Kristo Yesu.
我時時為你們,對天主在基督耶穌內所賜與你們的恩寵,而感謝我的又主,
5 Maana, kwa kuungana na Kristo mmetajirishwa katika kila kitu. Mmejaliwa elimu yote na uwezo wote wa kuhubiri,
因為藉著祂,你們在一切事上,在一切言論和知識上,都成了富有的;
6 kwani, ujumbe juu ya Kristo umethibitishwa ndani yenu,
並且我為基督所作的證言,在你們中是這樣的堅定,
7 hata hampungukiwi kipaji chochote cha kiroho mkiwa mnangojea kufunuliwa kwake Bwana wetu Yesu Kristo.
以致你們已不缺少任何恩寵,只待我們的主耶穌基督的出現;
8 Yeye atawaimarisha ninyi mpaka mwisho mpate kuonekana bila hatia Siku ile ya Bwana wetu Yesu Kristo.
天主必要堅定你們到底,使你們在我們的主耶穌基督的日子上,無瑕可指。
9 Mungu ni mwaminifu; yeye aliwaita ninyi muwe na umoja na Mwanae Yesu Kristo Bwana wetu.
天主是忠信的,你們原是由祂所召,為同祂的聖子,我們的主耶穌基督,合而為一。
10 Ndugu, ninawasihi kwa jina la Bwana wetu Yesu Kristo: pataneni nyote katika kila jambo msemalo; yasiweko mafarakano kati yenu; muwe na fikira moja na nia moja.
弟兄們,我因我們的主耶穌基督之名,求你們眾人言談一致,在你們中間不要有分裂,但要同心合意,全然相合。
11 Ndugu zangu, habari nilizopata kutoka kwa watu kadhaa wa jamaa ya Kloe, zaonyesha wazi kwamba kuna kutoelewana kati yenu.
因為,我的弟兄們,我由黑羅厄的家人聽說你們中發生了紛爭。
12 Nataka kusema hivi: kila mmoja anasema chake: mmoja husema, “Mimi ni wa Paulo,” mwingine: “Mimi ni wa Apolo,” mwingine: “Mimi ni wa Kefa,” na mwingine: “Mimi ni wa Kristo,”.
我的意思是說,你們各自分稱:我是屬保祿的,我是屬阿頗羅的,我是屬刻法的,我是屬基督的。
13 Je, Kristo amegawanyika? Je, Paulo ndiye aliyesulubiwa kwa ajili yenu? Au je, mlibatizwa kwa jina la Paulo?
基督被分裂了嗎?難道保祿為你們被釘死在十字架上嗎?或者你們受洗是屬於保祿名下嗎?
14 Namshukuru Mungu kwamba sikumbatiza mtu yeyote miongoni mwenu isipokuwa tu Krispo na Gayo.
我感謝天主,除了克黎斯頗和加約外,我沒有給你們中的任何人付過洗,
15 Kwa hiyo hakuna awezaye kusema amebatizwa kwa jina langu.
免得有人說:你們受洗是歸我的名下。
16 (Samahani, nilibatiza pia jamaa ya Stefana; lakini zaidi ya hawa, sidhani kama nilimbatiza mtu mwingine yeyote.)
我還給斯特法納一家付過洗;此外我就不記得還給誰付過洗了。
17 Kristo hakunituma kubatiza, bali kuhubiri Habari Njema; tena, niihubiri bila kutegemea maarifa ya hotuba za watu kusudi nguvu ya kifo cha Kristo msalabani isibatilishwe.
原來基督派遺我,不是為施洗,而是為宣傳福音,且不用巧妙的言辭,免得基督十字架失去效力。
18 Maana ujumbe kuhusu kifo cha Kristo msalabani ni jambo la kipumbavu kwa wale walio katika mkumbo wa kupotea, lakini kwetu sisi tulio katika njia ya wokovu ujumbe huo ni nguvu ya Mungu.
原來十字架的道理,為喪亡的人是愚妄,為我們得救的人,卻是天主的德能,
19 Maana Maandiko Matakatifu yasema: “Nitaiharibu hekima yao wenye hekima, na elimu ya wataalamu nitaitupilia mbali.”
因為經上記載:『我要摧毀智者的智慧,廢除賢者的聰明。
20 Yu wapi basi, mwenye hekima? Yu wapi basi, mwalimu wa Sheria? Naye bingwa wa mabishano wa nyakati hizi yuko wapi? Mungu ameifanya hekima ya ulimwengu kuwa upumbavu. (aiōn g165)
智者在哪裡?天主豈不是使這世上的智慧變成妄嗎? (aiōn g165)
21 Maana, kadiri ya hekima ya Mungu, watu hawawezi kumjua Mungu kwa njia ya hekima yao wenyewe. Badala yake, Mungu amependa kuwaokoa wale wanaoamini kwa njia ya kile ambacho wenye hekima wanakiona kuwa ni upumbavu, yaani ujumbe tunaohubiri.
因為世人沒有憑自己的智慧,認識天主,天主遂以自己的智慧,決意以愚妄的道理來拯救那些相信的人。
22 Wayahudi wanataka ishara, na Wagiriki wanatafuta hekima;
的確,猶太人要求的是神蹟,希臘人尋求的智慧,
23 lakini sisi tunamhubiri Kristo aliyesulubiwa. Kwa Wayahudi jambo hili ni kikwazo, na kwa watu wa mataifa ni upumbavu;
這為猶太人固然是絆腳石,為外邦人是愚妄,
24 lakini kwa wale walioitwa, Wayahudi kwa Wagiriki, Kristo ni nguvu ya Mungu na hekima ya Mungu.
但為那些蒙召的,不拘是猶太人或希臘人,基督卻是天主的德能和天主的智慧:
25 Maana kinachoonekana kuwa ni upumbavu wa Mungu, kina busara zaidi kuliko hekima ya binadamu; na kinachoonekana kuwa ni udhaifu wa Mungu, kina nguvu zaidi kuliko nguvu za binadamu.
因為天主的愚妄總比人門智,天主的懦弱也總比人強。
26 Ndugu, kumbukeni wakati mlipoitwa: wengi wenu hawakuwa wenye hekima hata kwa fikira za binadamu; wengi hawakuwa wenye nguvu au watu wa tabaka ya juu.
弟兄們!你們看看你們是怎麼蒙召的:按肉眼看,你們人聰明的人並不多,有權勢的人也不多,顯貴的人也不多;
27 Ndiyo kusema, Mungu aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni upumbavu, ili awaaibishe wenye hekima; na aliyachagua yale ambayo ulimwengu huyaona ni dhaifu, ili awaaibishe wenye nguvu.
天主偏召了世上愚妄的,為羞辱那智慧的;召選了世上懦弱的,為羞那堅強的;
28 Mungu ameyachagua yale ambayo kwa fikira za dunia ni mambo yaliyo duni na yanayodharauliwa, mambo ambayo hata hayakuwako, ili kwa hayo ayafutilie mbali yale ambayo kwa fikira za binadamu ni mambo ya maana.
甚而天主召選了世上卑賤的和受人輕視的,以及那些一無所有的,
29 Basi, hakuna mtu awezaye kujivunia chochote mbele ya Mungu.
為使一切有血肉的人,在天主前無所誇耀。
30 Mungu mwenyewe ndiye aliyewaunganisha ninyi na Kristo Yesu. Mungu amemfanya Kristo awe hekima yetu; kwa njia yake sisi tunapatanishwa na Mungu, tunakuwa watu wake Mungu na kukombolewa.
你們得以結合於基督耶穌內,全是由於天主,也是由於天主,基督成了我們的智慧,正義,聖化者和救贖者,
31 Basi, kama yasemavyo Maandiko Matakatifu: “Mwenye kutaka kujivuna, basi, na ajivunie kazi ya Bwana.”
正如經上所記載的:『凡要誇耀的,應因主而誇耀。』

< 1 Wakorintho 1 >