< 2 Wakorintho 5 >

1 Maana tunajua kwamba hema hii ambayo ndani yake tunaishi sasa hapa duniani, yaani mwili wetu, itakapong'olewa, Mungu atatupa makao mengine mbinguni, nyumba ya milele isiyotengenezwa kwa mikono. (aiōnios g166)
因為我們知道:如果我們這地上帳棚式的寓所拆毀了,我們必由天主獲得一所房舍,一所非人手所造,而永遠在天上的寓所。 (aiōnios g166)
2 Na sasa, katika hali hii, tunaugua, tukitazamia kwa hamu kubwa kuvikwa makao yetu yaliyo mbinguni.
誠然,我們在此嘆息,因為我們切望套上那屬天上的住所,
3 Naam, tunapaswa kuvikwa namna hiyo ili tusije tukasimama mbele ya Mungu bila vazi.
只要我們還穿衣服,不是赤裸的。
4 Tukiwa bado katika hema hii ya duniani, tunalia kwa kukandamizwa; si kwamba tunataka kuuvua mwili huu wa kufa, ila tuna hamu ya kuvalishwa ule usiokufa, ili kile chenye kufa kimezwe kabisa na uhai.
我們在這帳棚裏的人,苦惱嘆息,是由於我們不願脫去衣服,而就套上另一層,為使這有死的為生命所吸收。
5 Mungu mwenyewe alitutayarishia mabadiliko hayo, naye ametupa Roho wake awe dhamana ya yote aliyotuwekea.
但那安排我們如此的,是天主,是衪給我們賜下了聖神作抵押。
6 Tuko imara daima. Tunajua kwamba kuishi katika mwili huu tu ni kukaa mbali na Bwana.
所以不論怎樣,我們時常放心大膽,因為我們知道,我們幾時住在這肉身內,就是與主遠離,──
7 Maana tunaishi kwa imani, na si kwa kuona.
因為我們現今只是憑信德往來,並非憑目睹──
8 Lakini tuko imara na tungependelea hata kuyahama makao haya, tukahamie kwa Bwana.
我們我們放心大膽,是為更情願出離肉身,與主同往。
9 Lakini jambo la maana zaidi, tunataka kumpendeza, iwe tunaishi hapa duniani au huko.
為此,我們或住在或出離肉身,常專心以討主的喜悅為光榮。
10 Maana sote ni lazima tusimame mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo, ili kila mmoja apokee anayostahili kwa matendo aliyoyafanya wakati alipokuwa anaishi duniani, mema au mabaya.
因為我們眾人都應出現在基督的審判台前,為使各人藉著他肉身所行的,或善或惡,領取相當的報應。
11 Basi, sisi tunajua umuhimu wa kumcha Bwana, na hivyo tunajitahidi kuwavuta watu. Mungu anatujua waziwazi, nami natumaini kwamba nanyi pia mnatujua kinaganaga.
我們既然知道主的可畏,遂盡力使人相信我們;我們在主前是顯明的,我也盻望在你們的良心前也是顯明的。
12 Si kwamba tunajaribu tena kujipendekeza kwenu, ila tunataka kuwapa ninyi sababu zetu za kuona fahari juu yenu, ili mpate kuwajibu wale wanaojivunia hali yao ya nje zaidi kuliko jinsi walivyo moyoni.
這並不是我們又向你們舉薦自己,而是為給你們一個有為我們誇耀的機會,使你們有以對付那些只憑外貌,而不憑內心誇耀的人們,
13 Ikiwa tumeonekana kuwa wendawazimu, hiyo ni kwa ajili ya Mungu; na ikiwa tunazo akili zetu timamu, hiyo ni kwa faida yenu.
因為如果說我們是發狂,那是為了天主;如果說我們是清醒,那是為了你們。
14 Maana mapendo ya Kristo yanatumiliki sisi ambao tunatambua ya kwamba mtu mmoja tu amekufa kwa ajili ya wote, na hiyo ina maana kwamba wote wanashiriki kifo chake.
因為基督的愛催迫著我們,因我們曾如此斷定:既然一個人替眾人死了;
15 Alikufa kwa ajili ya watu wote, ili wanaoishi wasiishi kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili yake yeye aliyekufa, akafufuliwa kwa ajili yao.
衪替眾人死,是為活著的人不再為自己生活,而是為替他們死而復活了的那位生活。
16 Basi, tangu sasa, sisi hatumpimi mtu yeyote kibinadamu. Hata kama kwa wakati mmoja tulimpima Kristo kibinadamu, sasa si hivyo tena.
所以我們從今以後,不再按人的看法認識誰了;縱使我們曾按人的看法認識過基督,但如今不再這樣認識衪了。
17 Mtu yeyote akiungana na Kristo huwa kiumbe kipya, mambo ya kale yamepita, hali mpya imefika.
所以誰苦在基督內,他就是一個新受造物,舊的已成過去,看,都成了新的。
18 Yote ni kazi ya Mungu mwenye kutupatanisha sisi naye kwa njia ya Kristo, akatupa nasi jukumu la kuwapatanisha watu naye.
這一切都是出由天主,衪曾藉基督使我們與衪自己和好,並將這和和的職務賜給了我們:
19 Ndiyo kusema: Mungu, amekuwa akiupatanisha ulimwengu naye kwa njia ya Kristo, bila kutia maanani dhambi zao binadamu. Yeye ametupa ujumbe kuhusu kuwapatanisha watu naye.
這這是說:天主在基督內使世界與自己和好,不再追他們的過犯,且將和好的話放在我們的口中。
20 Basi, sisi tunamwakilisha Kristo, naye Mungu mwenyewe anatutumia sisi kuwasihi ninyi. Tunawaombeni kwa niaba ya Kristo, mpatanishwe na Mungu.
所以我們是代表基督作大使了,好像是天主與著我們來勸勉世人。我們如今代基督請你們:與天主和好罷!
21 Kristo hakuwa na dhambi, lakini Mungu alimfanya ahusike na dhambi kwa ajili yetu, ili sisi kwa kuungana naye, tupate kuushiriki uadilifu wake Mungu.
因為衪錔使那不認識罪的,替我們成了罪,好叫我們在衪內成為天主的正義。

< 2 Wakorintho 5 >