< 2 Wakorintho 2 >
1 Basi nimeamua nisiwatembelee tena kuwatia huzuni.
I decided that I would not visit you again in grief;
2 Maana nikiwahuzunisha ninyi, basi, ni nani atakayenifariji? Ni walewale niliowahuzunisha!
for if I cause you grief, who is there to cause me joy except those whom I have grieved?
3 Ndiyo maana niliwaandikia—sikutaka kuja kwenu na kuhuzunishwa na ninyi ambao ndio mngepaswa kuwa furaha yangu. Nina hakika kwamba, mimi nikifurahi, ninyi nyote pia mnafurahi.
And for this very reason I wrote you, that I might not come only to be grieved by those who ought to give me joy; and because I trusted in you all, that my joy is the joy of all of you.
4 Nilipowaandikia hapo awali katika hali ya huzuni na sikitiko moyoni na kwa machozi mengi, haikuwa kwa ajili ya kuwahuzunisha ninyi, bali kwa ajili ya kuwaonyesheni kwamba nawapenda mno.
For I wrote to you out of much affliction and anguish of heart, through many tears; not to pain you, but to convince you of my love, my abundant love for you.
5 Ikiwa kuna mtu aliyemhuzunisha mwingine, hakunihuzunisha mimi—ila amewahuzunisha ninyi nyote, na sipendi kuwa mkali zaidi.
As to him who has been, and now is, causing pain, it is not I whom he has pained, but all of you - at least some of you (not to overstate the case).
6 Adhabu aliyokwisha pata kutoka kwa wengi wenu inamtosha.
Sufficient for the offender is the punishment imposed by the majority;
7 Iliyobakia ni afadhali kwenu kumsamehe mtu huyo na kumpa moyo ili asije akahuzunika mno na kukata tamaa kabisa.
so that now you ought rather to forgive and comfort him, lest he should be overwhelmed by the excess of his grief.
8 Kwa hiyo nawasihi: mwonyesheni kwamba mnampenda.
So I beg you to reinstate him in your love.
9 Madhumuni yangu kuandika ile barua yalikuwa kutaka kujua kama mko tayari kutii katika kila jambo.
For this very purpose also I wrote you (before), that I might test you, to see if you were obedient in every respect.
10 Mkimsamehe mtu, nami pia ninamsamehe. Maana ninaposamehe—kama kweli ninacho cha kusamehe—nasamehe mbele ya Kristo kwa ajili yenu,
If you forgive the man, I forgive him, too; for whatever I have forgiven has been forgiven in the presence of Christ,
11 ili tusimpe nafasi Shetani atudanganye; maana twaijua mipango yake ilivyo.
for your sakes, that I may not be overreached by Satan, for I am not ignorant of his devices.
12 Nilipofika Troa kuhubiri Habari Njema ya Kristo, nilikuta mlango u wazi kwa ajili ya kazi ya Bwana.
Now when I came to Troas to preach the gospel of Christ, although a door was opened to me in the Lord,
13 Lakini nilifadhaika sana kwa kutomkuta ndugu yetu Tito. Ndiyo maana niliwaaga wote pale nikaenda Makedonia.
I could get no peace of mind because I failed to find Titus, my brother. So I bade them good-bye and started off for Macedonia.
14 Lakini, shukrani kwa Mungu anayetuongoza daima katika msafara wa ushindi wa Kristo. Yeye hutufanya tuueneze ukweli wa Kristo kama harufu nzuri, kila mahali.
But thanks be to God, who in every place is leading me in the train of Christ’s triumph, and is making manifest through me the knowledge of him, an odor of incense everywhere.
15 Maana sisi ni kama harufu nzuri ya ubani ambayo Kristo anamtolea Mungu, harufu nzuri inayofikia wote wanaookolewa na wanaopotea.
I am Christ’s fragrance upwafted unto God, among those who are being saved and those who are perishing;
16 Kwa wale wanaopotea, harufu hiyo ni kifo; lakini kwa wale wanaookolewa, harufu hiyo ni uhai. Nani basi, awezaye kushiriki katika kazi ya namna hiyo?
to these latter an odor of death to death, to the former, of life to life. For such service as this, who is sufficient?
17 Sisi si kama wengine ambao hufanya biashara na ujumbe wa Mungu; sisi tunahubiri kwa unyofu mbele ya Mungu, kama watu tuliotumwa na Mungu, tukiwa tumeungana na Kristo.
I am; for I am not like most, trafficking in the word of God, but rather from a sincere heart, like a man of God, I speak in Christ, in the very presence of God.