< Tito 3 >

1 Uwakumbushe kuwanyenyekea viongozi na mamlaka, kuwatii na kuwa tayari katika kila kazi njema.
Put them in mind to be subject to principalities and authorities, to obey rulers, to be ready for every good work,
2 Wakumbushe kutokumtendea mtu yeyote ubaya, waepuke majibizano, wawape nafasi watu wengine katika kufanya maamuzi, na kuonesha unyenyekevu kwa watu wote.
to revile no one, not to be contentious, but gentle, showing all meekness to all men.
3 Kwa kuwa sisi pia tulikuwa na mawazo potofu na wakaidi. Tulikuwa upotevuni na tulifanywa watumwa kwa tamaa nyingi na starehe. Tuliishi katika wivu na uovu. Tulichukiza na kuchukiana.
For we ourselves also were formerly foolish, disobedient, deceived, serving various desires and pleasures, living in malice and envy, hateful, and hating one another.
4 Lakini wakati huruma ya Mungu mwokozi wetu na upendo wake kwa wanadamu ulipoonekana,
But when the kindness and philanthropy of God our Savior appeared, he saved us,
5 haikuwa kwa matendo yetu ya haki tuliyofanya, bali alituokoa kwa neema yake. Alituokoa kwa kutuosha kwa kuzaliwa upya na katika kufanywa upya kwa Roho Mtakatifu.
not by works of righteousness which we had done, but according to his own mercy, by the washing of regeneration, and renewing of the Holy Spirit,
6 Mungu alimwaga Roho Mtakatifu kwa wingi juu yetu kupitia Yesu Kristo mwokozi wetu.
which he poured out on us richly, through Jesus Christ our Savior;
7 Alifanya hivi ili kwamba, tukiwa tumehesabiwa haki kwa neema yake, tuwe washirika katika uhakika wa maisha ya milele. (aiōnios g166)
that, being justified by his grace, we might become heirs according to the hope of eternal life. (aiōnios g166)
8 Huu ni ujumbe wa kuaminika. Ninawataka myanene kwa ujasiri mambo haya, ili kwamba wale wanaomwamini Mungu wawe na dhamira juu ya kazi nzuri ambayo aliiweka mbele yao. Mambo haya ni mazuri na yanafaida kwa ajili ya watu wote.
This saying is true, and in respect to these things, I will that you affirm strongly, in order that those who have believed in God may be careful to practice good works: these are the things that are honorable and profitable for men.
9 Lakini jiepusheni na mijadala ya kipumbavu, nasaba, mashindano, na migongano kuhusu sheria. Mambo hayo hayana maana wala faida.
But foolish questions and genealogies and strifes and contentions about the law, avoid; for they are unprofitable and vain.
10 Mkataeni yeyote anayesababisha migawanyiko kati yenu. Baada ya onyo moja ama mawili,
A man that is a sectary, reject, after the first and second admonition,
11 jueni kwamba mtu wa jinsi hiyo ameiacha njia iliyo sahihi na anatenda dhambi na kujihukumu mwenyewe.
knowing that such a one is perverted, and sins, being self-condemned.
12 Nitakapomtuma kwako Artemi au Tikiko, harakisha uje kwangu huku Nikopoli ambapo nimeamua kukaa kipindi cha baridi.
When I send Artemas to you, or Tychicus, hasten to come to me at Nicopolis; for I have determined to spend the winter there.
13 Harakisha na umtume Zena mtaalamu katika sheria, na Apolo, pasipo kupungukiwa na kitu.
Conduct Zenas the lawyer, and Apollos on their journey with care, that nothing may be wanting to them.
14 Watu wetu lazima wajifunze kujishughulisha katika kazi nzuri ambazo zinagusa mahitaji muhimu ili kwamba wasije wakawa wasiozaa matunda.
Let our people also learn to practice good works for necessary uses, that they may not be unfruitful.
15 Wote walio pamoja nami wanakusalimu. Wasalimu wale watupendao katika imani. Neema iwe nanyi nyote.
All that are with me salute you. Salute those who love us in faithfulness. Grace be with you all. Amen.

< Tito 3 >