< Wahebrania 5 >

1 Kwani kila kuhani mkuu, aliyechaguliwa kutoka miongoni mwa watu, amechaguliwa kusimama badala yao katika vitu vinavyohusiana na Mungu, ili aweze kutoa kwa pamoja zawadi na dhabihu kwa ajili ya dhambi.
For every high priest chosen from among men, is appointed for men, in things pertaining to God, that he may offer gifts and sacrifices for sins:
2 Anaweza kujishughulisha kwa upole na wajinga na wabishi kwa kuwa yeye mwenyewe pia amezungukwa na udhaifu.
being able to have compassion on the ignorant and erring, because he himself is beset with infirmity:
3 Kwa sababu ya hili, ana wajibu wa kutoa sadaka kwa ajili ya dhambi zake kama afanyavyo kwa dhambi za watu.
and on account of this, he ought, as for the people, so also for himself, to make offering for sins.
4 Na hakuna mtu achukuaye heshima hii kwa ajili yake mwenyewe, lakini badala yake, lazima aitwe na Mungu, kama alivyokuwa Haruni.
And no one takes this honor to himself, but he that is called by God, as Aaron also was called.
5 Hata Kristo hakujipa heshimu mwenyewe kwa kujifanya mwenyewe kuwa kuhani mkuu. Badala yake, Mungu alisema kwake, “Wewe ni mwanangu, leo nimekuwa Baba yako.”
So, also, the Christ did not take upon himself the honor of becoming a high priest: but he gave him this honor, who said to him, Thou art my Son, this day have I begotten thee:
6 Ni kama asemavyo pia sehemu nyingine, “Wewe ni kuhani milele baada ya mfumo wa Melkizedeki.” (aiōn g165)
as he says also in another place, Thou art a priest forever, after the order of Melchisedec. (aiōn g165)
7 Wakati wa kipindi chake katika mwili, aliomba na kuombea, alimwomba Mungu kwa machozi, kwa yeye awezaye kumwokoa kutoka kwenye kifo. Kwa sababu ya unyenyekevu wake kwa Mungu, alisikiwa.
In the days of his flesh, having offered up prayers and supplications, with strong crying and tears, to him that was able to save him from death, and having been heard with respect to that which he feared,
8 Ijapokuwa alikua mwana, alijifunza kutii kwa mambo yaliyomtesa.
although he was a Son, he yet learned obedience from the things which he suffered;
9 Alikamilishwa na kwa njia hii alifanyika kwa kila mtu amwaminiye kuwa sababu ya wokovu wa milele, (aiōnios g166)
and, having been made perfect, he became the author of eternal salvation to all that obey him, (aiōnios g166)
10 kwa kutengwa na Mungu kama kuhani Mkuu baada ya zamu ya Melkizedeki.
being called by God a high priest after the order of Melchisedec.
11 Tuna mengi ya kusema kuhusu Yesu, lakini ni vigumu kuwaelezea kwa kuwa ninyi ni wavivu wa kusikia.
Of him we have many things to say, and difficult to be explained, if we do say them, since you are slow in understanding.
12 Ijapokuwa kwa kipindi hiki mlipaswa kuwa walimu, bado kuna umuhimu wa mtu kuwafundisha mafundisho ya awali ya kanuni za neno la Mungu. Mnahitaji maziwa na si chakula kigumu.
For though you ought to be teachers, considering the time, yet you have need that some one teach you again what are the first elements of the oracles of God; and you have become such as have need of milk, and not of strong food.
13 Kwa kuwa yeyote anywaye maziwa tu hana uzoefu katika ujumbe wa haki, kwa kuwa bado ni mtoto.
For every one that partakes of milk is unskillful in the word of righteousness: for he is a babe.
14 Kwa upande mwingine, chakula kigumu ni cha watu wazima, wale ambao kwa sababu ya uzoefu wao katika kutofautisha haki na ubaya wamefundishwa kutambua jema na ovu.
But strong food belongs to those who are of mature age, who, by use, have their internal senses exercised to the discerning of both good and evil.

< Wahebrania 5 >