< Wahebrania 6 >
1 Kwa hiyo, tukiacha tulichojifunza kwanza kuhusu ujumbe wa Kristo, twapaswa kuwa na juhudi kuelekea kwenye ukomavu, tusiweke tena misingi ya toba kutoka katika kazi zisizo na uhai na imani katika Mungu,
Therefore, omitting the elementary Christian teaching, let us go on to the perfection of Christian instruction, not laying again the foundation of repentance from dead works, and of faith toward God,
2 wala misingi ya mafundisho ya ubatizo, na kuwawekea mikono, ufufuo wa wafu, na hukumu ya milele. (aiōnios )
of the teaching with respect to immersions, and of the laying on of hands, of the resurrection of the dead, and of eternal condemnation. (aiōnios )
3 Na tutafanya hivi ikiwa Mungu ataruhusu.
And this we will do, if God permit.
4 Kwa kuwa haiwezekani kwa wale ambao waliipata nuru awali, ambao walionja kipawa cha mbinguni, na kufanywa kuwa washirika wa Roho Mtakatifu,
For it is impossible to renew again to repentance those who have once been enlightened, and have tasted of the heavenly gift, and have been made partakers of the Holy Spirit,
5 na ambao walionja uzuri wa neno la Mungu na kwa nguvu za wakati ujao, (aiōn )
and have tasted the good word of God, and the powers of the coming age, (aiōn )
6 na kisha wakaanguka - haiwezekani kuwarejesha tena katika toba. Hii ni kwa sababu wamemsulubisha Mwana wa Mungu mara ya pili kwa nafsi zao, wakimfanya kuwa chombo cha dhihaka hadharani.
if they fall away; since they again crucify in themselves the Son of God, and put him to an open shame.
7 Kwa kuwa ardhi iliyopokea mvua inyeshayo mara kwa mara juu yake, na ikatoa mazao muhimu kwa hao waliofanya kazi katika ardhi, hupokea baraka kutoka kwa Mungu.
For the land which drinks up the rain that comes often upon it, and produces herbs suitable for those for whom it is cultivated, receives blessing from God.
8 Lakini ikiwa huzaa miiba na magugu, haina tena thamani na ipo katika hatari ya kulaaniwa. Mwisho wake ni kuteketezwa.
But that which produces thorns and thistles is rejected, and is near the curse, the end of which is to be burned.
9 Ijapokuwa tunazungumza hivi, rafiki wapenzi, tunashawishiwa na mambo mazuri yawahusuyo ninyi na mambo yahusuyo wokovu.
But, beloved, we are confident of better things concerning you, and of things that tend to salvation, though we thus speak.
10 Kwa kuwa Mungu si dhalimu hata asahau kazi yenu na kwa upendo mliouonesha kwa ajili ya jina lake, katika hili mliwatumikia waamini na bado mngali mnawatumikia.
For God is not unjust, that he should forget your work, and the love which you have shown for his name by having ministered to the saints, and by continuing to minister.
11 Na tunatamani sana kwamba kila mmoja wenu aweze kuonesha bidii ile ile mpaka mwisho kwa uhakika wa ujasiri.
But we desire every one of you to show the same diligence, in order to have your hope fully assured to the end:
12 Hatutaki muwe wavivu, lakini muwe wafuasi wa wale warithio ahadi kwa sababu ya imani na uvumilivu.
that you may not become slothful, but imitators of those who, through faith and patience, inherit the promises.
13 Kwa maana Mungu alipompa Abrahamu ahadi, aliapa kwa nafsi yake, kwa kuwa asingeliapa kwa mwingine yeyote aliye mkubwa kuliko yeye.
For when God made promise to Abraham, because he could swear by no greater, he swore by himself,
14 Alisema, “Hakika nitakubariki, na nitauongeza uzao wako zaidi.”
saying: Most surely will I abundantly bless you, and abundantly multiply you.
15 Kwa njia hii, Abrahamu alipokea kile alichoahidiwa baada ya kusubiria kwa uvumilivu.
And so, when he had waited patiently, he received the promises.
16 Maana wanadamu huapa kwa yeye aliye mkuu kuliko wao, na kwao ukomo wa mashindano yote ni kiapo kwa kuyathibitisha.
For, verily, men swear by the greater, and an oath for confirmation is to them an end of all contradiction.
17 Wakati Mungu alipoamua kuonesha kwa uwazi zaidi kwa warithi wa ahadi kusudi lake zuri lisilobadilika, alilithibitisha kwa kiapo.
Wherefore, God, being more abundantly willing to show to the heirs of his promise the immutability of his purpose, interposed an oath,
18 Alifanya hivyo ili kwa vitu viwili visivyoweza kubadilika, ambavyo katika hivyo Mungu hawezi kusema uongo, sisi tulioikimbilia hifadhi tupate kutiwa moyo kushikilia kwa nguvu tumaini lililowekwa mbele yetu.
that by two immutable things, in which it was impossible for God to lie, we might have strong consolation, who have fled to lay hold on the hope set before us;
19 Tunao ujasiri huu kama nanga imara na ya kutegemea ya roho zetu, ujasiri ambao unaingia sehemu ya ndani nyuma ya pazia.
which, hope we have as an anchor for the soul, both sure and steadfast, and which enters in beyond the vail,
20 Yesu aliingia sehemu ile kama mtangulizi wetu, akisha kufanyika kuhani mkuu hata milele baada ya utaratibu wa Melkizedeki. (aiōn )
whither a forerunner for us has gone, even Jesus, who is made a high priest forever after the order of Melchisedec. (aiōn )