< Warumi 12 >

1 Kwa hiyo nawasihi, ndugu, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, inayokubalika kwa Mungu. Hii ndiyo ibada yenu yenye maana.
Wherefore, brethren, I beseech you, by the tender mercies of God, that you present your bodies a living sacrifice, holy, acceptable to God, which is your reasonable service.
2 Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu. Fanyeni hivi mpate kujua mapenzi ya Mungu yaliyo mema, yakumpendeza na kamilifu. (aiōn g165)
And be not conformed to this world, but be transformed by the renewal of your mind; that you may approve the will of God, which is good, and acceptable, and perfect. (aiōn g165)
3 Kwa maana nasema, kwa sababu ya neema niliyopewa, kwamba kila mtu ambaye yupo miongoni mwenu hapaswi kufikiri zaidi juu yake mwenyewe kuliko inavyompasa kufikiri. Bali, imempasa kufikiri kwa hekima, kama ambavyo Mungu amewapa kila mmoja kiasi fulani cha imani.
Also, by the favor which is given to me, I charge every one of you not to think more highly of himself than he ought to think; but to think modestly, as God has distributed to every one a portion of his faith.
4 Kwa kuwa tuna viungo vingi katika mwili mmoja, lakini si viungo vyote vina kazi moja.
For, as in one body we have many members, but all the members have not the same office;
5 Vivyo hivyo, sisi tulio wengi tu mwili mmoja katika Kristo, na viungo kila mmoja kwa mwenzake.
so we, the many, are one body under Christ, and individually members of one another.
6 Tuna karama zilizo mbalimbali kwa kadiri ya neema mliyopewa. Ikiwa karama ya mtu ni unabii, na itendeke kwa kadiri ya imani yake.
Having, then, gifts, differing according to the favor which is given to us--if prophecy act according to the measure of faith--
7 Ikiwa karama ya mtu ni huduma, na atumike. Ikiwa mwingine ana karama ya kufundisha, basi, afundishe.
if a ministerial office, in that office--if one is a teacher, in teaching--
8 Ikiwa karama ya mtu ni faraja, basi, afariji. Ikiwa karama ya mtu ni kutoa, afanye hivyo kwa ukarimu. Ikiwa karama ya mtu ni kuongoza, na litendeke kwa uangalifu. Ikiwa karama ya mtu ni katika kuonesha huruma, na litendeke kwa furaha.
and the exhorter, in exhortation. Let him who distributes act with disinterestedness--him that presides, with assiduity--him that shows mercy, with cheerfulness.
9 Pendo lisiwe na unafiki. Chukieni uovu; mshikilie yaliyo mema.
Let love be without hypocrisy. Abhor the evil--adhere closely to the good.
10 Kuhusu upendo wa ndugu, pendaneni ninyi kwa ninyi. Kuhusu heshima, heshimianeni ninyi kwa ninyi.
In brotherly love, be tenderly affectionate to one another--in honor, prefer one another.
11 Kuhusu bidii, msiwe walegevu. Kuhusu roho, iweni na shauku. Kuhusu Bwana, mtumikieni.
In business, be not slothful. Be fervent in spirit-- constant in serving the Lord.
12 Furahini katika ujasiri mlionao kuhusu siku zijazo. Muwe na subira katika matatizo yenu. Mdumu katika kuomba.
Be joyful in hope, patient in affliction, steadfastly persevering in prayer.
13 Mshiriki katika mahitaji ya waumini. Tafuteni njia nyingi za kuonesha ukarimu.
Communicate to the necessities of the saints. Follow hospitality to strangers.
14 Watakieni baraka wote wanaowatesa ninyi; muwabariki na wala msiwalaani.
Bless them who persecute you--bless, and curse not.
15 Furahini pamoja na wanaofurahi, lieni pamoja na wanaolia.
Rejoice with them who rejoice, and weep with them who weep.
16 Muwe na nia moja ninyi kwa ninyi. Msifikiri kwa kujivuna, lakini wakubalini watu wa hali ya chini. Msiwe na hekima juu ya mawazo yenu wenyewe.
Be of the same disposition toward one another. Do not care for high things; but accommodate yourselves to those which are humble. Be not wise in your own conceits.
17 Msimlipe mtu yeyote ovu kwa ovu. Fanyeni mambo mema machoni pa watu wote.
To no one return evil for evil. Seek after things honorable in the sight of all men.
18 Kama inawezekana, kama ilivyowekwa kwenu, muwe na amani na watu wote.
What relates to you is, live in peace with all men, if possible.
19 Wapenzi, msijilipizie kisasi wenyewe, lakini ipisheni ghadhabu ya Mungu. Kwa maana imeandikwa, '' 'kisasi ni changu; Mimi nitalipa,' asema Bwana.”
Beloved, do not avenge yourselves, but give place to the wrath of God; for it is written, "Vengeance belongs to me; I will repay, says the Lord."
20 “Lakini ikiwa adui yako ana njaa, mlishe. Akiwa na kiu, mnyweshe. Kwa maana ukifanya hivyo, utampalia makaa ya moto juu ya kichwa chake.”
Therefore, if your enemy hunger, give him food: if he thirst, give him drink: for by doing this, you will heap coals of fire on his head.
21 Usishindwe na ubaya, bali ushinde ubaya kwa wema.
Be not overcome by evil, but overcome evil with good.

< Warumi 12 >