< Warumi 11 >
1 Basi nasema, je, Mungu aliwakataa watu wake? Hata kidogo. Kwa kuwa mimi pia ni Mwiisraeli, wa ukoo wa Abrahamu, wa kabila la Benyamini.
I say, then, has God cast off his people? By no means. For, even I am an Israelite, of the seed of Abraham, of the tribe of Benjamin.
2 Mungu hakuwakataa watu wake, aliowajua tangu mwanzo. Je hamjui andiko linasema nini kuhusu Eliya, jinsi alivyomsihi Mungu juu ya Israeli?
God has not cast off his people whom formerly he acknowledged. Do you not know, what the scripture says to Elijah; when he complains to God against Israel, saying,
3 “Bwana, wamewaua manabii wako, nao wamebomoa madhabahu zako. Mimi peke yangu nimesalia, nao wanatafuta uhai wangu.”
"Lord, they have killed thy prophets, and have digged down thy altars, and I am let alone, and they seek my life?"
4 Lakini jibu la Mungu lasema nini kwako? “Nimetunza kwa ajili yangu watu elfu saba ambao hawampigii magoti Baali.”
But what says the answer to God to him? "I have reserved to myself seven thousand men, who have not bowed the knee to Baal."
5 Hata hivyo, wakati huu wa sasa pia kuna walio salia kwa sababu ya uchaguzi wa neema.
So, then, even at this present time, there is a remnant according to an election by favor.
6 Lakini ikiwa ni kwa neema, si tena kwa matendo. Vinginevyo neema haitakuwa tena neema.
And if by favor, it is no more of works: otherwise favor is no more favor.
7 Ni nini basi? Jambo ambalo Israeli alikuwa akitafuta, hakukipata, bali wateule walikipata, na wengine walitiwa uzito.
What then? The thing Israel earnestly seeks, that he has not obtained. But the election has obtained it, and the rest are blinded.
8 Ni kama ilivyoandikwa: “Mungu amewapa roho ya ubutu, macho ili wasione, na masikio ili wasisikie, mpaka leo hii.”
As it is written, "God has given them a spirit of deep sleep; eyes not seeing, and ears not hearing, until this present day."
9 Naye Daudi anasema, “Acha meza zao na ziwe wavu, mtego, sehemu ya kujikwaa, na kulipiza kisasi dhidi yao.
And David says, "Let their table be for a snare, and a trap, and a stumbling block, and a recompense to them.
10 Acha macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona. Ukawainamishe migongo yao daima.”
Let their eyes be darkened, so as not to see; and let them bow down their back continually.
11 Basi nasema, “Je, wamejikwaa hata kuanguka?” Isiwe hivyo kamwe. Badala yake, kwa kushindwa kwao, wokovu umefika kwa Mataifa, ili wao wenyewe watiwe wivu.
I ask, then, have they stumbled, that they may fall? By no means. But, through their fall, salvation is given to the Gentiles, to excite them to emulation.
12 Sasa ikiwa kushindwa kwao ni utajiri wa ulimwengu, na kama hasara yao ni utajiri wa mataifa, ni kiasi gani zaidi itakuwa kukamilika kwao?
Now, if the fall of them be the riches of the world; and the diminishing of them the riches of the Gentiles; how much more their fullness?
13 Na sasa naongea nanyi watu wa Mataifa. Kwa kuwa nimekuwa mtume kwa watu wa Mataifa mengine, najivunia huduma yangu.
Now, I speak to you, Gentiles, (and inasmuch as I am the Apostle to the Gentiles, I do honor to my ministry, )
14 Labda nitawatia wivu walio mwili mmoja na mimi. Labda tutawaokoa baadhi yao.
if by any means I may excite to emulation my kindred, and may save some of them.
15 Maana ikiwa kukataliwa kwao ni maridhiano ya dunia, kupokelewa kwao kutakuwaje ila uhai toka kwa wafu?
For, if the casting away of them be the reconciling of the world; what will the receiving of them be, but life from the dead?
16 Kama matunda ya kwanza ni akiba, ndivyo ilivyo kwa donge la unga. Kama mzizi ni akiba, matawi nayo kadhalika.
Moreover, if the first fruit be holy, the mass is also holy; and if the root be holy, so are the branches.
17 Lakini kama baadhi ya matawi yamekatwa, kama wewe, tawi pori la mzeituni, ulipandikizwa kati yao, na kama ulishiriki pamoja nao katika mizizi ya utajiri wa mzeituni,
Now, if some of the branches were broken off, and you who are a wild olive, are ingrafted among them, and are become a joint partaker of the root and fatness of the olive;
18 usijisifu juu ya matawi. Lakini kama unajisifu, si wewe ambaye unaisaidia mizizi, bali mizizi inakusaidia wewe.
boast not against the branches: but if you boast, still, you bear not the root, but the root you.
19 Basi utasema, “Matawi yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika shina.”
You will say, however, The branches were broken off, that I might be grafted in.
20 Hiyo ni kweli. Kwa sababu ya kutoamini kwao walikatwa, lakini wewe ulisimama imara kwa sababu ya imani yako. Usijifikirie mwenyewe kwa hali ya juu sana, bali ogopa.
True: by unbelief they were broken off, and you by faith, stand. Be not high-minded, but fear.
21 Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, hatakuhurumia wewe pia.
For, if God spared not the natural branches; perhaps, neither will he spare you.
22 Angalia, basi, matendo mema na ukali wa Mungu. Kwa upande mmoja, ukali ulikuja juu ya Wayahudi ambao walianguka. Lakini kwa upande mwingine, wema wa Mungu huja juu yako, kama utadumu katika wema wake. Vinginevyo wewe pia utakatiliwa mbali.
Behold, then, the goodness and severity of God! Toward them who fell, severity: but toward you, goodness, if you continue in his goodness: otherwise, you also shall be cut off.
23 Na pia, kama hawataendelea katika kutoamini kwao, watapandikizwa tena. Maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena.
And even they, if they continued not in unbelief, shall be grafted in: for God is able to graft them in again.
24 Kwa maana ikiwa ninyi mlikatwa nje kwa ulio kwa asili mzeituni mwitu, na kinyume cha asili mlipandikizwa katika mzeituni ulio mwema, si zaidi sana hawa Wayahudi, ambao ni kama matawi ya asili kuweza kupandikizwa tena ndani ya mzeituni wao wenyewe?
For if you were cut off from the olive, by nature wild, and were contrary to nature, grafted into the good olive; how much rather shall those who are the natural branches, be grafted into their own olive?
25 Kwa maana ndugu sitaki msijue, kuhusiana na siri hii, ili kwamba msiwe na hekima katika kufikiri kwenu wenyewe. Siri hii ni kwamba ugumu umetokea katika Israeli, hadi kukamilika kwa mataifa kutakapokuja.
For, brethren, that you may not be, wise in your own conceits, I would not have you ignorant of this secret, that blindness, in part, has happened to Israel, till the fullness of the Gentiles come in.
26 Hivyo Israeli wote wataokoka, kama ilivyoandikwa: “Kutoka Sayuni atakuja Mkombozi. Atauondoa uovu kutoka kwa Yakobo.
And so all Israel shall be saved; as it is written, "The deliverer shall come out of Zion, and shall turn away ungodliness from Jacob.
27 Na hili litakuwa agano langu pamoja nao, wakati nitakapoziondoa dhambi zao.”
For this is my covenant with them, when I shall take away their sins."
28 Kwa upande mmoja kuhusu injili, wanachukiwa kwa sababu yenu. Kwa upande mwingine kutokana na uchaguzi wa Mungu, wamependwa kwa sababu ya mababu.
With respect to the gospel, indeed, they are enemies, on your account: but with respect to the election, they are beloved on account of the fathers.
29 Kwa kuwa zawadi na wito wa Mungu haubadiliki.
For the free gifts and calling of God are without repentance.
30 Kwa kuwa awali ninyi mlikuwa mmemwasi Mungu, lakini sasa mmeipokea rehema kwa sababu ya kuasi kwao.
Besides, as you, in times past, have disobeyed God, yet now have obtained mercy through their disobedience;
31 Kwa njia iyo hiyo, sasa hawa Wayahudi wameasi. Matokeo yake ni kwamba kutokana na huruma mliyojaliwa ninyi wanaweza pia kupokea rehema.
even so these, also, have no disobeyed, that through your mercy, they also may obtain mercy.
32 Maana Mungu amewafunga watu wote katika uasi, ili aweze kuwahurumia wote. (eleēsē )
For God has shut up together all for disobedience, that he might have mercy upon all. (eleēsē )
33 Jinsi zilivyo kuu utajiri na hekima na maarifa ya Mungu! Hazichunguziki hukumu zake, na njia zake hazigunduliki!
Oh that depth of the riches and of the wisdom and of the knowledge of God! How unsearchable are his judgments, and his ways past finding out!
34 “Maana ni nani aliyeijua nia ya Bwana? Au ni nani amekuwa mshauri wake?
For who has known the mind of the Lord? or who has been his counsellor?
35 Au ni nani kwanza aliyempa kitu Mungu, ili alipwe tena?”
or who has first given to him, and it shall be recompensed to him again?
36 Kwa maana kutoka kwake, na kwa njia yake na kwake, vitu vyote vipo. Kwake uwe utukufu milele. Amina. (aiōn )
For, from him, and by him, and to him, are all things: to him be the glory forever. Amen. (aiōn )