< Zaburi 91 >
1 Yeye aishiye katika makazi ya Aliye Juu atakaa katika uvuli wa mwenyezi.
居住在至高者護佑下的人,在全能者蔭庇下居住的人,
2 Nami nitasema kuhusu Yahwe, “Yeye ni kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu, ambaye niaamini katika yeye.”
請向上主說:我的避難所,我的碉堡,我的天主,我向您投靠。
3 Kwa maana yeye atakuokoa dhidi ya mtego wa mwindaji na dhidi ya pigo liletalo mauti.
祂必救您脫離獵人戶的縲絏,祂必救你脫免害人的瘟疫。
4 Yeye atakufunika kwa mbawa zake, na chini ya mbawa zake utapata kimbilio. Uaminifu wake ni ngao na ulinzi.
祂以自己的羽毛掩護你,叫你住祂的翼下逃避:祂的忠信是盾牌和鎧衣。
5 Nawe hautaogopeshwa na vitisho wakati wa usiku, wala mishale ipaayo kwa siku,
你不必怕黑夜驚人的顫慄,也不必怕白天亂飛的箭矢,
6 wala pigo lizungukalo gizani, wala ugonjwa ujao wakati wa mchana.
黑暗中行的瘟疫,正午毒害人的癘疾。
7 Maelfu waweza kuangukia upande wako na makumi elfu mkono wako wa kuume, lakini uovu hauwezi kukupata.
在你身旁雖倒斃一千,在你右邊雖跌仆一萬,疫疾卻不到你身邊。
8 Wewe utatazama tu na kuona hukumu ya waovu.
然而你親眼要觀臨,要見到惡人的報應。
9 Kwa kuwa Yahwe ni kimbilio langu! Umfanye Aliye Juu kuwa kimbilio lako pia.
你既知道上主是你的避難所,你就該以至高者為你的碉堡;
10 Hakuna uovu utakao kushinda wewe; mateso hayatakuja karibu na nyumba yako.
災殃不會走近你的身邊,禍患也不臨近你的帳幔。
11 Maana yeye atawaelekeza malaika moja kwa moja kukulinda wewe, na kukuwekea ulinzi katika njia zako zote.
上主必為你委派祂的天使,在你行走的每條路上保護您。
12 Nao watakuinua juu kwa mikono yao ili usiweze kujigonga mguu wako kwenye jiwe.
他們把你托在自己的手掌,不使你的腳在石頭上碰傷。
13 Utawaangamiza simba na nyoka chini ya miguu yako; utawakanyaga wana-simba na nyoka.
你可經過獅子和毒蛇身上,你可踐踏在猛獅和毒身上。
14 Kwa sababu amejitoa kwangu, nitamuokoa. Nitamlinda kwa sababu yeye ni mwaminifu kwangu.
上主說:因為他依戀我,我必拯救他,他承認我的名,我必保護他。
15 Aniitapo, nitamjibu. Katika shida nitakuwa naye; nitampatia ushindi na nitamuheshimu.
他若呼求我,我必應允,他若有困苦,我必與他同在,我必拯救他,光榮他。
16 Nitamtosheleza kwa maisha malefu na kumuonesha wokovu wangu.
我必要使他享壽,他必看到我的救援。