< Zaburi 77 >

1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
in finem pro Idithun psalmus Asaph voce mea ad Dominum clamavi voce mea ad Deum et intendit me
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
in die tribulationis meae Deum exquisivi manibus meis nocte contra eum et non sum deceptus rennuit consolari anima mea
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
memor fui Dei et delectatus sum exercitatus sum et defecit spiritus meus diapsalma
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
anticipaverunt vigilias oculi mei turbatus sum et non sum locutus
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
cogitavi dies antiquos et annos aeternos in mente habui
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
et meditatus sum nocte cum corde meo exercitabar et scobebam spiritum meum
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
numquid in aeternum proiciet Deus et non adponet ut conplacitior sit adhuc
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
aut in finem misericordiam suam abscidet a generatione in generationem
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
aut obliviscetur misereri Deus aut continebit in ira sua misericordias suas diapsalma
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
et dixi nunc coepi haec mutatio dexterae Excelsi
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
memor fui operum Domini quia memor ero ab initio mirabilium tuorum
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
et meditabor in omnibus operibus tuis et in adinventionibus tuis exercebor
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
Deus in sancto via tua quis deus magnus sicut Deus noster
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
tu es Deus qui facis mirabilia notam fecisti in populis virtutem tuam
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
redemisti in brachio tuo populum tuum filios Iacob et Ioseph diapsalma
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
viderunt te aquae Deus viderunt te aquae et timuerunt et turbatae sunt abyssi
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
multitudo sonitus aquarum vocem dederunt nubes etenim sagittae tuae transeunt
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
vox tonitrui tui in rota inluxerunt coruscationes tuae orbi terrae commota est et contremuit terra
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
in mari via tua et semitae tuae in aquis multis et vestigia tua non cognoscentur
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
deduxisti sicut oves populum tuum in manu Mosi et Aaron

< Zaburi 77 >