< Zaburi 76 >
1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
in finem in laudibus psalmus Asaph canticum ad Assyrium notus in Iudaea Deus in Israhel magnum nomen eius
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
et factus est in pace locus eius et habitatio eius in Sion
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
ibi confregit potentias arcuum scutum et gladium et bellum diapsalma
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
inluminas tu mirabiliter de montibus aeternis
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
turbati sunt omnes insipientes corde dormierunt somnum suum et nihil invenerunt omnes viri divitiarum manibus suis
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
ab increpatione tua Deus Iacob dormitaverunt qui ascenderunt equos
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
tu terribilis es et quis resistet tibi ex tunc ira tua
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
de caelo auditum fecisti iudicium terra timuit et quievit
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
cum exsurgeret in iudicium Deus ut salvos faceret omnes mansuetos terrae diapsalma
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
quoniam cogitatio hominis confitebitur tibi et reliquiae cogitationis diem festum agent tibi
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
vovete et reddite Domino Deo vestro omnes qui in circuitu eius adferent munera terribili
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
et ei qui aufert spiritus principum terribili apud reges terrae