< Zaburi 38 >

1 Yahwe, usinikemee katika hasira yako; usiniadhibu katika ghadhabu yako.
達味紀念歌。 上主,求你不要在你的震怒中責罰我,求你不要在你的氣憤中懲戒我。
2 Kwa kuwa mishale yako hunichoma, na mkono wako huniangusha chini.
因為你的箭射中了我,你的手重壓了我。
3 Mwili wangu wote unaumwa kwa sababu ya hasira yako; kwa sababu ya dhambi zangu mifupa yangu haina afya.
因了你的盛怒,我已體無完膚;因了我的罪行,我已粉身碎骨。
4 Kwa maana maovu yangu yamenielemea; yamekuwa mzigo mzito kwangu.
因為我的罪過高出我的頭頂,好似重擔把我壓得過分沉重。
5 Vidonda vyangu vimeoza na vinanuka kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
我的創痍漬爛流膿,完全由於我的愚矇。
6 Nimepindika na kuwa mnyonge kila siku; ninaenenda katika maombolezo siku zote.
我悲傷得身已傴僂,終日行動滿懷憂愁。
7 Kwa maana ndani yangu, ninaungua; hakuna afya katika mwili wangu.
因為我的腰肢焦灼難受,我的肉體已無完膚。
8 Nimedhohofika na kulemewa sana; ninaugua kwa sababu ya dhiki yangu.
我已筋疲力盡,奄奄一息;我已心痛欲絕,嗟嘆不已。
9 Bwana, wewe unaielewa shauku ya ndani kabisa ya moyo wangu, na kuugua kwangu hakujifichika kwako.
我主,我的呻吟常在你的面前,我的悲歎不向你隱瞞;
10 Moyo wangu unapwita pwita, nguvu zangu zinaniisha, macho yangu yanafifia.
我的心顫慄,我的精力衰退,我眼目的光明也已消逝。
11 Marafiki na ndugu zangu wamenitenga kwa sababu ya hali; majirani zangu hukaa mbali nami.
我遭難時,我的友朋都袖手旁觀,我的親人都站得很遠。
12 Wale wanaoutafuta uhai wangu hutega mitego kwa ajili yangu. Wao ambao hutafuta kunidhuru huongea maneno ya uharibifu na husema maneno ya uongo siku nzima.
追尋我命的人,張設網羅,設法害我的人,散布惡謨,他們行詭計日夜思索。
13 Lakini, niko kama mtu kiziwi na sisikii lolote; niko kama mtu bubu ambaye hasemi lolote.
但我好像是一個有耳聽不見的聾子,我又好像是一個有口不能言的啞巴。
14 Niko kama mtu asiye sikia na mbaye hawezi kujibu.
我竟成了一個沒有聽覺的人,成了一個口中沒有辯詞的人。
15 Hakika ninakungoja wewe, Yahwe; wewe utanijibu, Bwana Mungu wangu.
因為我唯有仰慕你,上主,你必應允我,我主我天主!
16 Ninasema hivi ili kwamba maadui zangu wasije wakafurahia juu yangu. Ikiwa mguu wangu utateleza, watanifanyia mambo mabaya.
我原來說過:「不要讓他們洋洋得意,不要讓他們因我的失足而沾沾自喜。」
17 Kwa kuwa niko karibu mashakani, na niko katika maumivu ya mara kwa mara.
我生來就易於失足,因此我常心懷痛苦。
18 Ninatubu makosa yangu; ninahuzunika kwa dhambi zangu.
我的確承認我犯了罪愆,我為了我的過惡而憂慚。
19 Lakini maadui zangu ni wengi; wale wanichukiao ni wengi.
無故加害我的人,力強兇暴,無理憎恨我的人,成群結伙;
20 Wao wananilipa mabaya kwa mema; wanavurumiza shutuma kwangu ingawa nimefuata lililo jema.
他們都以怨報德而對待我,因我追求正義而惱恨我。
21 Usinitelekeze, Yahwe, Mungu wangu, usikae mbali nami.
上主,求你不要捨棄我,我主,求你不要遠離我。
22 Njoo haraka unisaidie, Bwana, wokovu wangu.
我的上主,我的救助,求你速來給我護祐。

< Zaburi 38 >