< Zaburi 36 >
1 Dhambi hunena kama unabii katika moyo wa mwovu; machoni mwake hamna hofu ya Mungu.
For the end, by David the servant of the Lord. The transgressor, that he may sin, says within himself, [that] there is no fear of God before his eyes.
2 Kwa maana yeye hujifariji mwenyewe, akifikiria kuwa dhambi zake hazitagundulika na kuchukiwa.
For he has dealt craftily before him, to discover his iniquity and hate it.
3 Maneno yake ni yenye dhambi na udanganyifu; hataki kuwa mwenye hekima na kutenda mema.
The words of his mouth are transgression and deceit: he is not inclined to understand [how] to do good.
4 Alalapo kitandani, hupanga namna ya kutenda dhambi; yeye hukaa nje kwenye nja ya uovu; yeye hakatai uovu.
He devises iniquity on his bed; he gives himself to every evil way; and does not abhor evil.
5 Uaminifu wa agano lako, Yahwe, unafika mbinguni; uaminifu wako unafika mawinguni.
O Lord, thy mercy is in the heaven; and thy truth [reaches] to the clouds.
6 Haki yako ni kama milima ya Mungu; hukumu yako ni kama kina kirefu. Yahwe, wewe huwahifadhi wote wanadamu na wanyama.
Thy righteousness is as the mountains of God, thy judgments are as a great deep: O Lord, thou wilt preserve men and beasts.
7 Ni jinsi gani uaminifu wa aganao lako ni wa thamani, Mungu! Watu hukimbilia usalama chini ya uvuli wa mbawa zako.
How hast thou multiplied thy mercy, O God! so the children of men shall trust in the shelter of thy wings.
8 Nao watatoshelezwa tele na utajiri wa chakula nyumbani mwako; utawafanya wanywe kutoka katika mto wa baraka zako za thamani.
They shall be fully satisfied with the fatness of thine house; and thou shalt cause them to drink of the full stream of thy delights.
9 Kwa kuwa mna chemichemi ya uzima; na katika mwanga wako tutaiona nuru.
For with thee is the fountain of life: in thy light we shall see light.
10 Uupanue uaminifu wa agano lako kikamilifu kwa wale wanao kujua wewe, ulinzi wako uwe juu ya wanyoofu wa moyo.
Extend thy mercy to them that know thee; and thy righteousness to the upright in heart.
11 Usiuache mguu wa mwenye kiburi unisogelee. Usiiache mkono wa mwovu unitoweshe.
Let not the foot of pride come against me, and let not the hand of sinners move me.
12 Kule wafanyao maovu wameanguka; wameharibiwa hawawezi kuinuka.
There have all the workers of iniquity fallen: they are cast out, and shall not be able to stand.