< Zaburi 19 >

1 Kwa kiongozi wa muziki. Zaburi ya Daudi. Mbingu za tangaza utukufu wa Mungu, na mawingu hufanya kazi ya mikono yake ijulikane!
למנצח מזמור לדוד השמים מספרים כבוד אל ומעשה ידיו מגיד הרקיע׃
2 Siku hadi siku hotuba hutokea; usiku hadi usiku hufunua maarifa.
יום ליום יביע אמר ולילה ללילה יחוה דעת׃
3 Hakuna hotuba wala misemo; sauti zao hazisikiki.
אין אמר ואין דברים בלי נשמע קולם׃
4 Bali maneno yao husambaa nje duniani kote, na hotuba zao hata mwisho wa dunia. Yeye ametengeneza hema kwa ajili ya jua kati yao.
בכל הארץ יצא קום ובקצה תבל מליהם לשמש שם אהל בהם׃
5 Jua liko kama mfano wa bwana harusi akitokea chumbani kwake na kama mtu shujaa ambaye hushangila pale anapokimbia mbio zake.
והוא כחתן יצא מחפתו ישיש כגבור לרוץ ארח׃
6 Jua huchomoza kutokea upeo wa macho na likikatisha winguni kwenda jingine; hakuna chochote kinacho epuka joto lake.
מקצה השמים מוצאו ותקופתו על קצותם ואין נסתר מחמתו׃
7 Sheria ya Yahwe ni kamilifu, huokoa roho; ushuhuda wa Yahwe ni wa kuaminika, ukifanya hekima nyepesi.
תורת יהוה תמימה משיבת נפש עדות יהוה נאמנה מחכימת פתי׃
8 Maelekezo ya Yahwe ni ya hakika, yakiufanya moyo kuwa na furaha; amri ya Yahwe ni safi, ikileta mwanga kwenye macho yetu.
פקודי יהוה ישרים משמחי לב מצות יהוה ברה מאירת עינים׃
9 Hofu ya Yahwe ni safi, inadumu milele; amri za haki ya Yahwe ni za kweli na zote ni za hakika!
יראת יהוה טהורה עומדת לעד משפטי יהוה אמת צדקו יחדו׃
10 Nazo zina thamani kuliko dhahabu, nazo ni tamu kuliko asali na matone ya asali kutoka sega la asali (sega la nyuki).
הנחמדים מזהב ומפז רב ומתוקים מדבש ונפת צופים׃
11 Ndiyo, kupitia hizo mtumishi wako anaonywa; na katika kuziamini kuna thawabu.
גם עבדך נזהר בהם בשמרם עקב רב׃
12 Ni nani ambaye aweza kuyatambua makosa yake yote mwenyewe? Unitakase makosa yaliyo fichika.
שגיאות מי יבין מנסתרות נקני׃
13 Pia umuepushe mtumishi wako na dhambi za majivuno; usiziruhusu kunitawala. Ndipo nitakuwa mkamilifu, na mimi sitakuwa na hatia ya makosa mengi.
גם מזדים חשך עבדך אל ימשלו בי אז איתם ונקיתי מפשע רב׃
14 Maneno ya midomo yangu na mawazo ya moyo wangu nayakubalike machoni pako, ewe Yahwe, mwamba wangu na mkombozi wangu.
יהיו לרצון אמרי פי והגיון לבי לפניך יהוה צורי וגאלי׃

< Zaburi 19 >