< Zaburi 18 >

1 Nakupenda, Yahwe, nguvu yangu.
למנצח לעבד יהוה לדוד אשר דבר ליהוה את דברי השירה הזאת ביום הציל יהוה אותו מכף כל איביו ומיד שאול ויאמר ארחמך יהוה חזקי׃
2 Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, yeye ambaye aniwekae kweye usalama; yeye ni Mungu wangu, mwamba wangu; ninapata kimbilio kwake. Yeye ni ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, na ngome yangu.
יהוה סלעי ומצודתי ומפלטי אלי צורי אחסה בו מגני וקרן ישעי משגבי׃
3 Nitamuita Yahwe kwa sababu anastahili kusifiwa, na nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
מהלל אקרא יהוה ומן איבי אושע׃
4 Kamba za mauti zilinizunguka, na mafuriko yakimbiayo yalinielemea.
אפפוני חבלי מות ונחלי בליעל יבעתוני׃
5 Kamba za kuzimu zilinizunguka; mitego ya mauti ilininasa. (Sheol h7585)
חבלי שאול סבבוני קדמוני מוקשי מות׃ (Sheol h7585)
6 dhiki yangu nilimuita Yahwe; Niliita msaada kwa Mungu. Naye alisikia sauti yangu kutoka hekaluni mwake; kuita kwangu msaada kulienda mpaka uweponi mwake; na kuingia masikioni pake.
בצר לי אקרא יהוה ואל אלהי אשוע ישמע מהיכלו קולי ושועתי לפניו תבוא באזניו׃
7 Kisha nchi ikatikisika na kutetemeka; misingi ya milima pia ilitetemeka na kutikiswa kwa sababu Mungu alikuwa amekasirika.
ותגעש ותרעש הארץ ומוסדי הרים ירגזו ויתגעשו כי חרה לו׃
8 Moshi ulifuka kutoka kwenye pua zake, na moto mkali ulitokea mdomoni mwake. Makaa yaliwashwa kwa moto huo.
עלה עשן באפו ואש מפיו תאכל גחלים בערו ממנו׃
9 Yeye alizifunua mbingu na alishuka chini, na giza nene lilikuwa chini ya miguu yake.
ויט שמים וירד וערפל תחת רגליו׃
10 Alipanda kwenye kerubi na akaruka; alinyiririka kwenye mabawa ya upepo.
וירכב על כרוב ויעף וידא על כנפי רוח׃
11 Yahwe alilifanya giza kuwa hema likimzunguka yeye, wingu la mvua zito katika mbingu.
ישת חשך סתרו סביבותיו סכתו חשכת מים עבי שחקים׃
12 Mawe ya barafu na makaa ya moto yalianguka kutoka katika mwangaza kabla yake.
מנגה נגדו עביו עברו ברד וגחלי אש׃
13 Yahwe aliongea katika mbingu! Sauti ya aliye juu ilisikika.
וירעם בשמים יהוה ועליון יתן קלו ברד וגחלי אש׃
14 Yeye aliifyatua mishale yake na kuwatawanya adui zake; na radi nyingi zenye mwanga alizitawanya katika maeneo tofauti tofauti.
וישלח חציו ויפיצם וברקים רב ויהמם׃
15 Ndipo mifereji ya maji ilitokea; misingi ya dunia ikadhihirishwa kwa mlio wa pigo lako, Yahwe kwa sauti ya pumzi ya pua zako.
ויראו אפיקי מים ויגלו מוסדות תבל מגערתך יהוה מנשמת רוח אפך׃
16 Yeye alishuka chini kutokea juu; akanishikilia mimi! Akanivuta nje ya maji yafurikayo.
ישלח ממרום יקחני ימשני ממים רבים׃
17 Aliniokoa kutoka kwa maadui zangu wenye nguvu, kutoka kwa wale ambao walinichukia mimi, kwa kuwa walikuwa na nguvu sana kuliko mimi.
יצילני מאיבי עז ומשנאי כי אמצו ממני׃
18 Wao walikuja kinyume na mimi katika siku ile ya dhiki yangu lakini Mungu alikuwa msaada wangu!
יקדמוני ביום אידי ויהי יהוה למשען לי׃
19 Yeye aliniweka huru katika eneo pana la wazi; yeye aliniokoa kwa sababu alipenezwa nami.
ויוציאני למרחב יחלצני כי חפץ בי׃
20 Yahwe amenitunuku mimi kwa sababu ya haki yangu; yeye amenirejesha mimi kwa sababu mikono yangu ilikuwa misafi.
יגמלני יהוה כצדקי כבר ידי ישיב לי׃
21 Kwa kuwa nimezitunza njia za Yahwe na sijafanya uovu wa kumgeuka Mungu wangu.
כי שמרתי דרכי יהוה ולא רשעתי מאלהי׃
22 Kwa kuwa amri zake zote za haki zimekuwa mbele yangu; kama asemavyo, sijaenda kinyume nazo.
כי כל משפטיו לנגדי וחקתיו לא אסיר מני׃
23 Pia nimekuwa sina hatia mbele zake, na nimejiweka mwenyewe mbali na dhambi.
ואהי תמים עמו ואשתמר מעוני׃
24 Hivyo Yahwe amenirejesha kwa sababu ya haki yangu, na kwa sababu mikono yangu ilikuwa safi mbele ya macho yake.
וישב יהוה לי כצדקי כבר ידי לנגד עיניו׃
25 Kwa yeyote aliye mwaminifu, jionyeshe wenyewe kuwa mwaminifu; kwa mtu asiye na lawama, jionyeshe mwenyewe kuwa usiye na lawama.
עם חסיד תתחסד עם גבר תמים תתמם׃
26 Kwa yeyote aliye msafi, jionyeshe mwenyewe safi; bali ni mjanja kwa yeyote aliye geuzwa.
עם נבר תתברר ועם עקש תתפתל׃
27 Kwa kuwa wewe huwaokoa watu walio taabishwa, lakini wewe huwashusha chini wale wenye majivuno, yaani macho yaliyo jinua!
כי אתה עם עני תושיע ועינים רמות תשפיל׃
28 Kwa kuwa wewe huipa mwanga taa yangu; Yahwe Mungu wangu hutia mwanga giza langu.
כי אתה תאיר נרי יהוה אלהי יגיה חשכי׃
29 Kwa kuwa kwa kupitia wewe ninaweza kuruka juu ya kiwazo kilichowekwa; kupitia Mungu ninaweza kuruka juu ya ukuta.
כי בך ארץ גדוד ובאלהי אדלג שור׃
30 Kama kwa Mungu: njia yake ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi! Yeye ni ngao kwa yeyote anaye kimbilia katika yeye.
האל תמים דרכו אמרת יהוה צרופה מגן הוא לכל החסים בו׃
31 Kwa kuwa nani ni Mungu ispokuwa Yahwe? Nani ndiye mwamba ispokuwa Mungu wetu?
כי מי אלוה מבלעדי יהוה ומי צור זולתי אלהינו׃
32 Ni Mungu anitiaye nguvu ndani yangu kama vile mkanda, ambaye humweka mtu mwenye lawama katika njia yake.
האל המאזרני חיל ויתן תמים דרכי׃
33 Yeye hunifanya miguu yangu kuwa myepesi kama mbawala na kuniweka mahali pa juu!
משוה רגלי כאילות ועל במתי יעמידני׃
34 Yeye hufunza viganja vyangu kwa ajili ya vita na mikono yangu kupiga upinde wa shaba.
מלמד ידי למלחמה ונחתה קשת נחושה זרועתי׃
35 Wewe umenipa mimi ngao ya wokovu. Mkono wako wa kuume umenisaidia, na neema yako imenifanya kuwa mkubwa.
ותתן לי מגן ישעך וימינך תסעדני וענותך תרבני׃
36 Wewe umetengeneza nafasi pana kwa ajili ya miguu yangu ili miguu yangu isiteleze.
תרחיב צעדי תחתי ולא מעדו קרסלי׃
37 Ninawashawishi adui zangu na kuwakamata; nami sikurudi nyuma mpaka walipo haribiwa.
ארדוף אויבי ואשיגם ולא אשוב עד כלותם׃
38 Niliwashambulia hata hawakuweza kuamka; nao wameangukia chini ya miguu yangu.
אמחצם ולא יכלו קום יפלו תחת רגלי׃
39 Kwa kuwa unanitia nguvu kama mshipi kwa ajili ya vita; wewe unawaweka chini yangu wale ambao wanainuka kinyume na mimi.
ותאזרני חיל למלחמה תכריע קמי תחתי׃
40 Wewe ulinipa visogo vya maadui zangu; niliwaagamiza wale walio nichukia.
ואיבי נתתה לי ערף ומשנאי אצמיתם׃
41 Wao waliita msaada lakini hakuna aliye wasaidia; walimuita Yahwe, lakini hakuwaitikia.
ישועו ואין מושיע על יהוה ולא ענם׃
42 Niliwapiga wao katika vipande vidogo vidogo kama vile vumbi mbele ya upepo; niliwatupa nje kama udongo mtaani.
ואשחקם כעפר על פני רוח כטיט חוצות אריקם׃
43 Wewe uliniokoa mimi kutoka katika migogoro ya watu. wewe umenifanya kichwa juu ya mataifa. Watu ambao sikuwahi kuwafahamu huntumikia.
תפלטני מריבי עם תשימני לראש גוים עם לא ידעתי יעבדוני׃
44 Pindi tu waliposikia kuhusu mimi, wao walinitii; wageni walilazimishwa kunisujudu.
לשמע אזן ישמעו לי בני נכר יכחשו לי׃
45 Wageni walitoka kwenye ngome yao wakitetemeka.
בני נכר יבלו ויחרגו ממסגרותיהם׃
46 Yahwe anaishi; mwamba wangu usifiwe. Ainuliwe Mungu wa wokovu wangu.
חי יהוה וברוך צורי וירום אלוהי ישעי׃
47 Yeye ni Mungu ambaye hutelekeza visasi kwa ajili yangu, ambaye huwatiisha mataifa chini yangu.
האל הנותן נקמות לי וידבר עמים תחתי׃
48 Nimewekwa huru kutoka kwa adui zangu! wewe uliniinua juu ya wale walioinuka kunyume na mimi! Wewe uliniokoa kutoka kwa watu wenye vurugu.
מפלטי מאיבי אף מן קמי תרוממני מאיש חמס תצילני׃
49 Kwa hiyo nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya mataifa; Nitaliimbia sifa jina lako!
על כן אודך בגוים יהוה ולשמך אזמרה׃
50 Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na yeye huonyesha uaminifu wa agano lake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na ukoo wake milele.
מגדל ישועות מלכו ועשה חסד למשיחו לדוד ולזרעו עד עולם׃

< Zaburi 18 >