< Zaburi 148 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni Yahwe, ninyi mlio katika mbingu; msifuni yeye, ninyi mlio juu.
alleluia laudate Dominum de caelis laudate eum in excelsis
2 Msifuni yeye, enyi malaika wake wote; msifuni yeye, majeshi ya malaika wake wote.
laudate eum omnes angeli eius laudate eum omnes virtutes eius
3 Msifuni yeye, enyi jua na mwezi; msifuni yeye, nyota zote zing'aazo.
laudate eum sol et luna laudate eum omnes stellae et lumen
4 Msifuni yeye, enyi mbingu zilizo juu zaidi na maji yaliyo juu ya anga.
laudate eum caeli caelorum et aqua quae super caelum est
5 Na vilisifu jina la Yahwe, maana aliamuru, navyo vikaumbwa.
laudent nomen Domini quia ipse dixit et facta sunt ipse mandavit et creata sunt
6 Pia ameviimrisha milele na milele; naye alitoa amri ambayo haitabadilika.
statuit ea in saeculum et in saeculum saeculi praeceptum posuit et non praeteribit
7 Msifuni yeye kutoka nchi, ninyi viumbe wa baharini na viumbe vyote katika kina cha bahari,
laudate Dominum de terra dracones et omnes abyssi
8 moto na mvua ya mawe, theluji na mawingu, upepo wa dhoruba ukitimiza neno lake.
ignis grando nix glacies spiritus procellarum quae faciunt verbum eius
9 Msifuni yeye, enyi milima na vilima, miti ya matunda na mierezi yote,
montes et omnes colles ligna fructifera et omnes cedri
10 wanyama pori na wanyama wafugwao, viumbe vitambaavyo na ndege.
bestiae et universa pecora serpentes et volucres pinnatae
11 Msifuni Yahwe, wafalme wa nchi na mataifa yote, wakuu na watawala wote wa nchi,
reges terrae et omnes populi principes et omnes iudices terrae
12 wote vijana wa kiume na vijana wa kike, wazee na watoto.
iuvenes et virgines senes cum iunioribus laudent nomen Domini
13 Na walisifu jina la Yahwe, kwa kuwa jina lake pekee limetukuka na utukufu wake umeongezwa juu ya nchi na mbingu.
quia exaltatum est nomen eius solius
14 Naye ameyainua mapembe ya watu wake kwa ajili ya sifa kutoka kwa waaminifu wake wote, Waisraeli, watu wa karibu naye. Msifuni Yahwe.
confessio eius super caelum et terram et exaltabit cornu populi sui hymnus omnibus sanctis eius filiis Israhel populo adpropinquanti sibi

< Zaburi 148 >