< Zaburi 146 >

1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
Praise YAH! Praise, O my soul, YHWH.
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
I praise YHWH during my life, I sing praise to my God while I exist.
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
Do not trust in princes—in a son of man, For he has no deliverance.
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
His spirit goes forth, he returns to his earth, In that day his thoughts have perished.
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
O the blessedness of him Who has the God of Jacob for his help, His hope [is] on his God YHWH,
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
Making the heavens and earth, The sea and all that [is] in them, Who is keeping truth for all time,
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
Doing judgment for the oppressed, Giving bread to the hungry.
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
YHWH is loosing the prisoners, YHWH is opening (the eyes of) the blind, YHWH is raising the bowed down, YHWH is loving the righteous,
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
YHWH is preserving the strangers, He causes the fatherless and widow to stand, And He turns the way of the wicked upside down.
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
YHWH reigns for all time, Your God, O Zion, to generation and generation, Praise YAH!

< Zaburi 146 >