< Zaburi 140 >

1 Yahwe, uniokoe dhidi ya waovu; unikinge dhidi ya watu wenye vurugu.
[Psalm lal David] LEUM GOD, moliyula liki mwet koluk; Langoeyula liki mwet sulallal.
2 Wao wanapanga uovu mioyoni mwao; wanasababisha mapigano kila siku.
Pacl nukewa elos pwapa in oru ma koluk; Elos purakak akukuin in pacl e nukewa.
3 Ndimi zao zinajeruhi kama nyoka; sumu ya fira imo midomoni mwao. (Selah)
Lohulos oana serpent sulallal; Kas lalos oana pwasin ke wet cobra.
4 Ee Yahwe, unilinde dhidi ya mikono ya waovu; unikinge na vurugu za watu wanaopanga kuniangusha.
LEUM GOD, moliyula liki ku lun mwet koluk; Langoeyula liki mwet sulallal Su kena tuh nga in ikori.
5 Wenye majivuno wameweka mtego kwa ajili yangu; wameeneza nyavu; wameweka kitanzi kwa ajili yangu. (Selah)
Mwet filang elos kena sruokyuwi; Elos oakiya mwe kwasrip lalos, Ac filiya sruhf pe inkanek uh in sruokyu.
6 Nilimwambia Yahwe, “Wewe ni Mungu wangu; usikie kilio changu unihurumie.”
Nga fahk nu sin LEUM GOD, “Kom God luk.” LEUM GOD, porongeyu ke nga pang in suk kasru sum!
7 Ee Yahwe, Bwana wangu, wewe ni mwenye nguvu uwezaye kuniokoa; hunifunika ngao kichwa changu siku ya vita.
LEUM GOD Fulatlana luk, ke ku lom Kom langoeyula in pacl in mweun.
8 Ee Yahwe, usiyatimize matakwa ya waovu; usiruhusu njama zao kufanikiwa. (Selah)
LEUM GOD, nikmet sang nu sin mwet koluk ma lungse lalos; Nikmet akfahsrye pwapa koluk lalos.
9 Wale wanao nizunguka huinua vichwa vyao; madhara ya midomo yao wenyewe na yawafunike.
Nikmet sang kutangla nu sin mwet lokoalok luk, Lela tuh ma koluk elos akoo nu sik in folokyang nu faclos.
10 Makaa ya moto na yawaangukie; uwatupe motoni, kwenye shimo refu, wasiweze kuinuka tena.
Lela tuh mulut firir in putati faclos; Lela in sisila elos nu in luf loal ma elos tia ku in sifil illa liki.
11 Watu wenye ndimi na wasifanywe salama juu ya nchi; na uovu umuwinde kumpiga mtu mwenye vurugu mpaka afe.
Lela mwet su kinauk kas sutuu ke mwet saya in tia akilenyuk, A ma koluk in ukweya na mwet sulallal ac kunauselosla.
12 Ninajua kuwa Yahwe atahukumu kwa haki walioteswa, na kuwa atawapa haki wahitaji.
LEUM GOD, nga etu lah kom loango sripa lun mwet sukasrup Ac orala nununku suwohs nu sin mwet enenu.
13 Hakika watu wenye haki watalishukuru jina lako; watu wanyoofu wataishi uweponi mwako.
Pwayena lah mwet suwoswos elos fah kaksakin kom. Elos fah muta ye motom.

< Zaburi 140 >