< Zaburi 124 >
1 “Kama Yahwe asingekuwa upande wetu,” Israeli na aseme sasa,
若不是上主保佑我們,唯願以色列子民再說:
2 “Kama asingekuwa Yahwe ambaye alikuwa upande wetu wakati watu walipoinuka dhidi yetu,
若不是上主保佑我們,當世人起來攻擊我們,
3 basi wangekuwa wametumeza tungali hai hasira yao lipozidi dhidi yetu.
並向我們發洩怒火時,必會活活將我們舌食。
4 Maji yangetugharikisha; mto ungetuzidia.
就像淹沒我們的水禍,流過我們頭頸的洪波。
5 Kisha maji yafurikayo yangetuzamisha.”
又像洶湧澎湃的狂浪,早已將我們淹沒滅亡。
6 Atukuzwe Yahwe, ambaye hajaruhusu tuwe mawindo kwa meno yao.
讚美上主,他沒有將我們拋出,使我們做成他爪牙的獵物;
7 Tumetoroka kama ndege mtegoni mwa wawindaji; mtego umevunjika, nasi tumetoroka.
我們像掙脫獵人羅網的小鳥,羅網扯破了,我們自然逃掉。
8 Msaada wetu uko katika Yahwe, aliyeziumba mbingu na nchi.
我們的救助是仰賴上主的名,上天和下地都是由他所造成。